LABDA staili ya NGONO , mwerevu imempa GONO!:-(
>> Thursday, December 04, 2008
Katika maono,
....nitakacho ni dhambi ingawa KINONO.
Sitangazi mgomo,
...wajua siri,kama wewe navizia  nono.
Tungefunzwa mauno,
.... labda peni kwenye TUNDU ingemwaga wino.
Karatasi lenyewe NONIHINO,
 ...kufuta ni KUJIPAKAZA na  kupakaza WINO.
Najifunza MUMO kwa MUMO,
.....werevu wan'teta udhaifu MGUNO.
Mwerevu an'nyima somo,
....hapendi kwenye bata firigisi ilimo.
Mwerevu mjuaji mno,
-Ni  uerevu kumnyima mwenye kundu KUNYA MNO?
Kama mjua PANYA mkata KIUNO,
-si ni uerevu kun'funza staili za  kula  panya MNONO?
Kama kidaka tonge kina meno,
....n'stue za kuchovya bila kung'atwa meno.
Kama staili zina udenda  moto mno,
.......n'stue nivae  glovu  na sio chupi au  kimono.
LAKINI....
Mwerevu  ana  SIRI na kisonono,
... hajulikani kwa KIDONDA NDUGU, MDUDU ,wala GONO.
Kukana mahiri mjanja mno,
..binadamu humsifu ,kwenye kosa yeye hayumo.
Atukataza tusifanye nono,
... akijua lazima tutaonja humo!
Badala ya kutufunza somo,
....adai tuvumilie na ni sumu unono.
YEYE afanya MPAKA  konokono,
....atunyima somo  na hafuati ajualo somo.
Mtaalamu MWEREVU, mwenye NGOMA na somo,
- mbona BADO wafa na GONO?
:-(
------------------------------------------------------------------------------------------------
NAWAZA tu MKUU!
Siku NJEMA !
Tupewe funzo kidogo na TENDER MVUNDLA...
Au twende tu NIGERIA kumsikiliza MAJEK FASHEK.......katika So  Long TOO LONG
 
  
 Posts
Posts
 
 




0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:
Post a Comment