Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kuna WATU wakoKimYa lakini wameona na kusikia! UKIWAPA upenyo ,WATAKUULIZA kama USHAWAHI kuugua Ugonjwa wa akili.

>> Friday, April 25, 2008

Kuna topiki fulani watu hukwepa kuongelea kutokana na topiki ilivyokaa kushoto.

Ukimpa mtu nafasi au kianzio cha sentensi kuhusu topiki asiyo kuwa na uhakika inakuathiri vipi ingawa akilini mwake anaona inauhusiano sana na jambo la kutia aibu , atakuuliza .

Ukimpa nafasi au kumchekea mara baada ya kumpa tabasamu wakati anahamu na wewe, anaweza kupata nguvu ya kukutongoza.


Cha ajabu ni kwamba , asicho kuuliza uso kwa uso anaweza kuwa kasha jadili na wadau wengine mara mia kadhaa na kufikia kwenye uhakika kuwa lile gari lako umelikopa.

Kuteta, umbea au hata kumuongelea mtu kama hayuko kijiweni, ni BOMBA la SANAA kwa atakaye urahisi wa kuhakikishia ubongo wake alichosikia kwenye redio za mbao ni kweli.

Umbea na kutetana ni dalili kwamba unamuda zaidi katika maisha yako ambao huutumii kujishughulikia au kufanikisha yanayo kuhusu wewe binafsi.

Umbeya , kuteta, uzushi au hata kutungia watu vistori visivyo vya ukweli ni bomba la kazi nzuri kama una hobi ya UMBEA.
Si unaona mpaka PEREZ HILTON kawa milionea kwa kuongea umbea na uzushi?


Si umeona Tanzania kuna magazeti mangapi yanayokiri ni ya UDAKU?
Watu hupenda kuwa na taarifa zako ambazo wanahisi hutaki zijulikane.

Swali:

  • Unahisi ni kwanini humuulizi , wakati unataka kujua kama kweli ana mke mdogo pale mtaa fulani au kama bado ana kaudhaifu ka-mapenzi yake ya watoto wa sekondari ya KIFUNGIRO, kama usikiavyo?
  • Unafikiri ni kwa nini huulizi ingawa unataka kujua?
Lakini.....:
...Ukiuliza aliye ulizwa anaweza kuhisi unajua tayari ,kitu ambacho kinaweza kufanya aanze kukukwepa.
....Ukiuliza maana yake umekiri kuwa hujui.
....Ukiuliza inaweza ukawa umetoa mwaliko wa kutaka kudanganywa.

INAWEZEKANA hujauliza kwa sababu hujapewa nafasi, kianzio cha topiki au kuchekewa, USIKONDE!

Unakumbuka lakini jinsi gani mazingira, topiki iliyokuwa hewani ....vilivyochangia ujisikie huru kuulizia au kutongoza?

Unajua mara nyingi ni wewe , mimi au yule tutengenezao mazingira ya kurahisisha mpaka kutukanwa?

DUH!
Inawezekana nimeshakutengenezea mazingira ambayo utataka kuniulizia ambacho nitakwepa kujibu!:-(

Inaruhusiwa kutojibu ingawa kwa mimi kutojibu unaweza kuondoka ukifikiria ni kweli mimi bado bikira.

NAACHA basi!

Nakutakia kila la KHERI katika maisha haya ambayo yanasababisha tutake kujua mpaka visivyo tusaidia kama vile :hivi yule msichana kavaa chupi au kaptura chini ya lile gwaguro.

Tulia na Mu-Itali (ambaye usipomuona unaweza kufikiri mweusi) kwa jina la Alberto D'Ascola A.k.a. AlBorosie


Au pata ujumbe wewe kama MTU MWEUSI kutoka kwa MORGAN HERITAGE wakimkumbusha MTU mweusi hali halisi ya MTU MWEUSI,
katika songi, FALLIN RACE

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 7:13 pm  

Mimi mdaku...nani anababaishwa na nani?

Simon Kitururu 7:58 pm  

@Serina::-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP