Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Maswala ya ,`HUYU demu asingekuwa AMEOLEWA, ningemtongoza!´

>> Sunday, April 13, 2008

DONDOO:

  • Hapa siongelei swala lililo karibu na swala kama la Raisi Mandela kumuoa mke wa rafiki yake Samora , baada ya Rais huyo wa Mozambiki kufariki.
Inawezekana kabisa ukinyimwa ,ukataka zaidi!
Inawezekana kabisa unataka na kinakufikirisha kwa sababu huna!
Vile viatu ambavyo ushavisahau chini ya kitanda, inawezekana mwenzako anavitamani leo hii katika duka fulani.

DUH!

Unaambiwa, MAJANI huonekana yakijani zaidi kwenye bustani ya mwenzio.
Ulichonacho , inawezekana umekizoea mpaka hustukii ni jinsi gani kilivyo kikali.

Ukionacho mtaani , na haswa kile ambacho hukijui, kina weza kikawa kinakuvutia sana tu.
Ukweli ni kwamba ukitamanicho chaweza kukukinaisha hata kabla hujavuka dakika tano yakuwa nacho.

Cha mwenzako ambacho unauhakika huwezi kukipata kinabakia kama kipimo cha yale ambayo akilini mwako umependa kuyakubali kuwa ndio ukweli ukizungukacho hicho kitu ulicho amua kukiita kitu kizuri.

Naamini si kitu kibaya kutamani cha mwenzio kama kinakusababisha upige hatua fulani mbele , katika kujijua au hata katika kukufanya ujitume kufanya mambo vizuri zaidi ilikufikia mwenzako alipo.

Tatizo ni pale tu kama tamaa ya yale usiyonayo yatakujenga chuki kwa yule ufikiriaye anacho kukuzidi.

Swali:
  • Unauhakika ulichonacho si kizuri kuliko cha mwenzio ikiwa kinakutosheleza?



DUH NAACHA na moja kwa moja natoka nje ya TOPIKI!

Huu wimbo hapa chini ni kwa wale (hasa Marasta) wasionielewa nikisema mimi si Rasta , hasa kutokana na ukweli sichani Nywele (kama ionekanavyo pichani) , hata baada yakujieleza mara kedekede kwanini mimi si RASTA.
Photobucket

Tulieni basi na hawa MARASTA wanaojulikana zaidi katika PUNK ROCK kutokea miaka ya sabini, ambao wale MARASTA waaminio kuwa urasta unaendana na ROOTS REGGAE pekee, wanakwazika hata kwa kuwasikiliza.Wapate basi BAD BRAINS

DUH!
Usitishike!
Niko na ERIC BIBB (niliyenaye pichani) ....masikioni.
Photobucket
Tulia naye basi!

Kwa mara nyingine , ASANTENI MARAFIKI wote popote mlipo kwa yote!

Nawatakia kila la heri katika harakati za kuishi!

Asanteni pia marafiki ambao tumebahati kukutana hivi karibuni !

Mungu akipenda tutakutana tena!
Baadhi mnaweza kujistukia katika picha zangu hizi katika filmloop....

Tuko pamoja na BAADAYE basi!

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Chemi Che-Mponda 7:28 pm  

Asante kwa ku-share picha!

Simon Kitururu 12:31 pm  

@Da Chemi:Asante kwa kunitembelea!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP