Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

LEO, KAMA NI SIKU YA MWISHO!

>> Tuesday, September 19, 2006



Malaika mweupe , Shetani Mweusi au?





Binadamu, binadamu, binadamu! Kwa nini unajifanya kusahau kuwa hujui kama sekunde ijayo inaweza kuwa ya mwisho katika maisha yako?

Kama kuna mbinguni na hii ni sekunde ya mwisho, basi mimi nitakwenda motoni:-(
Je, naogopa? Jibu ni, naogopa kwa herufi kubwa.

WEWE JE?

Kisirisiri naamini baaada ya kufa haitakuwa kama watu waaminivyo sasa.
Itakuwaje ubongo wa kibinadamu ambao unapungufu zinazofanya tusielewe ya Mungu na ya shetani leo, uwe umepatia kuelewa au kutabiri maisha baada ya kifo?

Lakini lolote litokealo naamini wafanyao maovu hawatafaidi kama watendao mema.

Iweje ubongo huu ambao unafanya tuogope hata kujiuliza au kukosoa maswala ya vitabu vya dini ambavyo maandishi yake yalinukuliwa na binadamu mpungufu, utuwezeshe kuelewa kuwa ni ukweli safari yetu ya mwisho ni motoni au mbinguni?

Labda unajiuliza kama nina imani kuwa kuna Mungu!
Labda unaamini mie nimepotea!
Unaweza kuwa umepatia katika yote mawili.
Hivi malaika ni weupe?

Basi usisahau kuniombea!



Namsikiliza Aswad akiniimbia swala la upendo.


1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Simon Kitururu 4:05 pm  

Thanx Suebadoozie

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP