Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

TANGAZO:AFRIKA INATAFUTA VIELELEZO NA NGUZO ZA KUEGEMEA.(Ukiziona Mtaarifu mwenzio)

>> Thursday, May 25, 2006

*Papa Wemba was not just a singer. He was also the prince, the "Pope" of SAPE.
Young men rushed to become clothes conscious dandies and carefully followed the special codes of SAPE, from their shoes to their hair style. A form of anti-poverty and anti-depression rebellion, SAPE was also a way of fighting against the dictatorship of the "abacost", a local version of the three-piece suit and virtually an official uniform of the Mobutu regime.
-RFI MUSIQUE

*Congolese immigrants living in Paris and Brussels, were busy living the Sapeur lifestyle - constantly hustling for money, keeping up with Papa Wemba's fashion ideology, and pursuing a `dedication' by Wemba, who is paid a lot of money by his fans in order to sing their names in his new album. Bragging and boasting, loud and proud, constantly advertising themselves and each other, they are stars on a stage they mentally construct in the absence of real ones. -IMDb



*Joseph Kony considers himself quite a good Christian, and he wants Uganda to be a Christian nation.If the LRA wins, Kony has promised that Uganda will become a theocracy, with laws based on the Biblical Ten Commandments.
-NNDB

*Joseph Kony adds: "Most people do not know me... I am not a terrorist... I am a human being, I want peace also." -BBCNEWS






Inasemekana binadamu alitokea Afrika, kwa hiyo si vigumu kuamini Muafrika ni miongoni mwa binadamu aliyekuepo muda mrefu hapa duniani. Hivyo lazima Waafrika tuna vielelezo(role models) au mifano mingi ambayo ingeweza kutupa kiegemeo wakati wa matatizo na mifano ya kufuata kujijenga kiakili, kiuchumi, kiutamaduni.....-au basi japo angalau kutupatia kujiamini katika mambo yetu. Hili si jambo dogo na kinanifurahisha kuwa bado watu tunaendelea kutafuta vielelezo hivi ingawa kama watapatapa maji hata nyoka unaweza ukafikiria ni mzizi ambao utakuokoa usichukuliwe na maji. Kuna mifano mingi ambayo ni rahisi kuiona ambayo inamwezesha Muafrika au mtu mweusi kutembea kifua mbele. Lakini pia iko mifano mingi zaidi ambayo inamsababisha mtu kuona haya kuonekana mbele za watu. Mifano mingine ni hii ya jinsi Waafrika tunavyotapatapa kutafuta nguzo na vielelezo vya kutusaidia.

Wenzetu Wamarekani weusi bado wananyanyua macho kutazama vielelezo kama vyakina Malcom X, Martin Luther King vikiwa mstari wa mbele.Lakini kwa miaka hii ya karibuni wamemchukua hata Mandela kama kielelezo chao. Sisi Waafrika hatuko nyuma tumewachukua akina Malcom X na Martin Luther, halafu Mandela ndio pekee bado ang'araye katika bara zima. Kwa mtazamo wangu mtu kama Nyerere pamoja na mafanikio yake mengi bado anachukuliwa kuwa ni kielelezo na nguzo iliyoshindwa, kutokana na baadhi ya mawazo yake mengi kushindwa kutimilika.Akina Mkwawa na wakina Kinjekitile hao ndio kabisa hatuwakumbuki, natukiwakumbuka ni kama hadithi isiyotufundisha kitu leo. Kitu ambacho si ukweli. Ila kukatisha hadithi ndefu , ningependa kusema vielelezo na nguzo zetu nyingi tunaziacha zife. Ila hii ni mifano ambayo iko wazi kupita kiasi. Ningerudi katika mifano miwili ambayo naiona inaelezea jinsi watu tunavyotapatapa kutafuta nguzo ya kuegemea katika maisha yetu ya leo kama Waafriaka.Mifano niliyopenda kuitumia ni Papa Wemba nguzo ni Nguo na Joseph Kony amri kumi za Mungu. Ingawa ukifikiria kidogo tu utapata kibunda cha mifano.

Mfano wa kwanza nautoa kwa Papa Wemba. Huyu Mkongo mimi nauhusudu sana muziki wake. Tukiachana na muziki kunakitu kingine yeye hujulikana nacho.Yeye ndio aliyeutia umaarufu Ukongoni mtindo wa kuvaa nguo za ghali na kusababisha kwa baadhi ya wafuasi wake kuamini katika mavazi kama vile watu wengine wanavyoamini katika Ukristo na Uisilamu. Yeye alipata kiegemeo katika nguo za ghali, akaanzisha kitu kinachoitwa SAPE('Société Ambianceurs et Persons Élégants') .Kuna documentary yake moja ukiiangalia utaona jinsi Wakongo kuanzia Afrika mpaka Brussels na Paris wanavyohangaika kutafuta pesa ilitu wasipitwe na toleo jipya la nguo kutoka mwanamitindo ya nguo Mfaransa, Mjapani au Muitali . Watu wako tayari kuiba ilitu wavae Armani, Gucchi,...nk. Soma hapa mahojiano ya watengeneza documentary hiyo. Ukifuatilia hii dini ya nguo ambaye papa wake ni Papa Wemba , utakuta kuna dalili nyingi zionyeshazo utapatapa maji wakujaribu angalau kujisikia kuwa kuna kanguzo kakuegamia. Tatizo lake ni moja tu. Kanguzo haka hakadumu kwa maana mitindo inabadilika kila kukicha. Hivyo Dini hii ya Kiafrika ambayo roho mtakatifu wake ni nguo za kutoka mtoni za bei ghali kama kielelezo na nguzo, naamini watu inabidi wafikiri mara mbili. Ndio utatembea uonyeshe maringo yako lakini sinauhakika na uwezo wake wakuziba uwazi katika maisha ya Muafrika na sifa ya Uafrika. Nguo kama mavazi tu sinatatizonalo lakini nguo zinapozidi kuwa kama mavazi naananza kuingiwa na mashaka.

Katika kutafuta kiegamio, mwafrika mwenzetu Joseph Kony akakipata kwenye biblia. Huyu Mwafrika mwenzetu mkereketwa wa dini na Afrika amekuwa vitani tokea mwaka 1987. Amejitahidi sana kupigania haki ya kutawala Uganda kikristo na kufanikiwa kuua watu katika maelfu, wengi tu kubakwa au hata kukosa kwa kukaa . Yeye anaamini kuwa amrikuu kumi zilizoko katika biblia zingeineemesha Uganda. Chakushangaza amefanikiwa kuzivunja hizo amri kumi mara nyingi tu katika kutafuta amani na maendeleo Uganda. Ila anasema anapenda sana amani.Msome hapa . Anakaririwa akisema anataka amani, wakati akishikishwa kitita cha dola elfu ishirini na makamu wa Raisi Sudani kusini. Mtu anaweza kumuamini, lakini je kielelezo anachokiegamia kinatufaa Afrika? Kama kinafaa sana mbona kinamshinda mwenyewe?

Naamini tunahitaji muelekeo Afrika. Mandela pamoja na upungufu wake amejaribu vyakutosha. Mandela amechoka sasa na ukweli ni kwamba Afrika inahitaji nguzo na vielelezo vingi. Tunazo nguzo na vielelezo vingi ambavyo tumevilaza. Inabidi tujaribu kuvifufua. Ushujaa wa watu kama akina Mkwawa inabidi urudi midomoni mwa watu. Pia tunahitaji mifano , vielelezo na nguzo mpya za kuegemea Waafrika. Kama ni wewe basi jitokeze. Akina Nyerere, Nkurumah na wale wote enzi ile walikuwa ni vijana wadogo tu. Usimsahau hata Gaddafi katika kundi hilo. Naamini nguzo na vielelezo vipya kama akina Kikwete hawatavitoa basi akina Jeff Msangi tunawasubiri.

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP