Binadamu huhitaji kitu kimoja tu awe MAARUFU au KUFANYA BINADAMU WENGINE wamuone WAMAANA au mjinga kwa mbaaali!:-(
>> Friday, November 20, 2009
Kumbuka wote uwajuao au kuwasikia kwa kufanikiwa au tu MIAKILI hata kama walifanya  mambo ELFU ,....
... sifazao zifanyazo uwajue/KUWASIKIA/ au hata kuwazimia mara nyingi ziko kwenye kitu KIMOJA TU walichowahifanya.
Na utaahira wa TAAHIRA wa binadamu adhaniwaye ni taahira au ana kichaa na MAELFU,...
.... hugeuzwa tafsiri na MAMILIONI mara moja TU NA  kuwa ni AKILI NYINGI  ndio maana KIJEBA HAELEWEKI , akigundua kitu kimoja tu ambacho wenye akili kwa akili zao WALISHINDWA KUFANYA:-(
Na kwa bahati mbaya UKUBWA wa kitu kimoja HAUNA KIPIMO maalumu au kipimo kimoja MAARUFU ,...
... kwa kuwa KIMFANYACHO MTU AWE MAARUFU inaweza tu ikawa ni  -Goli moja tu lililomfanya mtu awe BABA ya Obama  na kuwa maarufu kwa hilo au Goli MOJA  lililo sababisha Yanga imfunge SIMBA na kumfanya mtu aonekane muhimu kwa washabiki wa Yanga kwa hilo,  uvumbuzi mmoja kama tu ambao ulianzisha EINSTEIN ajulikane DUNIA NZIMA  kwa miakili hivyo au hata malezi ya wazazi wako KWA STAILI MOJA  tu isababishayo WOTE TUDHANIE  wazazi wa Venus WILLIAMS na Serena ni kiboko kwa kuwa wamelea mabinti WAKAWEZA  kupiga kimpira kinachodundadunda na KUSABABISHA WATU WAWAZIMIE KULIKO aliyegundua CHLOROKWINI  ingawa labda walitumia zaidi muda kuwafunda MENGI zaidi ambayo hatuyaoni  ambayo ndio siri halisi ya mafanikio yao ingawa hutuoni wakiyafanya.:-(
Ndio ,...
.... chaajabu LABDA PIA ni kitu kimoja tu inahitajika USIJUE ili kukufanya UWE MAARUFU  tusahau UNAJUA KWELI  HESABU na ni KUTOONGEA VIZURI  tu ndio kunafanya  DUNIA NZIMA tuamini wewe ni RAIS  GEORGE BUSH wa akili wastani wakati labda weye JINIASI na UNABOMBA LA MIAKILI  tu  kwa tusichoshuhudia UKIFANYA.:-(Swali:
- Si unakumbuka ni umaarufu wa kitu kimoja TU KIBAYA kwa mtu mmoja unaweza kusahaulisha watu kuwa kwa mengi wewe ni BONGE LA MTU MZURI kwa wengi?
- Unafikiri tabia za binadamu za KWA KAWAIDA KUZIMIA mtu kwa kitu kimoja tu na kumuona Bonge la David Beckham kwa kila kitu INGAWA AJUACHO AFANYACHO DAVID BECKHAM NI KIMOJA ni mjanja ,wakati dunia yenyewe ina mengi na YAHITAJI MENGI na katika hayo yote labda la David Beckham NDILO si la muhimu na ni la kisenge kwa asiye msenge?
- Ukifikiria sana si unaweza kugundua mpaka kitu kimoja tu KWAKO kilichomfanya mpaka Yesu kawa bonge la Supa STAA a.k.a Bonge la maarufu/YUKO JUU?
KUMBUKA hili NI WAZO TU MHESHIMIWA!
Tuondokane na wazo kwa msaada wa dada kutoka GUINEA kwa jina ALAMA KANTE alainishe kwa ndude-DIS MOI
Au tu KEKELE na MBILIA BEL walete-Yo Odeconer
 
  
 Posts
Posts
 
 




0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:
Post a Comment