Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Cesaria Evora ang'atuka toka ulimwengu wa muziki !

>> Tuesday, September 27, 2011

Cesaria Evora kazini!



Kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa MOYO.....
..... Mwanamama CESARIA EVORA  kutoka Cape VERDE kashauriwa kuacha MUZIKI.

CESARIA ni moja ya wanamuziki kutoka AFRIKA niwapendao SANA!

HABARI zaidi kongoli HAPA au HAPA

PUMZIKA  MAMA na nakutakia MAISHA MAREFU!


Ngojea mie niendelee kukusikiliza,...
.... katika Miss Perfumado



Africa Nossa



Besame Mucho



Au tu hebu alete tena na -Angola

Read more...

TANESCO WATUMA SHUTUMA NZITO KWA KAMPUNI YA PAN AFRICA.

>> Monday, September 26, 2011

Afisa Uhusiano wa TANESCO Badra Masood.
Leo katika kipindi cha Breakfast kinachorushwa na Redio ya Clouds FM Afisa uhusiano wa TANESCO ameishutumu kampuni ya PAN AFRICA Enegy ndio inayosababisha matatizo haya ya Ugawaji wa umeme uwe haufuati Ratiba.
Hayo aliyasema baada ya kuona shutuma nyingi zinatumwa kwa TANESCO badala ya kampuni hiyo inayo iuzia Gesi Tanesco kwa ajili ya kuzalishia umeme. Ameyasema haya ili kampuni ya PAN AFRICA nayo iwaeleze wananchi ni kwa nini umeme mgao wake haueleweki. 
Tanzania kwa kipindi cha zaidi ya miaka mitano imekuwa na matatizo ya umeme yasiyo isha.

KAPINGAZBlog inampongeza kwa kuonyesha ujasiri, kuamua kutueleza wananchi nani anayetusababisha kupata umeme kwa mgao usioeleweka, pia tunapenda kuwashauri wajitahidi kutafuta vyanzo vingine vya kupata nishati hii muhimu kwa maendeleo ya Taifa.
Nimetumiwa na Henry Kapinga,...
.... wa KAPINGAZ blog.

Read more...

PIPI tamu , NYAMA tamu,...

... na kwa bahati mbaya  na MCHICHA  pia MTAMU!:-(


Swali:
  • Si umestukia labda liutamu LABDA LIKO kwenye  LIULIMI LAKO lisikialo tamu hata kwa kupapasa KITOVU na lisananishalo pengo kwako ni MWANYA?


Na CHAI  ni  chungu, ...
.... PIPI  pia lama MBILIMBI TAMU ni chungu,...
......kwa kuwa nasikia hata SUKARI huingia MDUDU!:-(

Ndio,...
.... ni wazo tu hili MHESHIMIWA na kutolielewa RUKSA!:-(
JUMATATU NJEMA MHESHIMIWA!




Hebu INI KAMOZE aingilie kati nakuanzisha upya kwa-GENERAL


INI KAMOZE aongezee dozi kwa -Trouble You A Trouble Me

Ini Kamoze aweke kidangachee ndude- Them Thing Deh



Ini Kamoze huyuhuyu a - Cool It Off



Au INI KAMOZE amalizie tu tena kwa- Here comes the HOT STEPPER


Read more...

Wakati tunamendea KINACHOHITAJIKA na kusahau umuhimu wa KILICHOPO!

KILICHOPO labda  ndio kitiacho nguvu MTU,...
... hata ya kufikiria  kile kiaminikacho ndio KIHITAJIKACHO!:-(

Swali:
  • SI SHILINGI iliyopo labda inamchango mkubwa kuliko ITARAJIWAYO  ambayo hatunauhakika itakujakuwepo?
  • Si kidude cha ZUBEDA labda kinatosha hata kama aliye na ZUBEDA anaamini  ahitajicho  ni kile cha KHADIJA?
  • Na vidhaniwavyo vingi si nasikia ni VYAKUFIKIRIKA kama kilichopo hata kama ni ugali tu kwa maharage  hicho ndio  bonge la NGUNA  kwa rojo?


Ndio,...
..... kilichopo labda ni MUHIMU ZAIDI ya kile kidhaniwacho ndicho chahitajika,...
....... kwa kuwa  nguvu ya MAHITAJI labda inamisingi yake ambayo ni muhimu zaidi  hata kama ni kwasababu tu inawezesha mtu  mpaka kufikiria MENGINE  kistaili ya MAHITAJI!:-(

Ni wazo tu hili NGULI ,...
.... na wala USIKONDE!:-(

Hebu Kevin Hart ajaribu kubadili kwa kuongelea - Other peoples personal problems



Capleton aingilie kati na kurudisha bolingo katika - That Day Will Come



I-WAYNE ajaribu tena kukiri - Can't satisfy her



I Wayne aongezee dozi kwa kukiri pia - Need Her In My Arms



Halafu sijui kwanini ila hebu FALLY IPUPA aibadili tena  kwa -CADENAS




Halafu LOKUA KANZA afunge tu ukurasa kwa - NAKAZONGA


Read more...

R.I.P Wangari Muta Maathai !

(1 April 1940 -26 September 2011)


Asante kwa yote,...
.....hasa kwa kutukumbusha,...
....... nguvu ya MTU MMOJA katika JAMII!
Pumzika Mama!


Hebu tumsikilize kidogo,...





Halafu,...

Habari zaidi,...
...HUKU au,...
......HUKU

Read more...

Katika SULUHISHO la kuvunja kioo ili MWANAIDI asijione ``SURAchaUPELE´´ na kujisikia VIBAYA!

Ndio,...
.... kunawashaurio kivunjwe KIOO,...
.... ili siye wenye sura mbaya tujisikie vizuri kwa kutojiona!

Swali:
  • Si  kujiangalia ndio saa nyingine hukumbusha mtu  ujazo wa pua   kama jipu?

Ila TATIZO tu ni kwamba,...
..... kuvunjika  kwa KIOO kusababishako  MTU  asijione,...
.... bado hakubadili  SURA ya MTU!:-(


Swali:
  • Si hata tufanyeje kukwepa kutambua tatizo lipo kwa kutoliangalia huwa hakuondoi tatizo?
  • Na si WASENGE wapo tu BONGO  hata kama jamii inadai  hawapo na matatizo yao yasitambulike ingawa yapo?

Ndio,..
..... moja ya  dalili ya matakwa ya MWANAIDI  kioo kivunjike ,...
.... labda ni yale ya kumlaumu MESENJA wakati afanyacho ni kuwakilisha tu meseji  ambayo ipo tayari  na wala yeye  mesenja hahusiki  katika mtengenezo wake!:-(

Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!:-(


Hebu twende tena Zimbabwe ili Oliver Mtukudzi aanzishe kwa - Neria



Oliver Mtukudzi arudie- Ndakuvara



Oliver Mtukudzi aongezee dozi kwa - Tozeza baba





Aongezee zaidi tena-Todii



Au tu tena Ringo Madlingozi aingilie tena  kati kwa -Into Yam


Read more...

Katika UJEMADARI KIMBOO muongozo LABDA ni HISIA,....


..... na KATIKA nanihii labda kweli ni UJEMADARI,...
.... kama KUINGIZWA  mtu kichwakichwa  kwenye giza asikokujua ni UJEMADARi  ,...
..... kama tu  katika UJEMADARI wa VITA ambayo nanihii itabidi ingie gizani kichwakichwa,...
.... bado ni UJEMADARI labda kwa kuwa MTU kiaina ni kichwa kwa kuingia  waogopako WENGINE kwa kuwa hakijulikani kilichondani huko kwenye GIZA!:-(


Tahadhari:Inawezekana kile kidude kifananacho JINA ambacho hata mbwa na sungura wanacho -LABDA hakimaanishwi hivyo katika TARALILA HII  iliyopinda kiwazo na KITARALILA HII !:-(





Ndio,...
...JEMADARI ,...
.....hata KIMALAIKA wa KIHISIA   ,....
... tukiacha kugusia asifiwayo YAJULIKANAYO  YALIYOWAZI ,...
...labda  kama hakuna afikiriaye  labda hakutakuwa na JEMADARI asifiwaye kwa YALIYOWAZI njenje  ,...
.........na tutabaki na wenye sifa  zenye UJEMADARI kimboo  wa kuingia kwenye matundu ya giza  bila kutumia macho , pua au hata KUHOJI kiakili JAMBO  kwa kuwa NI HISIA TU  HILO na sio HALIHALISI  kiukweli ndio MUONGOZO kuwa  TAMU !:-(



Swali:
  • Na si SUKARI nasikia ni tamu KIHISIA  hata kama imetiwa SUMU?
  • Si wewe KWA WENGINE  labda ni  jengo tu la mtalimbo KIKIFIKIRIWACHO TU KIHISIA  kisa umevaa MIDABWADA  wakati ukweli ni kuwa wewe ni NGULI  utatuaye kwa UBONGO na sio MTALIMBO ?

Na kwa kuwa kuna wajisifiao MJENGO kihisia,...
....    labda MTU asivimbe KICHWA  kwa kuwa ukweli wawezakuwa   BADO ni kwamba  KIHISIA TU  kuna wasifiwao kama tu WALAANIWAO  kwa ya kweli amabyo MTU akiyafikiria na KUNYAMBULISHA kwa kutumia AKILI  na si HISIA TU kuna  kitu kinaweza kumstua kuwa si kweli  harufu ya WALI ni lazima iwe kuna WALI kwa kuwa INAJULIKANA  kuna mpaka NYOKA wanukiao  KIUBWABWAUBWABWA.:-(



Swali:
  • AU?

NA  ndio ,...
...labda JEMADARI kikuma yupo pia  kwa ya JEMADARI kimboo,..... 
....kwa kuwa pamoja na kwamba mambo mengi sio UDHU na hayahitajiki kwenye JENGO  na  hayana uhusiano na UMALAIKA uingiliwao  mtalimbo ingawa yapo ndani ya JENGO,...

.... kihuswishwi  cha KITU  BORA   labda sio  tu  kiko kwa  NJE  KIONEKANAKO KIRAHISI  kwa kuwa  vingi bora viko NDANI  na  UJEMADARI kikuma ni ile ruksa ya kuruhusu visivyotathiminiwa viingie ndani KUCHOKONOA vyenye MALIGHAFI BORA kitu ambacho kikuma LABDA  ni UJEMADARI!



Swali:

  • Si unajua  kwa ndani  hata ya jipu hakuishi usaha tu peke yake na na labda ni UJEMADARI kuruhusu SINDANO kimtumbuo?
  • Na kwani JENGO kanisani AU msikitini ni lazima WASWAHILINA au WALOKOLE wawe ndani ili  kisala SALA itoke STIRIO?


Ndio MHESHIMIWA ufikiriaye mpaka neno MBOO au KUMA ni tusi,...,...
.... labda MATUSI yako ndani ya  ufikiriavyo KIHISIA TU ZAIDI kuliko halihalisi ya TUSI  au utendavyo kuliko hata jengo ambalo ni NENO,...
... na KIHISIA kama kimaneno  labda  ya hata ´´KHADIDJA HAJAVAA CHUPI ´´haibadili ukweli  kuwa    kivitendo yaweza kuwa ni kweli ``KHADIDJA hajavaa CHUPI´´  na sio HISIA hiyo .:-(



Swali:
  • Si unajua tusi la ukweli  laweza kuwa bado ni HISIA tu ZA MTU?

Ndio,...
....kwa UNDANI,...
...... labda BINADAMU hana undani sana na ndio NDANI kwenye GIZA hata kama sio ndani ya kidude cha MTU  kunawezatisha WATU au ndio  maana kirahisi ana MPAKA dini ambayo anaamini  ni sahihi  kiasi kwamba waaminivyo wengine sio SAHIHI ,..
... wakati anajua misingi ya IMANI ni imani na imani  haina ushahidi  kama tu wengine waaminivyo  KIHISIA  ZISIZO NA USHAHIDI ambazo kiana zajenga UJEMADARI wauaminio ambao kwa lugha ya kipicha unaweza kuuoanisha na vitendo vya sehemu za siri vya ujemadari wa kuingia au kuingiliwa kwa ukakamavu bila woga wala kutumia akili  ingawa zaweza samehewa kwa kuwa SEHEMU ZA SIRI HIZO kimboo au kikuma hazina UBONGO.:-(


NIMEACHA wazo hili nyoko MHESHIMIWA!!:-(










Hebu IPHY OKOLI aabadili kwa kuanzisha mchezo upya  kwa -Ifeome




Lil' Kim ajaribu kugusagusa eneo kwa - No Matter What They Say




Au tu hebu Missy Elliott amalizie tu,...
............kwa kusema ukweli kuwa - She's A Bitch



Ndio,...
... bado nipo!:-(













Read more...

Kuna MATATIZO yapewayo MAJINA mazuri mpaka unaweza usiyaoanishe na TATIZO,.....

.... lakini  TATIZO labda ni TATIZO tu hata kama kijina  limegeuzwa kuitwa MFADHAIKO wakati kivitendo TATIZO  lionekanalo  kwenye foleni,...
....ni  mdada wawatu kachafuliwa na lijidume KAME lililotokwa mbegu kimfadhaiko  KAMA tu  itokeavyo  kwenye DALADALA.

Swali:
  • Si unakumbuka eti kuna wauguao mfadhaiko  na ugonjwa ukizidi  ni hatari hata hadharani wakiguswa na MDADA?
  • Na si MWIZI hurembeshwa jina na kuitwa FISADI saa zingine kisa  ni MHESHIMIWA?:-(

Ndio,...
..... binadamu  hata TOTO baya la MBWA huweza kulitungia JINA zuri,...
.... utafikiri   kwa kukipa kitu JINA zuri huondoa makali ya ubaya wa kitu!:-(




Ni wazo tu hili MHESHIMIWA!

Hebu tena Mahotella Queens warudie - Umculo Kawupheli



Simon Mahlathini aingilie kati na kuja na Mahotella Queens katika - Kazet



Au tugewe tu tena -Dikgomo remix

Read more...

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP