Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KUPAMBA maumivu kwa KUKIRI!

>> Saturday, May 03, 2008

Ukikiri, unatua MZIGO wa siri na UNAANZA kutibu ugonjwa wa nyuma YA KWANINI.
Nyuma ya Kwanini kuna ile kitu yenye jina fulani lakini inawakilisha NINI kimefanyika au hakikutendeka.

DUH!

Watu hupenda kusikia kutoka kwako mwenyewe umekiri walichosikia kuwa UMETENDA.
Kusikia kutoka kwa mwingine ni CHAKULA kisichoungwa, kuna ladha fulani MTU fulani anaweza kuhisi chai imekosa chumvi .

Lakini....
...IKIWEZEKANA ,usikiri JAMBO kama unaweza.

UKikiri , unawaondolea watu fulani faida za kubunia jambo(benefit of the doubt).

Ukikiri inasemekana kuwa unatatua jambo, ingawa inawezekana unasambaza maumivu kwa mwingine kama sio wengine kwa kuwasababisha kuishi wakijua ni kweli ulijinyea kwenye harusi ya jirani.

Binadamu anajaribu sana kuondoa kero maishani mwake na ni rahisi mtu kujisahau kuwa hata ufanyeje, wewe kama binadamu, basi wewe si malaika na kwahiyo utakereka tu sehemu fulani ingawa hutaki.

Kukiri ni moja ya njia tu binadamu hujaribu kutumia kukwepa KERO moja kabla hajadakwa na KERO jingine kwa sababu umekiri.

NIsikutishe, KIRI tu kama unapata AUHENI.
Swali:

  • Ushastukia kila siku kuna kitu unakiri hadharani ila huiti kitendo;KUKIRI?
  • Unafikiri ukikiri, UNATATUA au unabadili mchezo na kukabiliana na tatizo kwa kutumia kona nyingine?

Lakini....
......Ukifumaniwa unakula denda hata bila kukiri kuwa ulipata uroda, kuna watu watataka kujua na UKIRI kama ilikuwa chuma mboga au ulisomea umishenarini.

Lakini....
....watakao UKIRI hata wakijua, haikusaidii sana wala haiwasaidii sana kama unakumbuka dunia ilikuwepo tu kabla hujazaliwa na kufanya watakacho UKIRI .
Wanaodadisi jambo, hawataishiwa jambo la kufanya usipokiri kama bado wanataka kuwa katika uwezo wa kula na kunya(samahani, kwenda haja kubwa) kesho na kesho kutwa.

Basi bwana!
Kiri tu kama INATATUA!
Baadaye basi!


Pata tu swala kutoka kwa IMAM mtoto......akikuuliza DO YOU KNOW ALLAH?

Au pata tu Mahubiri kutoka kwa Mchungaji mtoto....


Au mshangae mpiga ngoma mtoto Kanisani......


AU msikilize tu MTOTO katika fani fulani za siku hizi.....

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP