Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

KWA MPENZI HAUSIGELI!

>> Saturday, September 02, 2006

Hivi ni kweli umempindua binamu kuwa nyama ya hamu?Nasikia siku hizi unapendeza tokea siku ya kwanza. Nasikia hautumii chupi za kitenge tena. Lakini je ni ukweli baba mwenye nyumba huku lazimisha utoe uroda mara mama mwenye nyumba aendapo kazini?Mpenzi hausigeli!Bado nasikia unaongoza katika kuwafunza watoto wa kiume wa mwenye nyumba maswala ya ngono.Nasikitika hawakupi shahada ya ukufunzi katika hilo. Je ni kweli wewe ni mwoga wa kushitaki polisi mambo ambayo hutendewa hapo majumbani? Je ni kweli haki zako hazifuatiliwi hapo majumbani?Je ni kweli kazi yako haitambuliki kitaifa? Mpenzi Hausigeli!Kama wewe ni kweli nyama ya hamu kwanini haujulikani kwa hilo!Mpenzi Hausigeli, sikuhizi kuna ukimwi hivyo nakuomba uripoti polisi kama unadhalilishwa. Mpenzi hausigeli ,kumbuka usipate mimba kwa maana mara nyingi penzi hufa mara upatapo mimba!Lakini Mpenzi , kama yote nayosikia ni kweli , naamini bado binamu ndio nyama ya hamu halisi. Nahisi wewe unalazimishwa tu kukizi hamu za watu. Kwa leo naishia hapa mpenzi.Usiwasalimie wenye nyumba. Kwa maana unakumbuka penzi letu ni la siri.
Wako,
Paskari

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP