Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

TUKIO LA MADEREVA WA MBEYA KUGOMEA TOCHI NYINGI BARABARANI KULIKONI!

>> Saturday, September 24, 2011

Madereva wa Mabasi na Matrafiki katika Stand kuu - Mbeya.
Tukio la Madereva wa Mabasi ya masafa marefu kutoka Mbeya kugoma kuendesha mabasi yao kwa kulalamikia 'TOCHI' nyingi barabarani limenishangaza sana, kwa faida ya wasioelewa, TOCHI ni Kamera za usalama barabarani zinazotumiwa na Matrafiki kuangalia magari yanayokwenda mwendo wa kasi katika eneo ambalo hawastahili kwenda mwendo huo.
KAPINGAZ Blog inapata shaka kidogo, ni kweli hao Madereva wanagomea TOCHI! au kuna kitu kingine Chini ya kapeti? nadhani wao madereva wanalijua hili. Wosia wangu, kama Madereva wanagomea TOCHI kama TOCHI isitende kazi yake, nitapingana nao kwa asilimia 100; ila kama kuna lingine nje ya hapo nawasapoti vile vile kwa asilimia hizo hizo.
"TAFADHALINI, TAIFA BADO LINAZIHITAJI NGUVU HIZI ZA WATANZANIA WANAOPOTEA KILA SIKU KWENYE AJALI AMBAZO NYINGI ZINASABABISHWA NA UZEMBE"


Nimetumiwa na Henry Kapinga ,...

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP