Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

NAKUPENDA!Si nilikupigia SIMU?

>> Friday, April 25, 2008

Ukimya unatafsiri nyingi.
Kirahisi tu , unaweza kutafsiri ukimya wa mtu kutokana na nini ulishaanza kumfikiria utakaye jibu kutoka kwake.

Unaweza mpaka kupata jibu kutoka kwa uliye jaribu kuwasiliana naye bila mafanikio, kuwa jamaa ananikwepa au ananidharau.

Wajanja husema ukiwasiliana na jamaa atakusikia au hata kukusoma.

Lakini....
...ukisikia au kusoma cha mtu, inawezekana hajawasilisha au ujumbe wake kuhusu jiko , wewe ukaelewa anazungumzia choo kichafu ambacho kina funza funza fulani WANONO.

Lakini....
...funza funza wanono watutiao kinyaa, kichefuchefu au hata hamu ya kutapika, wanaweza wakawa ni watoto wapendwa jichoni kwa mama yao NZI.

DUH!

Ningependa kuchukua nafasi hii kuomba msamaha kwa wote ambao nimeshindwa kuwasiliana nao.Najua ni watu kibao ambao wamekata tamaa nami kutokana na ka-ukimya fulani.

  • Samahani kama sijakupigia simu wala kupokea simu!
  • Samahani sijakujibu ile barua, e-mail wala labda sikugeuka uliponipigia ule mluzi!
Tuko Pamoja na WIKIENDI NJEMA!

Lakini..
.. kabla sijaondoka kabisa kwenye topiki ya kuwasiliana fulani,
nimefurahi kufanikiwa kukutana uso kwa uso na blogger wa Kitanzania ambaye tulikuwa tunajuana mtandaoni bila kuwahi kuonana uso kwa uso a.k.a EDO NDAKI

Pata baadhi ya picha zangu nilizozidaka baada ya kukutana na EDO NDAKI , pamoja na WADAU wengine.
Photobucket
Kwa wasio jua , huyu ndiyo Mzee EDO NDAKI:
Photobucket
Hapa nilijibanza naye.
Photobucket

Photobucket
MKUU wa Kikao a.k.a RAYMOND alikuwepo.

Tulia na HEAVY D akikuambia NUTTIN but LOVE

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP