Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

WATANZANIA wanaheshima ndio maana WANA TABIA MBAYA!:-(

>> Wednesday, December 02, 2009

Swali:

  • Unafikiri kwa sababu ya HESHIMA ZAKO huendekezi na kuchangia kushamiri kwa tabia MBAYA ?
  • Kwa heshima si unajua MKUBWA/umheshimuye akijamba ni TABIA NZURI kujifanya hujastukia mtu kajamba kwa kutobana AU KUPEPEA pua?




Katika TANZANIA ukichunguza :


Heshima imekuwa ni kipingamizi cha kukosoa .

Na kwa kuwa KUNA WENYE HESHIMA unaweza usiwasikie wakutukanao wakikutukana na kukufanya ufikiri hutukanwi.

Kwa heshima mpaka mambo yaathiriyo JAMII hayaongelewi kwa kuwa kwa mheshimiwa ni MATUSI KUONGELEA ingawa wayafanyayo ni waitwao WAHESHIMIWA.

NA kwa kifupi;...
- niliyonong'oneza hapo juu NI TABIA MBAYA!:-(




Na maana a.k.a FAFANUO fafa:

Kwa kuwa WATANZANIA twaheshimu wakubwa, ....

....WAKUBWA hawakemewi kwa kuwa jambo hilo LAKUKEMEA HATA UZEMBE WA WAKUBWA linatiwa UBUBU na MILA na DESTURI zitawalazo jamii karibu za MAKABILA yote ya TANZANIA liwapalo WAKUBWA SILAHA ya KUKUTISHIA kukulaani kwa tabia MBAYA kwa kudiriki kuwaletea KIBEZI magwiji waliokuzidi UMRI au hata tu cheo.:-(

Kumbuka kuna MILA na DESTURI ambazo Watanzania wengi wametoka ambazo MKUBWA kama unaheshima HAKOSOLEKI.



Kumbuka tu KISAIKOLOJIA umpaye SHIKAMOO a.k.a[ niko chini ya miguu yako] kwa KUMHESHIMU KIKWELI , kwa vyovyote utafsirivyo, KWA HESHIMA HIYO ushajiweka katika mazingira ambayo NI LAZIMA uwe mtaalamu SANA ILIKUWEZA KUJIENGUA kutoka katika shinikizo la uzito wa SHIKAMOO kumkosoa ULIYEMPA SHIKAMOO, kumuomba avae kondomu kama anataka kucheza bila soksi, KUMUULIZA kwanini ni FISADI au tu kumnyima jicho au tigo kwa kuwa MHESHIMIWA umheshimuye ndio atakacho, - KWA KUWA kumbuka asilimia KUBWA ya HESHIMA ambazo MILA na DESTURI za KITANZANIA zimewajengea WATANZANIA ni HESHIMA ZA WOGA.:-(



Kumbuka pia,...
.... wengi wenye TABIA MBAYA uwajuao , TABIA HIZO wamejifunza kutoka kwa wawaheshimuo.:-(

Swali:
  • Weye Mlevi, Mvizia mademu Kanisani na mlamba UGORO unafikiri ulijifunza tabia hiyo kutoka kwa nani?

Tukiachana na hilo:

Kwa WATANZANIA, kwa kipingamizi cha heshima,...

... ni vigumu kukuta hata vitendo vya unyumba vinaongelewa wazi na wajiitao WANAHESHIMA hata kwa manufaa ya watakao kujifunza kwa usahihi KUPEKECHA kiheshima.

Na cha kusikitisha shule za UNYAGO na JANDO hazina nguvu kama za zamani NA LABDA HILO ni kama tu kukwepa kukubali UNYAGO na JANDO havijafa kabisa wakati elimu mpya iendekezwayo haitilii maanani yaliyokuwa yanafunzwa na Unyago na JANDO kwa kuwa waheshimiwa huiga na kuacha yote ya zamani kikitokea kipya WAKIHESHIMUCHO - na ndio maana mpaka VIATU VYA MITUMBA vimeua biashara ya VIATU VYA MCHAGA KAJITAHIDI kabla MCHAGA YOYOTE FUNDI VIATU kufanikiwa kuanzisha KIWANDA cha viatu ambacho BRANDI ni MCHAGA KAJITAHIDI - made in TANZANIA viuzwavyo CHINA. :-(


Na WATANZANIA wenye heshima na wadaio kutunza TAMADUNI ,mila na DESTURI za KITANZANIA ,kwa kuwa mstari wa mbele kwa KURINGISHIA TABIA ZAO NZURI wengi wao wanalazimika KUZIONEA AIBU tamaduni ZAO ambazo vibwaya na NGOMA ZA KIENYEJI ruksa,.....

.... na wanaweza kukufurumusha MAENEO kwa kuvitetea VIBWAYA kama vazi la heshima na MDUNDIKO kama MAGOMA MOTO kwa kuwa tu wanavionea aibu na kwa TABIA MBAYA hiyo HAWAKIRI kuwa TANZANIA na JOTO LOTE VIBWAYA NI BOMBA kuliko SUTI ya MUITALIANO na WANALAZIMIKA KUSHANGILIA suruali na kanzu KWA KUWA kuna uwezekano wawazimiao KIUTAMADUNI na MPAKA kiuwao UWEUPE PEE kama KIAZI cha CHIPSI ,....

... vazi LAO la heshima ni KANZU bila chupi au SUTI na CHUPI ambayo itiavyo joto sehemu za nyeti UKIWA Dar-es-salam mpaka DAKTARI anaweza kukushauri nyeti uipungishe hewa mara kwa mara ipumue na kuondoa harufu ya uvundovundo,...


- yote ikiwa ni katika kujaribu kuwa na kujisikia ni WAHESHIMIWA kama WAKOLONI walioleta chupi wazipendazo TANZANIA ,...

....- yote hayo kusababisha WANAVIITA tu VIBWAYA na NGOMA ZA KIENYEJI ni TABIA au tamaduni, mila na desturi MBAYA kwa kuwa badala ya kuviimarisha vibwaya vije na dizaini tofauti tofauti au NGOMA ZA KIENYEJI kuafuta staili bomba ya kuwasilishwa ,.....

....KIHESHIMA WAMEVIACHA kwa kuwa:

-WAHESHIMIWA WANAAIBU NA VYA KWAO na hiyo ni TABIA MBAYA.:-(


Na kunauwezekano kabisa:
....HESHIMA na madai ya TABIA NZURI inaweza ikawa tu ni silaha ya kujikinga na ni nini TUNAVIONEA AIBU.

Na labda,....
.....tuvioneavyo aibu mara nyingi wala sio SHENZI bali ni vitu ambavyo tumejifunza kuvionea aibu kwa kuwa watu wengine WASIOVIJUA VITU VYETU ndio wanafanya tuvionee aibu kwa UKOSEFU wa KUJIAMINI.



NAKATIZA WAZO!:-(
Swali:
  • Unafikiri ustaarabu wa UMMA na KIJIKO unahitajika kwenye UGALI wakati wenye kudhani katika kula USTAARABU unahitaji UMMA na KIJIKO hawali UGALI?
  • Unafikiri ni mara ngapi umeshuhudia MHESHIMIWA kajamba na kwa tabia nzuri na heshima HUKUBANA PUA?


Hebu Lionel Richie alete kitu -STUCK on YOU na kubadili hali ya hewa.

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP