Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

TUNASAHAU faida za SIRI ya ASIYE na MPENZI au TUSIYEMJUA kuvaa chupi SAFI!

>> Thursday, October 16, 2008

Jambo lako binafsi zuri si lazima likae uchi kwa jamii kushuhudia , kwa jamii matunda yake kushuhudia.

Kitu ambacho hata hakijulikani, chaweza kuwa ni chanzo cha wewe kunichekea au hata kuwa na muda wa kunisaidia , kumsaidia ,kama sio kunionyesha chumba cha kujisaidia.

Tusichojua kikusumbuacho , chaweza kusababisha uwe mkali bila sababu katika kiwanja cha penzi .

Unawezaficha siri kwa kujifanya mzuri, lakini mficha siri hufanikiwa kuficha siri kwa yule tu ambaye si makini.

Siri yako ya KUBANA KIJAMBO, yaweza kujitokeza kwa utofauti wa staili yako ya mkao kwa akujuaye.
Siri yako ya kubana mkojo , yaweza kujitokeza katika mwendo wako wakwenda msalani kwa akujuaye.
Siri yako wakati unaongea na mpenzi wa siri , inaweza ikawa katika staili yako ya kunong'ona kwenye simu huku ukijichekesha katika visivyochekesha.

Siri yako wakati unadanganya , inaweza ikawa jinsi tu unavyosisitizia hoja kwa akujuaye.

Sasaaaaa.......!

Aina ya siri ni muhimu katika kugundua hata faida za ukubwa wa sehemu za siri.

Cha ajabu.....!

Tanzania mpaka yajulikanayo hunekana kama siri , ingawa wenyenavyo hawafanyi siri kutuonyesha ukubwa wa maeneo wayazungushiayo uwigo kuficha siri.

Pamoja na ustaarabu wa binadamu wengi katika ya faragha kuyaacha faraghani, huhitaji kuvua mtu nguo kugundua walio wengi hawana kificha sehemu za siri au hata imeshindikana kuvaa chupi nzuri.

Cha kutisha ni kwamba , kwa mwendo huu walio wengi watafikia kubakia na siri moja ambayo sio siri ,kwa sababu tayari unaona MATAJIRI na WANASIASA wanajijengea ngome ili wengi wasione kifichwacho kwa siri.


Na......
Wanasiasa wako makini , kutuibia mpaka maini
Nasi kwa matumaini , twategemea matatizo yetu watakabili

Labda tuwakumbushe...

Kitu tusichokijua kwa mtu tusiyemjua tunayepishananaye , chaweza kuwa ndio kilichotuhakikishia usalama au kukabwa hata pale sehemu tunapopajua.

Na inajulikana.....

Matajiri wanaogopa masikini na wanahitaji kujua SIRI ya furaha ya MPWEKE apatayo kwa kuiangalia chupi yake yenye rangi nzuri hata kama haitashuhudiwa na kipenzi katika kibanda cha faragha.

Na inajulikana .......

Wanasiasa wanajua kuwa sasa hivi waliowengi wanastukia kuwa hawafaidiki na siasa zao ingawa bado wanadanganyika kirahisi kwa stori za danganya toto ambazo zinakubalika kutokana na kitu ambacho sio siri chenye uhusiano na elimu na umasikini huohuo.

Muhimu kukumbuka kuwa , wenyenavyo hawataweza kufaidi walivyo kuwa navyo kama WASIONAVYO wataendelea kusahauliwa na kuendelea kutembea na siri ya machungu ya kukosa na kuwa na uhakika kuwa wenyenavyo ndio tatizo.

Wanasiasa na matajiri kumbukeni kuwa mtafaidi sana kwa kuhakikisha angalau na wengine wanapata mpatavyo hata kama vyenu bado ni vya dhuluma.

Hakuna atakaye taka kukuvamia na kuhatarisha maisha yake ili akuibie TV yako ya inchi 120 kama angalau anako kaTV kake ka nchi 32.

Utafaidi kutembea na LIFERARRI lako ikiwa angalau na wengine wana vi RAV 4.

Hata pesa za EPA labda hakuna ambaye angefuatilia sana kama watu wangekuwa wamejazwa mapesa angalau ya kuwa na uhakika familia itakuwa poa tu kesho na kesho kutwa, na hata vijipesa vya kuongezea maisha kutokana na kale ka UKIMWI, zipo.

Labda.......
Inategemea unaficha nini , kwa umahiri wako wa chaguo la ukubwa wa sehemu za siri kuwa mahiri.
Kifichikacho leo , kucha yake yaweza kukiumbua kesho .
Ikiwa huna ili, labda lile au kile chaweza kukahidi kuingia kwa ulaini katika pango hilo la siri.

Ukubwa wa jambo la siri waweza kugundulika SIKU ya KUFA kwa NYANI ambapo miti yote huteleza.
Swali:

  • Hivi umevaa chupi nzuri ee?
  • Hivi unataka chupi yenye rangi nzuri kutokana na yule akusaidiaye kuivua atakavyokujaji kutokana na kificha faragha au pale uianikapo mbele ya macho ya jamii?
  • Hivi maswala ya chupi ni maswala ya faragha eeh?
  • Unauhakika ninaongelea upumbavu gani?

DUH!
Naacha topiki!

Ngoja tumpate Henri Salvador aje tena na Jardin d'hiver


Au tu HAFSA na BANANA ZORRO watupe kitu PRESSURE.

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP