Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Nyumbani kwa Kitinda Mimba!

>> Thursday, May 10, 2007

Nilimuomba Mzee Maggid amtembelee Mama!
Asante kwa kufanya hivyo. Unajua haya maswala ya Ughaibuni nayaacha hivi karibuni. Mimi Kitinda mimba.... Narudi kwa mama hivi karibuni!
Kabla sijasema ngojea nimuache Richard Bona...

Sasa kabla sijaendelea , ngojea niache baadhi ya picha za chobisi Maggid
alizopiga.
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mtoni -Rock Garden
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Chobisi ya mama ileeeeeee!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Hapa ni ileile chobisi ya mama kwa karibu kidogo....
Duh!
Napamisi , lakini.....
Ngoja Manu Dibango anisaidie..

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mjengwa alimkuta Shangazi yangu pia.......
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Maggid Mjengwa eeh!Mama anakushukuru sana kwa kumtembelea.Ulichukua lakini tunda alilokua anakuchumia?Huyu ni mama yangu Mzazi. Nilimuaribu tumbo kwa sababu mimi ni Siziliani , kama unaelewa nacho sema.

Lakini....
namuachia Sizzla...


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Kabla hujafika chobisi ukitokea kwa mkuu wa Mkoa lazima uvuke mgomba huu...
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Hapa ni kutoka bustanini kwa mama ndio morogoro ionekanavyo.Umestukia Uwanja wa Jamuhuri pale chini?

Lakini unajua tena , pamoja nakupata faragha ya nyumbani , polisi wapo pia

Hebu Mpate KRS One


Mjengwa, nimefurahi sana!

Asante sana!

6 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 4:11 pm  

Bwana Yesu hakusema tuuvae msalaba bro.Kwani si wahalifu si ndo waliosulubiwa, Yesu walimsulubisha ingawa hakuwa miongoni mwao.Msalaba ni ishara ya ukombozi wa roho.Tuamini tu,yatosha.Maandiko hayajatuagiza kuuvaa shingoni.
Bro ile hoja ya Mkaguzi mkuu wa serikali uliahidi kuchangia.Nakukumbusha.Wale wezi wananitia hasira kweli. Kweli nchi inaliwa na wenye meno.

Simon Kitururu 6:12 pm  

Mzee Anony :usemayo kweli.Bwana Yesu hakuagiza kile kitu.Unajua tena, nawaza tu!Ile hoja sijaisahau!Nitaichangia.

NDABULI 2:01 pm  

Hiyo Morogoro imenivutia inavyonekana kijani, ni muda mrefu sijapita hapo, lakini na mimi ni karibuni nitakwenda huko.

Egidio Ndabagoye 3:37 pm  

Simon Raha ilioje kumuona Mama!.Kumbe wewe ni kitinda mimba?.Ngwala ulizopigwa ughaibuni zinatosha wahi fasta karithi uwanja huu.
Lakini sio uje upauze na kukimbilia darasalama...!!!

Anonymous 2:27 pm  

Simon,
lini "Mologolo" mtaleta wawekezaji wajenge bahari?

Simon Kitururu 1:25 am  

@Ndesanjo:-)
@Egdio:Raha kumuona mama.Dar esalaam kuna utamu wake lakini Morogoro ni jiji kasoro bahari tu.Na tushaanza mipango ya kujenga bahari ya mindu:-)
@Ndabuli: ni kweli ukijanni wake unavutia.Lakini wakati wa vumbi ni kasheshe pale

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP