Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

NIKIKUANGALIA wakati UNA-SHAbikia, CHEkelea au ukiLIA, TIMU yako IKISHINDA!

>> Wednesday, April 30, 2008

Ukiwa na TABIA ya kumtazama binadamu, utastukia kuwa huhitaji televisheni wala kucheza bao ili ujiliwaze.

Binadamu hakosi jipya la kukustaajabisha, kama unatabia au jicho la kumchunguza.

Na....
.....ukijenga tabia ya kumtazama sana binadamu , iko siku utastukia kuwa, kama ni kubwa zima halafu halitumii kinyoleo, linaweza likawa lina nywele nywele zinakua kuanzia mashavuni kama ni janaUME, au linakua manyoya mpaka maeneo ambayo kama halijavaa kificha nyeti, linaweza kuwa na kipilipili mpaka maKWAPAni. (Na cha ajabu ni kwamba ,inaweza ikawa ngumu kwako au kwangu kufumbua fumbo la umuhimu na madhumuni ya kwanini manyoya na nywelenywele hizi nyingine humuota huyu binadamu maeneo fulani fulani bila ya faida iliyouchi ).


Binadamu kwa jina la ushabiki anaweza kulia, kupiga mtu au hata kujiua ,timu yake ikishindwa.

Binadamu hata kama ni mchezaji na achukiaye tabia za kisenge, unaweza ukakuta kampiga busu, akamkatikia kiuno na kumkumbatia mwenziye mwenye sehemu za haja ndogo zilizo fanana na zake ,KISA, amefunga goli, bila kukumbuka kuwa tabia hizo hizo alizofanya kwa kufurahia na aina ya mtu aliyemfanyia vitendo hivyo, ukijumlisha ,ndizo tabia za kisagaji ambazo yeye na jamii yake kama ungeondoa mpira na kuweka muziki wa bluzi , basi angepigwa mawe mtu na wapambe kwa kosa la USHOGA.

Inawezekana UMUANGALIAVYO mtu , unaOAnisha mahali alipo na nini kinafanyika,ili kuwa na uhakika na kitendo kuwa; ingawa anaguna, haiwezekani akawa anajisaidia haja kubwa sebuleni.
Si agunaye chooni hata kama kajikwaa huko msalani , atashukiwa tu anaguna kwa sababu anakwenda starehe kubwa?

Labda ni ka-ubinadamu kakupenda ushindani na kushinda, kamsababishiako binadamu afurahie timu yake ikishinda na ahudhunike akishindwa.
Lakini si kufurahia kushinda na kuhudhunikia kushindwa , vyote ni vitu vya muda mfupi tu?

Au labda ni kaudhaifu ka-kibinadamu kakutojua mwisho wa mchezo matokeo yatakuwaje, kamleteako binadamu tamu tamu ya kufuatilia mchezo mpaka mwisho.
Lakini si wengine huwa na uhakika wakushinda au kushindwa katikati ya mchezo au kabla mchezo kuisha?

Labda ni ka-utamu wa kushinda au uchungu wa kushindwa , kasababishako unaendelea kuwa mshabiki wa timu fulani.
Swali:

  • Unajua ushabiki , inawezekana ni aina ya ugonjwa wa akili kama lilivyo penzi?
  • Ushastukia mshabiki , nukta kadhaa baada ya kushinda au kushindwa anaweza kufanya ambacho hawezi kukiri waziwazi amewahifanya maishani?
  • Ugonjwa wa akili ni nini?

SAMAHANI nawaza tu!
Si unakumbuka hiki ni kijiwe cha Simon kitururu-MAWAZONI?
Siku njema!

Tulia na Acoustic Blues vibes kutoka kwa Eric BIBB akikupa GOOD Stuff

Au turudi tu kwenye Zouk Love ikija katika wimbo La Zouk Horay kama iletwavyo na Kaysha na kuwa remixed na DJ DUKA(samahani video inaweza kumkwaza mtu fulani au kuwa inamdhalilisha mtu fulani kwa mtazamo wa mtu fulani.Kama mtoto au mkwazika kirahisi, usiangalie .SAMAHANI!:-()

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 2:08 am  

Kwa mara ya kwanza na thubutu kuzifanyia vujo "buttons" za keybord yangu, kwa kuandika comment hapa katika blog yako iliyotukuka!
Niwenye hekima na uwezo wa kutafakar tu ndio wanaoweza kujuwa undani na maana ya maneno yako. Maneno yaliojaa busara na hekima.
Ni mfano wa dawa chungu ilopakwa sukari kwa juu, ha ha, ukikosea kuimeza utaupata uchungu wake! lakini juu ya yote ni dawa, inaponesha!

Hongera kaka, wewe unahekima za watu wa karne 20 zijazo (umewahi sana), unajuwa kuyaangalia mambo in 3-dimensions (3D) at High Definition (HD)

Simon Kitururu 10:43 am  

@Bablii:Asante Mkuu!Jisikie uko Nyumbani hapa kijiweni. Usisite kuandika comment Mkuu

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP