Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

JE UNAWAKUMBUKA WAAFRIKA WASIO NA RANGI?

>> Friday, May 26, 2006

Tokea mara ya kwanza kumsikia Salif Keita ,nilishindwa kujizuia ila kuwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wake. Wakati nikijiandaa kwenda kuangalia onyesho lake jumanne ijayo hapo mjini Helsinki, nimeshindwa kuepuka kukumbuka kuwa yeye ni miongoni mwa Waafrika ambao pambano lao husahaulika.



SALIF KEITA
(The Golden Voice Of Africa)














Hili ni pambano lakukubalika katika jamii ya Waafrika na hata ya watu wenye rangi nyingine, aambalo limejaa kasumba na mila potofu za kuwatenga mazeruzeru. Kwa wale wasikiliza muziki wa reggae wanaweza kumjua Mzee Yellowman . Huyu Mjamaika namuingiza hapa ilikuonyesha kuwa hili pambano ni dunia nzima. Kwani hata yeye ukifuatilia maisha yake utakuta kuwa mila hizi za ubaguzi zilimdhuru sana huko Jamaika.

KING YELLOWMAN













Tukirudi hapa barani Afrika, huko nchi za kusini, inasemekana kumeingia mpaka imani potofu kuwa mtu akifanya mapenzi na zeruzeru basi atapona UKIMWI.

Ukisikia mambo watu wanayohusisha uzeruzeru nayo,utashangaa mwenyewe! Soma zaidi hapa. Kuanzia kuwa wamelaaniwa, wanaleta bahati mbaya mpaka kuwa wana mapepo wachafu. Mpaka dunia hii ya leo, achilia mabali siku hii ya leo, inashangaza kuwa watu wanashindwa kujua kuwa watu hawa walichopungukiwa ni chembechembe za melanin tu, ambazo ndizo zitufanyazo wengine tuwe weusi,wengine ,weupe , kahawia, nk. Lazima tukumbuke kuwa watu hawa bado wananyanyasika mashuleni , makazini , na katika jamii kwa misingi isiyo kuwa na ukweli. Cha zaidi cha kujua ni kwamba kutokana na kukosa hizi melanin , basi huathirika kirahisi na jua. Hupata cancer ya ngozi kirahisi kuliko watu wenye chembechembe. Pia huwa wana matatizo ya macho(vision). Basi sasa kwanini wanyanyaswe kwa mambo hata ambayo hayahusiani nao?


PRINCE YELLOW











Kabla ya kumaliza, nisingependa kusahau kumtaja Prince Yellow au Al Beeno na pia huyu mtoto wa Malawi Geoffrey Zigoma , wakiwatu ni baadhi ya wanamuziki wanaonikosha roho

GEOFFREY ZIGOMA













TUSISAHAU KUUNGAMKONO MAPAMBANO YA KUONDOA UBAGUZU HUU AMBAO UMEKITHIRI BADO KATIKA JAMII ZETU.

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Jeff Msangi 8:27 pm  

Bado sijamaliza kusoma yote uliyoandika hapa,ila mwaka huu mwezi wa saba tarehe nane,Keita ni mmojawapo wa performers kwenye AfroFest hapa Toronto.Nadhani itakuwa matata sana.Naupenda sana muziki wake pia.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP