Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Wanaume waingia Ubalozini Uingereza

>> Monday, September 19, 2011

Salam,

URBAN PULSE CREATIVE na Miss Jestina Blog wanakuletea Ziara ya Wanaume kutoka kundi la  TMK wakiwalishwa na Mh Temba na Chege walipopata fursa ya kutembelea Ubalozi wetu hapa mjini London kabla ya kumaliza show zao hapa nchini Uingereza siku chache zilizopita. Vilevile waliweza  kutembelea idara mbalimbali na kujionea jinsi gani Ubalozi wetu hapa London unavyofanya kazi hususani  katika idara nyeti ya Uhamiaji inayoongozwa na ofisa Ambokile na Kupiga Picha za pamoja wakiwa na  Mh Naibu Balozi Mh Chabaka Kilumanga Pamoja  na baadhi ya maofisa wa Ubalozi.

Baada ya Ziara yao Freddy Mtoi Kutoka BBC alifanya nao mahojiano maalum  ndani ya ubalozi na yatarushwa hewani  duniani kote.

Asanteni,

 Ziara hii iliandaliwa na Urban Pulse pamoja na Miss Jestina Blog,...
.....Ikishirikiana na Ubalozi wetu
 
Zamu ya Mh Temba

Chege akitoa Changamoto

Chege na Temba wakiwa na ofisa wetu Ambokile katika ofisi ya uhamiaji

Freddy Mtoi kutoka BBC akianza mahojiano na Mh Temba wakati Chege anakusanya data

Mh Naibu balozi akiwa, maofisa wa ubalozi katika picha ya pamoja TMK pamoja na promota wao George

MH Naibu Balozi Chabaka Kilumanga kwenye picha ya pamoja TMK na Goerge Ubalozini

Promota wa TMK Goerge Stanley Kutoka Gonex Service Limited akiwa na Joel Chacha katika ubalozi wetu London
 
 

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP