Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Labda VITA ya MALAYA ilishaisha wakati MALAYA WANASUTANA na mshindi wa UPASHKUNA alishapatikana kabla ya KUBWENGANA!:-(

>> Saturday, February 06, 2010

Kuna baadhi ya MAPIGANO YASHUHUDIWAYO ambayo hufanyika tu,...
.....ili tu kukamilisha KUJISHEBEDUA kwa kuwa vita ilishaisha na aliyeshindwa alishajua kashindwa WAKATI anafunuliwa TU sketi na KUSHIKIWA kiuno AKISUTWA.


Na aletaye VITA ya uso kwa uso ili AKUUMIZE HUKU akikuangalia usoni KATIKA KUJIAMINI NDIO ANAKUFUNDISHA ADABU kwa KUKUBWENGA kwa kuwa ANAAMINI wewe ni MALAYA kwa kuwa TU ulihitaji KUWA NA UHAKIKA kwa kuonja VIMILIKIWAVYO na wengine vifanyavyo waonekane kama wanafaidi sana KULIKO WEWE hata kama ni vile ujuavyo kwa vyovyote kunasiku vinanuka mkojo tu,...
.....aweza kuwa anahangaika na VITA ulioishindwa ,ULISHA ITUBU TAYARI KWA PADRE na MUNGU , ulisha JILAUMU au tu uliyofikia HITIMISHO ZAMANI kuwa yamekushinda na umekoma kuonja vya watu ambavyo labda wala havikukunogea na ULISHA KOMA kwa tu KUTETWA.:-(

Swali:
  • AU?
  • Kwani WAKATI UMEUSHINDWA MTIHANI hujui UMESHINDWA mtihani mpaka ukabiliane na KURUDISHIWA ulioushindwa mtihani?
  • Kwani kuna jipya ujifunzalo kwa kurudishiwa matokeo ya MTIHANI ULIOFELi ambalo hujifunzi wakati unafeli MTIHANI?







Na labda,....





VITA haihitaji silaha,....
.... kwa kuwa matumizi ya silaha sio vita.

Na wakati MAPIGANO yanaendelea yatumiayo SILAHA,....
.... labda ilishakwisha VITA.:-(

Swali:
  • Si unakumbuka wapiganao VITA huwa walishaweka wazi ni nini wanakipigania?
  • Unauhakika MAPIGANO ni vita?
  • Unauhakika VITA haipiganiwi UBONGONI na ashindwaye hushindwa tu kwa afikiriavyo UBONGONI?
  • Unafikiri kwa kumbwenga MTU na ukashinda kwa kumtoa ngeu maana yake umembadilisha mawazo?
  • Si unakumbuka matumizi ya BUNDUKI katika vita yalisababishwa na aliyekuwa anashindwa kupigana na kushinda kwa mapanga na mikuki kutunza AAMINICHO kustukia mwenye misuli kilaini anadondoshwa vitani na GOBOLE?
  • Si unajua mwenye bonge la misuli kuna vita azishindwazo hata kabla ya MAPIGANO kisa silaha ya ADUI itumikayo ni sauti nyororo na macho kama BUNDI ya kurembua?

NI wazo tu hili MHESHIMIWA!

JUMAMOSI NJEMA!



Au ngojea The ROOTS warudie -Next movement na Pussy Galore(sex in consumerism)



Au tu twende Senegal Baaba Maal arudie tu kitu- Yela

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP