Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kuhusu kimpandishacho Maimuna NYEGE ya UDAKU!

>> Friday, November 27, 2009

[Tahadhari: Wazo limepinda !:-(]

Meseji kutoka kwa MAIMUNA:

''Aku babu wee! MAKALA ZENU ZA UCHAMBUZI huko huko MCHELE NICHAMBUE halafu wataka tena mpaka FIKIRA nazo nichambue? Koma babu wee KOMA na kama unantaka si sema tu?´´mwisho wa nukuu.

...................................._________________.................................





Samahani naanza tararila hii UPYA!:-(


MAISHANI YAPO AMBAYO NI MUHIMU KWETU ili tuishi na KWA WENGINE UMUHIMU NI MPAKA kujaribu KUJUA na KUCHAMBUA kuwa labda YESU havai chupi.[Tahadhari: kama unakwazika na jina YESU kumbuka kwa Waspanish Yesu a.k.a JESUS ni jina la mtu yoyote yule na huyu ni Mpuetoriko:-(]


NDIO!

Kwa WENGINE kujua YASIYOWAHUSU ni muhimu kama TU wale wasioendekeza ya wengine wachokonoavyo YAO WENYEWE ili kujijua zaidi, - kitu ambacho kwa kawaida huhitaji MAISHA YOTE kama ukikumbuka kuwa yako MWENYEWE ya JANA, si YA LEO wala KESHO:-(


NA, kitu kidhaniwacho ni muhimu KWA MTU , kwa kawaida AIDIA NZIMA ni kitu cha ajabu sana hasa ukianza kufananisha ni kitu gani kwako ni MUHIMU na kusahau watu wengine sio WEWE.:-(


Ila kinachoudhi ni kwamba kitu cha muhimu kwako kinaweza kuwa ni kipoteza muda kwa wengine na kiwapotezeacho muda wengine kikawa ndio unauhakika ni muhimu na unaona mpaka jinsi wasiostukia umuhimu wake wanavyopotea au KUINGIA MKENGE .:-(


NA CHAKUSIKITISHA ZAIDI ni kwamba ingawa UDAKU LABDA ni muhimu KWA KILA MTU ,...
....ila UDAKU UKIZIDI inakuwa sio tena BURUDANI,....
....NA kwa hili na MAANISHA kuwa ukizidisha UDAKU,- UDAKU huachakuwa burudani NA kugeuka SHULE.

Na katika shule ya UDAKU kirahisi wakati KICHWA NI MUHIMU unaweza kujikuta unafikiria TAKO,....
....Nikiwa na maana;.....

...katika kubobea katika UDAKU matokeo yake swala la'' HIVI jirani ni kweli TAKO LIMEKUA'' linaweza chukua nafasi ya-'' hivi tufanye nini ili MTAANI kwetu pawe pasafi watoto wetu wasiugue'' katika maisha ya Binti Kadoda.


Na swala la ''Hivi Mheshimiwa ni kweli anatoa jicho a.k.a tigo'' linaweza likawa ni swala lichukualo nafasi MAWAZONI ya ''Hivi kama Rais wa Brazil LULA na James Brown walianzia kupiga kiwi viatu vya watu Mtaani NAKUFIKIA MAFANIKIO WALIYOFIKIA ,hivi kweli mimi siwezi kwenda mbali kwa kuwa kwanza HAPA NILIPO na taaluma KALI na kubwa kuliko ya kupiga kiwi viatu!'' kwa Kijeba mtaaani ambaye CHANZO CHA HEKIMA ni gazeti la UDAKU.


Samahani ngojea nirudi kwenye SWALA la nyege za UDAKU za MAIMUNA!:-(

Sababu za nyege za udaku ni nyingi NDIO MAANA kuanzia PROFESA, Meneja wa CHOO cha STENDI na shoga ambaye taaluma yake ni kulala chali Bwana akirudi kutoka KAZINI wananyegeleshwa nao.:-(
Lakini ukifuatilia utakuta :

1.Udaku NI kujitafuta wajijuavyo wapenda UDAKU katika stori za UDAKU za wengine.

Nikiwa namaaana -wajijuayo wanayo watu, ndio AMBAYO huwachekesha wakiyastukia jinsi yachezavyo kwenye maisha ya wengine.
Kielelezo :
''Ndio maana ni rahisi kuchekelea ukistukia nyege kama zako zimemponza Mheshimiwa mpaka kadakwa gesti na mke wa jirani.''


2. Maisha Magumu na yanaboa.

Kwa hiyo badala ya kuhangaika na swala gumu zaidi kama la kutatua matatizo yako , ni rahisi kujisikia UNAFUU kwa kustukia na wengine halizao sio MSWANO 100% kama wewe kitu kikupacho unafuu au pia kukusaidia mpaka kuwacheka ustukiao wana hali mbaya kuliko weye.

3. Ni kweli kwa wengi KUFIKIRI ni KUGUMU.

Kwa hiyo MTUZ hujikuta zinakwepa MAKALA ZA UCHAMBUZI kwa kuogopa kufikirishwa mambo mapya ambayo yanahofiwa ni magumu. Basi ndio maana MAGAZETI YA UDAKU yaongeleayo swala ambalo kila mmoja anahisi ni rahisi kama vile lile la KULALANA. Na ni kweli stori za NANI ANAMLALA NANI ni rahisi kuzielewa kwa hiyo naweza kuelewa kwanini MTU ANAWEZA fikia jawabu la '' KWANINI ajihangaishe na KUJIFIKIRISHA KUTATUA MAMBO MAGUMU ILI AFARIJIKE wakati stori ya Mke wa Mheshimiwa ANATOA JICHO a.k.a TIGO ni starehe tupu kwake a.k.a FULU KUFARIJI?:-(


4. UBINADAMU kwa kawaida unakuja na UVIVU !

Kama BINADAMU ukirahisishiwa hata kwa kujengewa ngazi , choo ndani, kupikiwa, - ni fulu kukenua meno kwa kuwa jinsi urahisishiwavyo jambo ndio unafikiri mambo ni MSWANO. Na haki ya nani UDAKU ni TAARIFA YA HABARI MUHIMU kwa yeyote ajisikiaye UVIVU wa kufikiria la muhimu lifikirishalo MUDA HUO aanogewao na UDAKU.:-(

NALIKATIZIA WAZO HILI HAPA KIJEBA na tutaendelea SIKU NYIINGINE na kitu MAKALA ZA UCHAMBUZI vs MAKALA ZA UDAKU nini TAMU na KWA NANI!:-(

Swali:

  • Unafikiri kwanini MAKALA ZA KICHAMBUZI kwa wabongo wengi hazinogi?





Nawatakieni wote KAMANYOLA BILA JASHO Ijumaa na WIKIENDI HII WAHESHIMIWA!







Tupumzike kwa katuni hii nilioitoa katika BLOGU ya MUMY HERY JP yenye bonge la swali baada ya KITENDO.























Hebu tupewe BONGO FLEVA na Hot galz Ft Dully Sykes waongelee ile KITU roho ya Wabongo inapenda ambayo ni-Raha ya Tunda

Ama tu Fresh JUMBE arudie- AMA ZAKE AMA ZANGU

6 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

MARKUS MPANGALA 5:49 pm  

duh watawashia na koroboi kujisalimisha na kupata uchambuzi wa FIKIRA...lakini kumbe waumini wa yudawa wa UDAKU. lakini wote wanapumilia mashine za mochwari za kuapndisha hanjamu za andunje na koko

MARKUS MPANGALA 5:49 pm  

duh watawashia na koroboi kujisalimisha na kupata uchambuzi wa FIKIRA...lakini kumbe waumini wa yudawa wa UDAKU. lakini wote wanapumilia mashine za mochwari za kuapndisha hanjamu za andunje na koko

malkiory 7:59 pm  

Mt.Kitururu, heko kwa utayari wako wa kuelimisha jamii kuhusu mada aliyoichokonoa profesa Matondo. Ukweli ni kwamba wanajamii huipa kipau mbele habari za udaku kulikoni zile zenye mwelekeo wa kuelimisha.

Fadhy Mtanga 7:43 am  

Mtakatifu Simon we acha kabisa na hiyo katuni... Sijui jamaa alijibuje!

Anonymous 3:44 pm  

nikiingiaga huku nasikia kizungu zungu!!

kilegu

Simon Kitururu 4:03 pm  

@Mkuu Markus: :-)
@Mkuu Malkiory: Kwa bahati mbaya staili yangu ya kuelimisha kuna watu lukuki hawaielewi na wapatacho ni lugha chafu na kuchanganyikiwa:-(
@Askofu Fadhy: :-)

@Mkuu KILEGU: Asante kwa kunitembelea ingawa kijiwe unakiona katika pipi Klorokwini.Tuko pamoja na karibu tena na tena ukijisikia kubadili vijiwe.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP