Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

TEKNOLOJIA IPO na katika ulimwengu wa FACEBOOK ,- kuna UJUMBE na status : ``Niko MSALANI!´´

>> Tuesday, February 16, 2010

 Katika ulimwengu wa  GBuzz,....
... MTONYO waweza kuwa ni  ,....
- ``Nimeenda KUCHIMBA dawa!´´


Katika  ulimwengu wa TWITTER ,....
... UJUMBE waweza kuwa ni ; .....
-``Niko CHOONI!´´

Na katika ulimwengu ambao TEKINOLOJIA  ni  ala ya NGOMA katika enzi  ZETU  za MKOLONI,...

..... UJUMBE;  Gdu du dududu du ,....

.. tafsiri yaweza kuwa ilikuwa ni ;...
-`` MKOLONI anakuja chimba choo kama hutaki kuchapwa HAMSA ishirini kwa kwenda haja  vichakani!``


Swali:
  • Weye uliyebobea kwenye INTERNET na  E-mail zako , UNAKUMBUKA  jinsi ya kuandika BARUA lakini?
  • Si unakumbuka hata teknologia ibadilike vipi haisaidii kutengeneza UJUMBE na ni MTU mwenyewe katika tumizi la tekinolojia  aamuaye ujumbe autumao  kwa   wasio na CHAKULA kuwa ni jinsi  CHOO cha kukaa  kisafi kiongezevyo upotezaji wa muda wa watu CHOONI ?

Kumbukumbu:


Kuna kipindi barua ya MTU ya kwanza kwa MPENZI MLENGWA  kutokana na elimu za vijiwe vya kitoto ,...
...ilifanikiwa kuchorwa  mpaka MAUA na kunyunyiziwa poda KWA WENGINE  huku  yote hayo MTU kiroho kikimdunda kutokana na UZITO wa  ujumbe ulioandikwa wa;...
.... ``Helo ,  mimi nakupenda na NAOMBA URAFIKI!``


Siku hizi MTU ZILIZOPIGA UMRI zinaweza onea wivu wale ambao WAMEZALIWA wakati  maswala yote ni TEXT MESEJI  za simu na MWALIMU ni TELEVISHENI  ;....

.....halafu UJUMBE wa mtafuta MPENZI mwenyewe  BADO ni;....
... ``Helo , kunakitu nataka kukuambia NI DIP basi simu yangu haina hela!´´


Swali:
  • Unafikiri tekinolojia hizi mpya usipoangalia hazikuondoi hata ujuzi wa kupiga mluzi ili kuita MTU?
  • Unafikiri pamoja na HIZI teknolojia kurahisisha upataji wa habari ukweli wenyewe si kwamba habari utakazo kuzipata ushazitengenezea mipaka na kwa mpenda habari za choo asilimia kubwa ya habari na ujumbe apatao ni wakuhusiana na CHOO kama tu mpenda BONGO FLEVA miziki kibao ailengayo na kuisikiliza isivyokuwa ni TAARABU?
  • Si unakumbuka ni wewe na sio TEKNOLOJIA itoayo na kupokea UJUMBE na hata kwa kutumia tekinolojia gani bado BINADAMU atafariki akiwa amefanikiwa kujua tu machache katika duniahii yenye mambo zaidi ya KIDUCHU kilengwacho na mtu?



Ndio,....
... kuna wakati madhumuni ya BARUA yalikuwa ni KUKUJULIA hali.

Na wakati tunaishi katika ulimwengu ambao MADHUMUNI ya kuwa ANONYMOUS MTANDAONI yanaweza kuwa ni KUTUKANA MTU, ...

.....tukumbuke tu TEKINOLOJIA  haiongezi idadi ya UJUMBE zaidi ya KUFIKISHA tu HATA UJINGA kama UJUMBE ,....

....na kitakiwacho KUJULIKANA ni kwamba UJUMBE upo tu kama unania ya kuupata na matumizi yako ya TEKNOLOJIA yaweza kuwa ndio kwanza yanakusaidia TU kuchanganyikiwa kama si mahiri wa KUBAINI ni  nini unakihitaji sasa hivi  kwa KUKULUNDIKIA MASWALA mpaka ya ambacho kingekuwa KWAKO ni  muhimu UKIBALEHE  , na kusababisha MWINGINE akipate kabla hata hajavunja UNGO.:-(






NI HILO TU na ni wazo tu MHESHIMIWA!




Hebu Spike Lee joints ituletee  Mo' BETTER BLUES ili akina Denzel Washington , Wesley Snipes,.... wamwage- DA BLUES



Au tu Tabi BONNEY arudie- YOU



Au tu TABI BONNEY aendelee tu kubadili kwa -The Pocket

3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Fadhy Mtanga 7:26 am  

Mtakatifu Simon leo umeniacha kinywa wazi. Umenikumbusha enzi zile nasoma nilikuwa naenda kutega mingo karibu na geti nikivizia atoke ili nimkonyeze na kuomba hako kaurafiki. Ama nategea katoto kapite nakatuma huku nikikashawishi kasinitaje jina. Kaseme tu "nanihino kuna mtu anakuita pale!" mwenyewe anaelewa ni mchizeni wake anamwita. Anazuga na ndoo kama anaenda bombani kuteka maji.
Sasa teknolojia imerahisisha kazi. Unatext tu "tukutane pale pale uchochoroni sasa mbili giza likishaingia"
Mtoto anategea wazazi wanaangalia ITV habari ye anazuga anamwaga takataka kumbe umebana uchochoroni ukiwa na hamu japo ya ulimi.
Duh!
Imebaki historia.

Ila kweli hao akina 'anonymous' hao kwanini wafiche majina?

Yasinta Ngonyani 4:57 pm  

Mtatifu Simo na Askofu Fadhi duh! ninyi kumbe mlianza utundu mapema hivi. Nashangaa huo Utakatifu na Uaskofi sijui mmeupataje..:-)

EDWIN NDAKI (EDO) 1:32 pm  

mmmh! tutafika tu ..ndio maana Dr Remmy aliimba kwenye moja nyimbo zake kipenda roho ndio yale yale ya kila moja na KWELI na UONGO wake

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP