Niko TANZANIA , najifunza KWA muda KIDUCHU kunanihii!
Niko BONGO nyoso , bado sijajulia.
Unawezakunipata kwenye namba:+255765855382
Usipoangalia, NITAKUJIBU!
Nikichelewa kurudi hapa kijiweni, NAOMBA MSAMAHA!
BAADAYE BASI!
FALSAFA na WAZO ndani ya neno!
Niko BONGO nyoso , bado sijajulia.
Unawezakunipata kwenye namba:+255765855382
Usipoangalia, NITAKUJIBU!
Nikichelewa kurudi hapa kijiweni, NAOMBA MSAMAHA!
BAADAYE BASI!
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 3:32 PM 22 kommenttia
WEWE si YULE!
Kuna ambacho YULE anaweza akakudanganya UKAAMINI!
:-(
Wakati unamkubalia, unaweza ukawa unauhakika ANAKUDANGANYA ingawa unapenda tu SAUTI ya SENTENSI.
Wakati unakataa , unaweza ukawa na sura ya FURAHA ingawa labda UNGEKUBALI, ungekula PILAU, kama wewe ni MPENZi wa PILAU.
SWALI:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 10:43 AM 0 kommenttia
Ukiwa na HAMU!
Akili yako itajaribu kukutimizia HAJA za HAMU.
Ukiwa na haja, ni rahisi kufikiria kuwa kuna staili BOMBA za kutimiza HAJA yako kama YAKE.
Kutimiza haja yako ,inawezekana kuwa ni WEWE PEKEE unaweza kusawazisha kwa sababu UKWELI ni kwamba haja yako unaijua vizuri wewe MWENYEWE.
Swali:























































Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 7:12 PM 1 kommenttia
Kuna watakaosema kuwa ,HATA UJUMBE wa YESU au IDDI AMINI , kuna waliousikia na KUUSAHAU kama tu UJUMBE wa NYERERE au yule BABU YAKO.
NGUVU ya UJUMBE ulioupata na KUTOUFANYIAKAZI ni MZURI tu kama MABIRINGANYA uliyopewa lakini HUKUYALA.
Tatizo la ujumbe uupatao,.........
....... ni ukweli kwamba MTU MWINGINE ndio anayekupa huo USHAURI ,ilikukusaidia ufike AFIKIRIAKO unataka kwenda au inawezapia kuwa ANAKUGAWIA UJUMBE katika kujisaidia YEYE MWENYEWE kujisikia kasaidia , kakusaidia AU kakushauri!
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 7:37 PM 0 kommenttia
Mazoea ni MATAMU!
CHAI ya CHUMVI inaweza kuwa TAMU kama tu CHAI ya SUKARI ukiizoea.
Uhusiano wako na NJIA ikatiziayo MIGOMBANI kwenda KULE, labda ni MAZOEA tu na SIO kweli ILE ni njia FUPI au INAKWEPA nyumbani kwa akina NOELA.
Lakini.....
....inawezekana , ile SURUALI inabidi TURUDIE tu kuivaa kwa sababu ndio kisitiri UUNGWANA kilichopo.
ULICHOZOEA kufanya unajua jinsi ya KUKIFANYA.
Ulichozoea kufanya unaweza kukifanya bila KUUMIZA sana FIKIRA.
Unajua tu UKIMTEKENYA PALE kwenye KIPELE ataKUFYONZA kama umemzoea au UMEZOEA.
UKIZOEA utajua tu BUIBUI wanajificha wapi pale kwenye KONA au kwenye SEHEMU za SIRI za KITANDA, wakati unasafisha CHUMBA.
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 7:03 PM 0 kommenttia
ASHKI ya KUFANYA mara nyingi ni kubwa kuliko ya KUONGELEA UTAFANYA.
KUONGELEA nini UTAFANYA ni rahisi kidogo, INGAWA ni NGUMU KIDOGO zaidi ya kufikiria tu UTAFANYA.
Kuongelea nini UTAFANYA kama vile kufikiria UTAFANYA , unaweza USIFANYE!
:-(
Lakini....
..... ukiongelea nini UTAFANYA , mwenzako anaweza KUFANYA.
FIKIRA zako za KUFANYA au KUMFANYA kama sio KUFANYWA , kama hujaziongelea , zinaweza zikabakia kuwa SIRI YAKO.
Kwa hiyo USIPOFANYA haina maana HAKIFANYIKI.
Kuna ambao hakijakatiza tu AKILINI ndio maana HAWAJAFANYA.
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 11:18 AM 2 kommenttia
MASWALA ya MUNGU magumu kuyaongelea kwa sababu unaweza ukajikuta UMEKUFURU kwa tafsiri zako au za YULE za kuelewa MASWALA ya MUNGU:
Uzuri wa maswala ya MUNGU , kuna dini bwelele zimsaidiazo yule, yeye au mimi kutafsiri au kuelewa ya MUNGU.
Ukishindwa zaidi kufikia kuelewa ya MUNGU, baadhi ya dini zitakushauri usali , au utubu ili hatima yako isiwe motoni au pale tu mahali pa mateso.
UZURI wake ni kwamba dini kibao tokea uanze kuijua ita-kuthibitishia kuwa MUNGU humshinda SHETANi na kwa hiyo wewe kama mjanja tokea mwanzo utajua ni nini chaguo zuri.
Lakini....
.... tunakumbushwa kuwa SHETANI atadaka wafuasi wengi kwenda nao pale kijiweni JEHANAMU kuliko wachache watakao kwenda PARADISO na baadhi ya dini maarufu.
Kwahiyo inawezekana MASWALA ya MUNGU si rahisi sana kuyaelewa, kwa hiyo hata mimi kuendelea kuyaandika hapa naweza tu nikakuzingua ingawa yako mawazoni leo ,kama jana na juzi.
LABDA hata kama hatuyaelewi......
....TUKUMBUKE kusali, Kuswali na kadhalika kadhaa, ilikujiweka katika mkao wa kwenda kijiwe cha PARADISO au kona ya MBINGUNI basi!
SWALI:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 9:38 AM 0 kommenttia
INASEMEKANA ...
.....MBWA , Nguruwe au hata NGEDERE wanauwezo mkubwa wa KUSTUKIA harufu kuliko BINADAMU.
Inasemekana....
......BATA , Nyoka au hata MINYOO, inauwezo mkubwa wa KUOGELEA kuliko BINADAMU.
Labda.....
......KUKU anaweza akawa MJANJA kuliko binadamu ndio maana bado hajaanza kutafuta kuvaa chupi na bado anatembea kwa maringo BILA VIATU.
SI BINADAMU anaamini ANAAKILI kuliko viumbe vingine, ndio maana hata VISIVYO vya MAANA ni vya MAANA kwa MTU?
SI...
...ndio maana BINADAMU anadharau BATA na hata BIN-ADAMU MWENZIE kwasababu eti yule ni ANDUNJE?
BASI MKUU naacha hiiTOPIKI!
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 9:09 AM 0 kommenttia
Kusema NISHAI!
Unaweza ukajikuta umehakikishia UMATI upumbavu kwa kitendo chako cha KUONGELEA KITU au hata SENENE.
Tatizo la kukaa KIMYA, ni udhaifu wake katika kusaidia watu kujua NANIHII au UPUMBAVU.
Ukitaka kuongea kama unaAKILI kuhusu jambo la KIPUMBAVU, kuna watakaofikiri jambo la KIPUMBAVU ni la MAANA au ni la akili.
Lakini...
...inawezekana kwamba ni kweli kila mtu anaAKILI na ni ujazo tu katika MATUMIZI ya AKILI utofautishao UJINGA wa yule na yeye kama sio MIMI.
Natishika na JINSI wenye BUSARA na AKILI wafanikishavyo KUFANYA UJINGA kwa kutumia AKILI!
SWALI:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 8:01 AM 0 kommenttia
KUMTEGEMEA ni starehe kwa sababu unahisi ANACHO.
Huhitaji shule kujifunza KUMTEGEMEA.
LAKINI.................
..utamu wa KUMTEGEMEA ni pale UHISIVYO anaKUNYIMA.
SWALI:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 10:45 AM 1 kommenttia
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 12:22 PM 0 kommenttia
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 7:51 AM 0 kommenttia
KILA kitu ni kitu cha kumuogopesha BIN-ADAMU !
Na
MIMI NAOGOPA kufanya dhambi kutokana na kufunzwa na kujifunza ubaya wa dhambi hasa katika kusababisha kuwezesha kwenda kwangu JEHANAMU!
:-(
Tatizo la uoga wa kufanya dhambi ni uwezo wetu binadamu kuzoea vitu hasa kama matokeo ya kucheza na moto huyastukii hapahapo kuwa UMEUNGUA .
UZOEFU wa kuzoea KIPORO cha wali na MAHARAGE ya nazi ya jana, hutufanya kudhani kuwa kwa sababu hatuumwi tumbo, basi KIPORO hakina vijidudu au , bakteria wakichezeacho MDAKO wakati unakigida.
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 4:43 PM 0 kommenttia
Pamoja na uzuri wa KONDOMU , ikitumika hutupwa!:-(
SAMAHANI !
Ngojea nikusalimie kwa sauti!
KONDOMU kiboko!
Ikishabeba ujauzito, hutupwa!
Inawezekana kuwa marafiki wengi uwaitao MARAFIKI ni kwasababu UNAWAITA marafiki na wanakupenda kama chakula kabla hujakistukia KIMECHACHA.
CHAKULA kilicho chacha kina harufu fulani ambayo unaweza usiistukie mpaka UONJE:
Labda RAFIKI yako mpenzi umuitaye RAFIKI mpenzi ni kwa sababu unaamini ni RAFIKI mpenzi.
LABDA...
...RAFIKI wa kweli ni yule umuitaye ADUI YAKO ambaye anakusaidia KUSTUKIA unacheza na moto wakati unacheza na MOTO:
DUH!
NAACHA TOPIKI HII!
ENDELEZA lakini PENZI na YULE , yeye au RAFIKI kwa furaha hata kama UTATAFUTA jalala kutupa mafanikio yatokanayo na kufanikisha ambayo hayakusitishi kutupa KONDOMU uisifiayo !:-(
--------------------------------------------------------------------------------------------------
Mpate tu RAY C akupe dawa iitwayo SOGEA SOGEA
AU pata baadhi ya PICHA zangu na baadhi ya WADAU ambao hawakunitenga maeneo fulani.


















AU wapate tu
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 7:46 AM 0 kommenttia
Moja ya udhaifu wa binadamu ni KUFANANISHA!
Hukawii kusikia mtu anamfananisha mtoto mwenye kitumbo kikubwa kutokana na KWASHAKOO kuwa anafanana na BABU yake mwenye kitumbo kikubwa kutokana na POMBE ya ULANZI.
Kirahisi tu, waweza kuogopwa au kupendwa kutokana na staili yako ya nywele kama MADENGE .
Watu kirahisi wataamini kuwa ULIFANYA kama unafanana na waaminiye ANAFANYA!
Ukifanana fanana na MWIZI au MALAYA pale maeneo, kama hawajui kuwa wewe swala tano au 24, watakutendea kwanza kama wamtendeavyo MWIZI au MALAYA .
Staili ya jamii kukushuku kutokana na KIMINI SKETI chako, PARA LAKO kama mvuta bange au MARASTA YAKO kama kichaa, INAWEZA KUKUSAIDIA KUPATA au KUKOSA.
Na staili ya jamii kutengeneza tuaminivyo kuwa PADRE au SHEKHE ni mwaminifu kuliko MFYEKA MAJANI au MUUZA KIGENGE pale kona, imesaidia sana kuwasababisha WAHALIFU wakubwa kutostukiwa na watenda wema kuonekana MAFALA .Na labda inasaidia wake na wanaume wa watu fulani KUONJA KITUMBUA wakikinai MAANDAZI kila siku,hasa pale watu wafikiriapo kuwa kwa sababu wewe WINNIE MANDELA basi huwezi kumfikiria CHAKUBANGA katika kutimiza kukuna NAZI.
INASIKITISHA sana kuwa BINADAMU WENYE AKILI bado tunadhani kuwa KIBAKA , MHUNI , MALAYA au MSWALIHINA ana sura fulani au anavaa kitu fulani na sio USHANGA ULE kiunoni.
DUH !
NAACHA topiki!
SAMAHANI!
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 2:16 AM 0 kommenttia
Ukinigusa pale..
........unaamsha huku
Ukiamsha kule
......naanza kustukia maswala ya NINI na KWANINI.
NINI na kwanini, ni maswala ya kujiuliza tu.
NA.....
Nikianza kujiuliza , nitataka kupata majibu.
AU...
Bila shaka nitaanza kutafuta majibu.
Tatizo la majibu ni kwamba, hata MAJIBU ya UONGO ni MAJIBU kwa afikiriaye kapata jibu.
Kwa yoyote MJANJA, usicheze na ufikiriaye mjinga ambaye KASHATEKENYWA na KASTUKIA, na anatafuta MAJIBU kutokana na UJANJA wako.
Akipata jibu , laweza likawa si jibu ulilotegemea!
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 4:22 AM 0 kommenttia
Kama mimi na wewe tushafundishwa maswala ya UMUHIMU wa BAJETI halafu tukachacha katikati ya mwezi, wakati mwanzo wa mwezi tulikuwa na pesa yakukupitisha mwezi mzima , kwa mtazamo mwingine , wewe na mie hatuna tofauti na aliyefundishwa UMUHIMU wa MISITU halafu akakata mti ,akifikiri atapanda mwingine baadaye kidogo kabla msitu haujaisha.
Tofauti ni kwamba ukichacha unaweza ukakopa au kuvizia misiba mpaka mwezi ukapita(si kwenye harusi ukizamia ni rahisi kustukiwa kuliko msibani?), na ukikata mti , kuotesha msitu mpya ni vigumu ,kutokana na muda au hata hali ya hewa iharibikayo au hali iuleteayo mizengweMTI KUKUA hasa pale UKUAPO wakati tunautolea macho kutokana na msitu kutokuwepo.
Sasaaaa....
Yule , yeye na mimi, tunaweza kukubali kuwa mtu na akili zake hawezi kuondoka tu nyumbani kwenda kujikatia miti bila sababu. Tunajua karibu watu bilioni tatu wanatumia kuni na mkaa ili kuhakikisha kisamvu au maharage yameiva.Kwa hiyo kila siku kuna watu bilioni tatu kinamna lazima wanyemele mti fulani uwe umekauka au la:-(
Halafu ,....
....kwa wale ambao hawajawahi kukata mti , napenda kuwakumbusha kuwa kukata mti sio kazi rahisi sana, hasa ukikumbuka wakataji miti waliowengi duniani hawana vifaa virahisishavyo sana kazi hii ya kutengeneza jangwa ,zaidi ya shoka , panga au goti.
Basi labda ....
....kuna watakao sema kuwa kupanda mbegu ya mti au kupanda mti ni rahisi kuliko kukata mti na wakaanza kushangaa kwanini wakatao mti walio wengi hawapandi mti.
Inawezekana ukafikiria hivyo kirahisi kama utasahau sifa ya binadamu ya kufikiria ya leo zaidi ya ya kesho au mtondogoo.
TATIZO hili la kufikiria kesho au kizazi kijacho linafundishika zaidi hasa pale binadamu anapokuwa na uhakika wa kwake binafsi kuhusu kesho au baadaye ataimuduje kitu ambacho ni kigumu kwa maskini .
Swali:
Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 3:17 AM 2 kommenttia
Kama unaishi inamaana unathaminisha vitu.
Kama unathaminisha vitu inawezekana unadharau kitu au kuna kitu unafikiri kinathamani zaidi ya kile , hiki au hata nywelenywele za kikwapa cha nanihiii.
Lakini ....
Labda thamani ni kama noti ya pesa ambayo ni karatasi tu, wengi mkiwa na machale nayo, inageuka kuwa kama pesa ya Zimbabwe mwaka 2008, ambayo hata uwe na noti ngapi, unawezapata tatizo lakukusaidia kununua vikusaidiavyo kukuwezesha kwenda choo.
Labda hata thamani hata ya maneno inafanya tuamini kuwa maneno fulani ni machafu na mengine ni ya kuimbia kwaya KANISANI au pale chini ya MBUYU.
AU
Labda kweli kuna uchafu na usafi, hasa kama kwako vipodozi ni usafi ingawa huvilambi, mate kwako ni uchafu ukitemewa lakini si ukipigwa busu, au ukioga unaamini ngozi ishakuwa safi kama tu uaminivyo ukipiga deki, sakafu ni safi.
Angalau bado inasemekana;
HESHIMA ni kitu cha BURE.
NA....
Labda ni kweli kuna kitu umewahi kufanya kwa thamani iitwayo bure!
Lakini ni kweli inasemekana ,
.... kuna vitu baadhi ya watu wanaweza wakakiri kutoweza kuthaminisha, kama vile, mapenzi yao kwa wazazi , ndugu ,jamaa au limpezi nanihino.
Swali:












Lähettänyt SIMON KITURURU osoitteessa 1:26 AM 0 kommenttia