Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

LABDA hutaki kuona MAJINI,MIZIMU, NDONDOCHA au hata KIDONDANDUGU!

>> Tuesday, April 15, 2008

SWALI:

  • Unataka kuona au KUTOSIKIA nini LEO?
Inawezekana tunalazimika kuona yatuzungukayo kwa sababu yametuzunguka.

Lakini...
....mwingine anaweza akawa na uhakika kuwa tunaona na kusikia mambo fulani kwa sababu tunawekea umuhimu mambo hayo au hata kuyatafuta kwa kutumia, jicho sikio au hata akili.

Inawezekana hata tukawa tunachagua jinsi ya kuona au kusikia jambo , ndio maana muziki mzuri kwangu , kwako makelele , na kitu kizuri kwangu, kwako kina sura mbaya na kinanuka kikwapa.

DUH!

Kutokana na utafiti mbalimbali, watu huona mpaka mizimu , majini au hata ndondocha kwa sababu tu walishaambiwa kuwa katika makaburi hayo, saa sita usiku , kuna jini na mizimu inacheza sindimba.

Hebu angalia hiki kideo uone jinsi kirahisi unavyoweza kutoona kitu mbele yako kama hutafuti kukiona....

Kisayansi pia wanadai kuwa sehemu iliyo na cabon monoxide nyingi, nguvu za elektro magneti kubwa, zinaweza kuingiliana na ufanyaji kazi wa ubongo, na kukukusababisha uanze kuhalusineti au kuona vitu ambavyo havipo.

Lakini....
.....kikubwa kikufanyacho uone au kusikia kile kitu, ukiondoa kuwa unataka kukiona au kusikia kutokana na yaliyojengeka akilini mwako tokea uzaliwe mpaka sekunde hii ya kukipigia chabo, ni kwa sababu jamaa washakuambia ukifika Makambako, usile nyama, kwa sababu zinaweza kuwa ni za kunguru.

Hebu cheki kideo hiki pia....


Unafikiri bila kusimuliwa kwenye kideo kuna nini, ungeona MBILIKIMO au WATOTO wanacheza MPIRA wa MIGUU?

Lakini....
...inawezekana unaona au kusikia pia vitu ambavyo vinaonekana na kusikika kutokana na kuwa vinaonekana na kusikika.

AU?

SIKU NJEMA!

7 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 2:29 pm  

yep.
yote umemaliza wewe bro sina la kusema..hicho kichwa sio urefu wa rasta tuu yaani una akili ndugu yangu.
lulu

Simon Kitururu 2:45 pm  

@Lulu: Asante sana kwa kunitembelea na kunifagilia Dada!

Anonymous 7:24 am  

Simon,kweli wewe mawazoni, duh kaka yangu unachimba sana kibook!!!!!asante sana,usichelewe kutulea habri zingine za kusisimua kama hizi!DUH

Aliko 10:51 am  

you see ...what I n I haffi deal with daily! guidance and protection against all evil

Simon Kitururu 6:02 am  

@Aliko:I &I haffi got to deal wit dat

Simon Kitururu 6:02 am  
This comment has been removed by the author.
Simon Kitururu 6:02 am  
This comment has been removed by the author.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP