Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

SURA BWANYENYE ya DUNIA kidunia kwa kuwa kuna kitu watu wanadhania WANAJUA kuliko KUKU wa kienyeji mzururaji!:-(

>> Thursday, December 23, 2010

Sura ya DUNIA kwa mtu,....
..... mara nyingi hutegemea sana MTU anafikiri ANAJUA NINI  ikisaidiwa sana  na ALIJIFUNZAJE afikiriacho ni KUJUA.:-(



Kama ilivyo katika kitu kidogo kama  ujuzi wa ni ipi CHAI NZURI kwa watu,.....
.....ajuaye ili CHAI iwe nzuri anahitaji SUKARI anaweza kudhania  CHAI BILA SUKARI si nzuri kutokana tu na afikiriacho NI SAHIHI kwa kuwa ndicho ALICHOJIFUNZA na ndicho  afikiriacho ndicho KUJUA.:-(



Na tofauti ya MTU afikiriaye kwa MDADA ni sahihi kutokana na ajuavyo  kutembea MATITI NJE  na  YULE MTU aaminiye sio ustaarabu hata kwa MDADA kucheza  ngoma za utamaduni wa KIAFRIKA WAKE ziruhusuzo MDADA kunengua huku akitikisa NYONYOZ  a.k.a MATITI yake MANONO nje katika kujivunia tamaduni yake na wake UTU,.....
.....mipingano ya MITAZAMO YAO  hutokana na jinsi tu walivyojifunza ni nini  ni USTAARABU au mpaka nini  ni kuwa UCHI bila kusahau ni njia gani walijifunza hayo mambo mpaka kufikia siku hiyo wanashuhudia bonge la NYONYO au tu  lile TITI lililokonda tayari  lenye bonge la kunyazi  ambazo ndizo zimechukua nafasi ambazo ziliwahi kutunisha TITI  likae mkao wa NCHALE saa sita kamili LIKITIKISWA KWA FURAHA NJENJE na kufanya ALICHOJIFUNZA kumsaidia KUTAFSIRI SWALA limfanyalo asikie aibu au KUJIVUNIA ambalo kwake ndio  KUJUA.:-(


Swali:

  • Si unajua YA DUNIA kama unayajua  kwa kupitia UISLAMU labda kujua kwako kwa mengi kutakuwa na tafsiri ya KIISLAMU kitu kiwezacho kufanya yale ya KIKRISTO kirahisi yawe ni KUCHEMSHA na sio kupatia KUJUA wakati WAKRISTO nao kutokana na njia walizojifunza KUJUA wakawa na uhakika kuwa ni WAISLAMu wakoseao kujua?

  • SI unajua kujua KISABATO kunaweza kumhakikishia MSABATO  kwanini WAKATOLIKI wanakosea katika yao ya KIROMANI KATOLIKI katika KUJUA?


  • Si unajua hata ni NINI KUJUA KUCHAMBA VIZURI baada ya kunya kama tu ni nini  ni PEMBEJEO sahihi  ya kuchambia ukiwafuatilia wapendeleao, TOILET PAPER a.k.a MAKOKONEO a.k.a TISHU, wachambiao mchanga..... mpaka waaminio NI MAJI tu ndio siri ya tako safi hutokana tu na jinsi gani MTU ALIJIFUNZA usafi wa kinyeo kuliko mpaka athiriwa na TAMADUNI YAKE , mazingira au tu  na  nani ndiye aliyefunza HIYO SHUGHULI na kumuweka katika uelewa anaouchukulia kuwa katika hilo jambo ndiko KUJUA?





Ndio,....
....KUDHANIWAKO ni kujua kwa mtu,.....
....kumeathiriwa sana tu na ELIMU YA MTU na pia NA ni jinsi gani huyo MTU alivyopata hiyo ELIMU kitu kiwezacho kirahisi KUFANYA kujua kwangu koooooote,.....
......kwako kunaweza kuwa ni USHUZI MTUPU kwa kuwa kuna kitu  unaamini wewe ndio una USAHIHI wake  kwa kuwa wewe ndio UNAJUA.

Swali:
  • Si kuna uwezekano KUJUA ni kudhaniatu  UNAJUA kwa kuwa labda ajuaye kikweli ni MUNGU pekee wakati labda hatuna uhakika tunajua kwa asilimia MIA Mungu yupo na TWAMJUA?
Ndio,....
.... sura ya DUNIA iliwahi kuwa kama MEZA na wala sio MDUARA ,....
....kutokana tu na WANADAMU waliyodhania KIPINDI HICHO ndiko KUJUA,...
....na labda tusishangae hata kwa ya LEO tuyachukuliayo ndiko KUJUA,....
.....yakigeuka somo la HISTORI kwa kizazi KIJACHO wakati wanajifunza ni jinsi gani tulikuwa tunachemsha katika tuliyokuwa TUNAJIGAMBA ndiko KUJUA.:-(



NI WAZO TU HILI Mheshimiwa na wala usikonde!


Hebu Black Stalin aingilie kati shughuli kwa - Black Man Feeling To Party




Mighty Shadow naye ashushe pia-Dingolay





Au tu Mighty SHADOW amalizie tu na jiwe -Poverty is hell

3 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

emu-three 8:19 am  

Kujua kitu ni utambuzi ni elimu kwani umejua kile usichokijua ingawaje wenzako walishakijua na kukiona labda hakina maana, lakini kwako umepevuka. Ni sawa na mtoto akiwa mchanga, hakuna kitu bora kwake kama maziwa ya mama. Yeye anajua hicho ndio kila kitu, kumbe kuna chakula!
Ndio ni kweli hata imani zinakizana kwa kule kuona kuwa imani yake ni bora kuliko nyingine, kwa ujuvi wao. Huwezi kumuhubiria/ kumpa waithi ujuavyo, kwani mwisho wa siku anaweza kukuambia umemkashifia imani yake.
Ni hayo tu mkuu

Upepo Mwanana 11:47 am  

Yote kwa yote, lakini kuchambia mchanga tena!!!

Simon Kitururu 5:57 pm  

@M3: Nakubaliana sana tu nawe katika hili!
@Upepo Mwanana wa marashi ya karafuu:

Ukichunguza watu wachambiavyo utastukia kuwa labda kuchambia mchanga wala sio ajabu JANGWANI pasipo na maji karatasi na hata angalau mawe.:-(

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP