Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Cheka nuna.

>> Friday, February 14, 2014

Na ukinuna,..
Je moyowo watabasamu?

Na ukicheka,..
Je moyo ununao ni wa kibinadamu?

Cheka nuna na ikibidi lia,...
Na si mwisho wa cheko  yalizayo ni utamu?

Cheka nuna,...
 Na wala usijilazimu.

Cheka,..
Ili nasi tudoee wako utamu.

Nuna,...
Ila usilize mpaka mizimu

Cheka nuna,...
Je si hata kulia ni ubinadamu?

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 12:10 pm  

Ni bonge la wazo ambalo ni ngumu kuchagua kucheka au kununa...Karibu tena katika dunia hii ya kublog..

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP