Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Watu husikiliza na MAISHA yao kwa hiyo uongeleapo HIKI wengine huweza amini unaongelea KILE!

>> Sunday, September 25, 2011

Ndio,...
.....labda WATU husikiliza na MAISHA yao,...
..... kitu kiwezacho fanya aongeacho MTU kieleweke tofautitofauti kutokana tu na ni nani ni msikilizaji na ni mwenye maisha gani!:-(


Swali:
  • Si  ukiongelea SHIDA labda unaelewekaji wake ni  tofauti  kama akusikilizaye ni TAJIRI au MASIKINI, MSOMI au  yule SHULE ni madangacheee?
  • SI unajua yasemekana aliyekulia katika waongeleao MAFUMBO hata ukiongea kitu moja kwa moja atajaribu kufumbua FUMBO?
  • Si yasemekana kuna wasioelewa kuwa sio wote ukiongea hata kwa kunukuu vitabu kanma VITAKATIFU bado sio wote watachukulia huo ndio ukweli kwa kuwa kimaisha yao BIBLIA na KORANI bado ni kitabu tu chenye stori za kutunga na hakina utakatifu waliouzoea wakuliao kwenye MAISHA YA waaminio ?


Ndio,...
......katika sanaa ya KUONGEA uongeleapo HIKI,...
.... yaweza kueleweka unamaanisha KILE!:-(




Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(

Hebu P.Square, Tiwa Savage na May D wabadili vita kwa -Do as I do



Tiwa Savage abaki mwenyewe kwa - Kele Kele love



Au tu tena Bunny Mack azime mshawasha kwa kutuliza na  - Let Me Love You


Read more...

KAPINGAZ Blog SIO MUDA MREFU TUTAKULETEA JEZI ZENYE LOGO YETU KAA MKAO WA KUVAA.


Mfano wa Jezi itakayokuwa na Logo yetu, karibu sana mdau.

Jezi hizi zitakuwa zikigawiwa Bure, haziuzwi. Kama utahitaji usisite kuwasiliana nasi mapema kupitia mawasiliano yetu yaliyopo kwenye Blog. Tunashauri ni vema ukatumia Email ili tuweza kuwa na kumbu kumbu nzuri badala ya simu

HABARI ndio HIYO!

Nimetumiwa na Henry Kapinga,...

Read more...

Katibu wa TA Reading na Mkewe Wameremeta!

Salam,


URBAN PULSE CREATIVE Inawaletea picha za tukio la Harusi ya nguvu iliyofanyika Jumamosi Tarehe 25 septemba 2011 Katika ofisi ya Reading Registrar kati ya Katibu wa Tawi la TA Hapa Mjini Reading Amri Dello na Alice Kapya.


Baada ya Kufunga pingu za maisha tafrija ilifanyika ndani ya Boat na kuzunguka mitaa ya berkshire hadi windsor kwa Queen na kumalizikia katika Mji wa Reading.

Wadau mbalimbali walikuwepo katika sherehe hii akiwepo Mh Balozi wetu Peter Kallaghe.

URBAN PULSE inapenda kuwapa hongera sana Maharusi wetu na kuwatakia kila la kheri katika safari yao ndefu walioianza leo.

MUNGU AWABARIKI,
Asanteni

URBAN PULSE CREATIVE

Bonge la kiss

Zawadi Maalum kutoka kwa Mzee Abdul Dello

Boti inayoitwa caversham Princess ikiwasubiri maarusi tayari kwa ajili ya sherehe

Bwana Harusi akiweka Sahihi kwenye cheti cha ndoa

Bwana harusi Dello

Bwana na Bibi Harusi

Bwana na Bibi Harusi wakiwa wanameremeta

Dello akimlisha keki mkewe

Kila Kitu kimekwenda poa na jiko nshavuta sasa tugange yajayo

Maarusi wakipewa maelekezo kabla ya kuingia kwenye boti

Mh Balozi akitoa nasaha zake kwa bwana na bibi Harusi

Mh Balozi Kallaghe Akiwa na MH Balozi Kapya wakibadilishana mawili matatu

Mh Balozi Kapya na Binti yake wakiingia katika ndani ya Reading Registry Office

Picha ya Pamoja kutoka kwa pande zote za famailia na wadau waliokuja leo kushuhudia Harusi

Pozi baada ya Harusi

Wadau wakijimwaga kwa raha zao

Wakati wa kulisakata Rumba

Read more...

KULIA ya KUSHOTO!

Ndio,...
... KULIA kwako ,...
.... ni KUSHOTO kwa mwingine!

Swali:
  • AU?

Ni wazo tu hili MKUU!
Nakutakia Jumapili MCHELEMCHELE kwako BINGWA!



Hebu Julio Iglesias aanzishe kwa - El amor



Julio Iglesias aongezee dozi kwa - I want to know what love is



Au tu hebu George Michael aingilie kati kwa -Careless Whispers


Read more...

Tantra Zawadi

>> Saturday, September 24, 2011

Hebu arudie - Girl: A Choreospective


Read more...

Haya wana NDONDI!

Deku,...

Read more...

Katika kuoanisha MAANDISHI ya KIPENZI MTANDAONI, sauti yake kama MALAIKA na LISURA kama JIPU!

Sauti na MAANDISHI  kwenye sura ya KISURA ambaye hujawahi kukutananaye  kwa kuwa penzi liko MTANDAONI,....

.... hujenga  pia SURA ya KISURA uitakayo,....
.... kwa kuwa  moja ya kikumbushacho  na kukamilisha sura ya MTU  labda wala sio SURA.:-(

Swali:
  • Ushawahi kustuka baada ya kukutana na mtu ambaye ulikuwa unamjua kwa maandishi  au sauti tu na kujikuta  unahitimisha hayuko kama ulivyomjenga akilini kimategemeo?

Ndio,...
.... kuna VISURA ambao ni wazuri  KIMAANDISHI na SAUTI tu ,...
.... ambao ukikutananao itabidi uanze kujifunza upya kuoanisha SAUTI , maandishi na SURA,...
.... ili MPENZI apendeke  kama ulivyowahi  kumpenda kwenye ndoto mara kadhaa kila siku ukilala ,...
.... kabla hujakutananaye!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!
Jumamosi NJEMA!

Hebu TITI aanzishe upya kwa -Ilove U




Titi aongezee mnuso kwa - Sy Malick



Au tu Werrason arudishe tu -Likambo


Read more...

TUKIO LA MADEREVA WA MBEYA KUGOMEA TOCHI NYINGI BARABARANI KULIKONI!

Madereva wa Mabasi na Matrafiki katika Stand kuu - Mbeya.
Tukio la Madereva wa Mabasi ya masafa marefu kutoka Mbeya kugoma kuendesha mabasi yao kwa kulalamikia 'TOCHI' nyingi barabarani limenishangaza sana, kwa faida ya wasioelewa, TOCHI ni Kamera za usalama barabarani zinazotumiwa na Matrafiki kuangalia magari yanayokwenda mwendo wa kasi katika eneo ambalo hawastahili kwenda mwendo huo.
KAPINGAZ Blog inapata shaka kidogo, ni kweli hao Madereva wanagomea TOCHI! au kuna kitu kingine Chini ya kapeti? nadhani wao madereva wanalijua hili. Wosia wangu, kama Madereva wanagomea TOCHI kama TOCHI isitende kazi yake, nitapingana nao kwa asilimia 100; ila kama kuna lingine nje ya hapo nawasapoti vile vile kwa asilimia hizo hizo.
"TAFADHALINI, TAIFA BADO LINAZIHITAJI NGUVU HIZI ZA WATANZANIA WANAOPOTEA KILA SIKU KWENYE AJALI AMBAZO NYINGI ZINASABABISHWA NA UZEMBE"


Nimetumiwa na Henry Kapinga ,...

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP