Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

NAMKUMBUKA MPENZI KINUKA MKOJO!

>> Tuesday, April 22, 2008

Hakuna kitu kamili duniani!:-(

Inategemea na engo au kona umuangaliayo au umchunguliayo kipenzi , kama hutaki kugundua huwa anajamba kama wewe na kijambo kingine kinachembechembe.

DUH!

Kinuka mkojo hanuki mwili mzima.
Kuna maeneo kinuka mkojo ananukia kitunguu swaumu.

AU?

Kwa mpenzi Salome!
Nakuonyesha penzi kwa kukununulia mkorogo wakati sipendi wajichubuao.

Kwa mpenzi Zubeda!
Nakuonyesha penzi kwa kukununulia manukato, wakati napata ashki kwa mnuko wako wa kikwapa.

Kwa mpenzi Tanzania nchi ya amani mpaka inafungwa katika MPIRA wa MIGUU na RWANDA na BURUNDI katika kipindi nchi hizo ziko vitani.
Nakupenda kwa kama kawaida ya Watanzania, nazungumzia penzi la bila vitendo vya kuzuia wafisadi hata kama najua siri zao kwa sababu :SI TUNA AMANI?
Kwa mpenzi Tanzania, nchi yenye Mlima Kilimanjaro , lakini watalii watakao kuuona mlima Kilimanjaro bado wanajisikia vizuri wakija kutokea Kenya na wakishuka mlimani, wanarudi Kenya kwa sababu wanauhakika zaidi ndani ya Kenya.

Bado nakupenda kwa dhati ingawa najua sisi wengi Watanzania hatukiri kuwa Makaka na Madada zetu Wakenya, kunakitu wamefudhu au kwa sababu fulani fulani wanafanikiwa kitu ambacho tunaweza kujifunza kutoka kwao kiridhishao wageni a.k.a. watalii.

Usitishike, kila mtu kuna kitu anaweza kujifunza kutoka kwa mwingine!
Ujanja ni kukiri kuna kitu mwenzio anakijua zaidi yako.

AU?

Swali:

  • Kupenda ni nini?
  • Nikisema nakupenda unaridhika kwa sababu umesikia nimesema nakupenda?
  • Kwa mpendwa, je, nikuache kwa sababu wewe ni kinuka mkojo ingawa unanikojolesha?
Kwa mpenzi fulani!
Najua wengi hulalamika, kusema, na nahisi labda hata mimi hufanya hivyo ilikujisikia vizuri kwa sababu sitendi!:-(
Mawazoni , sisi Watanzania nahisi tumelewa kusikia kuwa tuna amani kiasi kwamba kinuka mkojo nahisi hatukinusi.
AU?

DUH!
Naacha wazo hili, nisije nikajifunga bure halafu ukapata cha kunidaka.
Msikilize tu Mmoja wa wanamziki wa AFRO BEAT niwapendao KUBWA kuliko, Lagbaja akikupa kitu ROCK ME GENTLE

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP