Wednesday, May 30, 2007

KUANDIKA UJINGA!KUONGEA UJINGA!KUFIKIRIA UJINGA!

Duh!Kumbe ni hawa werevu wanaotambua nani mjinga eeh?

Lakini si utani, ni kweli watu wengi wanaujuzi wa kumnyooshea kidole mjinga au wamdhaniaye kuwa mjinga.Na tatizo langu mimi ndio hilo hilo la kutoelewa jinsi gani watu wanapata uhakika sana kuwa wanaweza kutofautisha ujinga, mjinga na werevu, mwerevu!

Duh!
Usitishikeeee! Wewe na mimi si ni werevu!
AU?????????????


Lakini...........................!

  • Si werevu hawahawa walikuwa wanaamini kuwa dunia ikotambarare kama meza, miaka si mingi iliyopita wakibarikiwa na mpaka kanisa katoliki?
  • Si werevu hawahawa wanaamini kuwa binadamu walitaka kujenga mnara wa babeli kwenda mbinguni, hivyo Mwenyezi akakorofisha lugha iliwasije kufika mbinguni ndio kiyao na kipare kikatokea?
  • Si ndio werevu hawahawa waliotengeneza mabomu ya hatari ya nyukilia kwa malengo ya kulinda amani duniani?
  • Si ndio werevu hawahawa wanaacha watoto yatima mtaani kwa sababu bajeti ni ya kujaribu kufundisha nyani na chimpazii kusoma na kuelewa lugha za wanadamu?
  • Si waerevu wa jamii pia ndio walio kuwa wanashauri wanawake wakatwe kinanihii ?
  • Si ndio hawa wanao.......................ili ku..............................
  • Na kadhalika kadhaa wa kadhaa, si ndio hawa hawa wanafanya.......?
Duh!
Samahani sikutoa mfano unaokugusa wewe!


Lakini......................
Kweli inawezekana wewe na mimi ni werevu leo. Ila kesho kamjamaa kanaweza kakastukia kitu, halafu ukashindwa kuelewa jinsi gani unachekesha kwa gia ya uwerevu tulio uzoea.

Hivi...........
  • Walioamini kuwa mtu anaweza kujenga mnara kwenda mbinguni, hivi leo wakisikia kuna wanasayansi waruka na maspesi shato yao mpaka chobisi, wana darubini zinaona mpaka sehemusehemu bila kupastukia kwa Mwenyezi, watasemaje?
  • Wale waerevu walio kufa wakiamini dunia iko kama meza watasemaje?
  • Wale ambao waliamini ubongo uko moyoni je?
  • Na wale......................................
Duh!
Umestukia naandika ujinga eeh?

Swali:
Hivi ujinga ni nini?
Una uhakika?

Duh!
Basi wewe unabahati!
Siku njema!
Ngojea nikuachie na Frankie Lymon







Duh!
Basi Bwana, nimekuelewa kuwa nimekupeleka miaka ya mbali nakurudisha kwa Ludacris

Ee Bwana eeh!NAKUTANIA TU!

Si ushagundua utani unahitaji muwe zaidi ya mtu mmoja eeh?

Nafikiri ni kwa sababu kama nakutania basi lazima awepo atakaye chekeshwa na utani wangu.Nikikuita kwenye kona tukawa wawili tu halafu nikaanza kukutania , hainogi.
Labda mpaka nikutishie kuwa nitawashtua washkaji kuhusu hako kakitu nakokatumia kama kigezo cha kukutania.

Duh!
Inasemekana asilimia kubwa ya wachekeshaji ni watu wenye huzuni!

Lakini hili neno utani
...... na hiki kisentensi, nakutania
vinamambo yake!

Eti utani mara nyingi hufikia kwenye hiki kisentesi:Ee bwana eeh !Mimi sitaki utani, nitakubamiza wewe!Ohooo!

Au unakumbuka haka kasentensi:
Mimi sio mtani wako utalia sasa hivi!

Basi,
kautani kakifikia hapo, watu wengi hudai kuwa kameingiliwa na kaukweli ndani yake!

Swali:
Hivi utani ni uongo eeh?

Duh!
Uongo si dhambi lakini?

Lakini eti nasikia kuna uongo na uongo. kamoja ni haka kauongo keupe(white lie),haka eti sio kabaya sana.

Swali:
Hivi kale kauongo kengine kabaya kanaitwaje vile?

Sasa tukirudi kwenye utani.......

Ukifuatilia utani na haka kasentensi; nakutania tu! Utastukia nakutania tu, inatumika kupunguza makali ya utani ili usichukie.

Kwa hiyo jihadhari na kasentensi nakutania tu kwa sababu kanamaanisha mtaniaji kakuweka kwenye kona tayari.

Duh!
Kwahiyo utani una uhusiano na vichekesho lakini hauko mbali na huzuni au chuki.

Swali:
Ushawahi kuchekeshwa na kitu cha kuhuzunisha?

Usistuke sana!
Nadhani hakuna aliyeshuhudia ukicheka mtu akianguka!
Duh!
Lakini hivi ni kweli ulitaka kumcheka kilema siku moja katika dansi?
Duh!Basi bwana, hiyo siri yako!


Ngojea umsikie Chris Rock akichekesha hapa kuhusu mahusiano ya mwanamke na mwanaume!(kama hujakatiza miaka ya kumi na nane labda usimsikilize lakini)

Okei labda anatania......


Msikilize Eddie Murphy hapa akiongelea matatizo ya kusubiria nanihii....Duh!(kama ukochini ya miaka 18 labda usimsikilize)....


Duh!
Ngoje turudi kwenye NAKUTANIA TU.........!
Au kwenye Utani!

Swali:
Hivi utani ni nini?
Nakuacha na Eric Clapton

Monday, May 28, 2007

Funzo kutokana na Uingereza na Marekani walivyoiba Chagos!



Kabla sijasema.
Binadamu unaweza kumpenda panzi kuliko binadamu mwenzako?
Sitanii!Katika baadhi ya nchi naona imefikia kipindi ambacho kitu cha muhimu ni , mbwa wako, wanyama fulani , vipepeo na unaweza ukafungwa kwa kumpiga teke mbwa na kupewa onyo tu ukimpiga mwenzio.

Dondoo:
Hivi unajua USA walikuwa wanataka visiwa vya Aldabra na sababu kubwa waliyotoa kutokichukua kisiwa ilikuwa kuwa pale kuna Kobe wakubwa wanao ishihapo.Jibu walilopata likawa kuwafukuza watu Chagos .



Ukifuatilia mkasa uliowakumba watu wa Chagos, unaweza ukasahau jinsi gani sehemu nyingine kibao zinavyozidi kuibiwa.Kinachofurahisha ni kwamba watu wa Chagos wamefanikiwa kushinda kesi ya kurudishiwa nchi yao, ila tatizo linakuja kwetu wale ambao hatakustukia nchi imeibiwa hatujastukia.

Waingereza na Wamarekani walifanikiwa kuwafukuza wenyeji katika nchi yao kwa kisingizio cha vita baridi dhidi ya USSR. Sasa hivi ukifikiria sana utastukia kuwa hakuna haja ya kufukuza watu kwao, unawachukulia nchi kwa kumiliki bunge lao , miundo mbinu yao na hata akili zao.

Ukiniuliza mimi nitakuambia kuwa , hata kushinda kesi kwa Chagos sasa hivi kunatokana na kupungua kwa umuhimu wa visiwa hivyo kwa Wamarekani na Waingereza.

Nachojua ni kwamba , nchi zetu hasa za Afrika , hazitaachiwa kama maslahi wapatayo kwa kuzimiliki yanazidi nguvu zetu za kujikwamua.Tunaposhindwa kuweza kututumua misuli yetu kufanya nchi nyingine kushindwa kututawala kamwe hatutaachwa kutawaliwa.

Duh!
Samahani, nakumbuka tulipata uhuru miaka kadhaa iliyopita!


Swali:
Hivi wewe ukiwa ndio Mtawala, ukakiri kuwa umetoa uhuru sehemu sehemu ambayo ilikuwa inakufaidisha, unafikiri utakubali kuchangia pesa za kuendesha hiyo sehemu ya uliowaachia ili wajinome bila wewe kuwa na lako ulipatalo hapo?


Je,unafikiri kwanini watawala wa zamani wa nchi za Afrika bado ndio wachangiaji wakubwa wa bajeti za nchi walizosema wamezipa uhuru?
Au unafikiri wanatupenda sana?


Duh !
Siasa kidogo iko mawazoni leo!
Sijapata kamuda kakuandika sana siku kadhaa!

Baadhi ya sehemu niliyopotelea ilikuwa ni hii Photo Sharing and Video Hosting at PhotobucketWorld Village
Picha na Arto Salonen

Baadhi ya wadau wengine niliokuwa nao.......

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Aiyekoto mchana

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Aiyekooto Usiku

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
BassSoul

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Victor

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Riinah

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Aicha

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mandevu:-)

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Tompura

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ghanan Prinsi

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Abdul Senegal

Duh!
Na wengine wote!Tuko pamoja!
Pata Kool and the Gang basi!

Friday, May 25, 2007

Nani kasema Jua lina zama?

Si ni dunia inazunguka ?

Unajua kua ni mchezo wa dunia kuizunguka jua halafu.....
Tuna lala eti halafu eti tuna......
Halafu......
Tuna.......


AU?
Dondoo za janaaaa!
Jhikoman alifanya mambooo....
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Kabla Jhikoman hajaingia kazini
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mimi na Jhikoman

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Zimbabwen´vibe kabla Jhiko haja ingia

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ghanan Prinsi kabla Jhikoman hajaingia
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Don Cuba kutoka Cuba!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Tony Bass katika mixer
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Tompura , making sure hakiharibiki kitu
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Kutoka Nairobi aki sipu kitu fulani....

Photo Sharing and Video HMimi Nnikaribisha....osting at Photobucket

Mimi Nikimkaribisha......

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Jhikoman kazini
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Jhikoman
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Kazini

Ngojea basi nikupe minong'ono ya.....

Samahani niko kazini lakini ..................
Bebel Gilberto nilitaka aku nong'oneze. Ulipata mnong'onono?

Thursday, May 24, 2007

Leo Nimehubiriwa Sana!Lakini naogopa Kukufuru!

Nimepata bahati ya kuhubiriwa sana leo hii!
Hasa baada ya kukiri kuwa sina imani na dini ziendeshwazo katika mfumo.Mfumo na maanisha dini yenye kiongozi na mfuasi na .....
Nahisi umenipata!
Moja ya jambo nilikuwa na habarishwa, lilianzia kwenye jina langu Simon.Kwa sababu linaashiria kuwa ni Mkristo.Lakini hivi unajua Simon maana yake ni Jiwe tu?Hivyo nikilibadilisha kulifanya la kiswahili, mimi naitwa Jiwe.

Ngoja nikupe dondoo ya yaliyonikuta ili ufikirie mwenyewe. Mimi niko mawazoni tu hapa lakini, samahani kama utajisikia vibaya au uka........

Mimi sisemi kitu zaidi yakukupa dondoo zilizokuwepo mjadalani.

Kwanza kulikuwa na hivi vitu viwili vilivyosababisha baadhi ya watu waanze kusema Wakristo wamepoteza nguvu za kutetea dini yao .....

1.Jose Luis de Jesus



Nilishawahi kumuandika hapa


2.Halafu cheki kazi ya Javier Prato

3.Bila kusaha hoja hizi:
Nani zaidi?


Ukiniuliza mimi kuhusu maswala haya, nitakuambia kuwa sina la kusema!
Wewe tu na Mungu wako!

Au Tubu basi !
AU

Kama unamfuata Jose , yeye anasema huna dhambi!

Kama unafuata Voodoo au Bwiti au........sijui!



Duh!
Mimi ntakuambia ngojea tuendelee kumsikiliza
Santana hapa , akikupa kile kibao Soul Sacrifice kama alivyo kipiga Woodstock 1969

Haya tena , Kesho basi!

Wednesday, May 23, 2007

Je , Unaridhika na Ulivyozaliwa?


Je, unanungunika na kujisikia vibaya kwasababu

  • Matiti madogo?
  • Mweusi sana?
  • Mweupe sana?
  • Unamatege?
  • Unavigimbi?
  • Una.................
Lakini..........

Mbilikimo(primordial dwarfs)

Mapacha walounganika(Siamese twins)

Mapacha Walounganika(Siamese twins)


Usifikiri nakukataza kutoridhika!
  • Najua kama unanywele fupi , unataka ndefu.
  • Najua kwa sababu mweusi unajichubua ili uwe mweupe
  • Najua kuwa kwa sababu mfupi unaombea ungekuwa mrefu
  • Kwasababu una kifua kidogo unapiga chuma ili kiwe kikubwa
  • Najua kuwa.........................ili ................... iwe......................
  • Na kadhalika kadhaa....
  • Najua video nilizotundika hapo juu ,zinaweza kutoongea na wewe.
Lakini......................!
Nawaza tu hapa mawazoni !

Lakini isije kuwa mara nyingi kuwa tunanungunika na haturidhiki bila kuwa na sababu za muhimu. Nakutania, kwa sababbu najua maranyingi tunalalamika na kunung'unika bila kuwa na sababu za muhimu.

Usitishike!

Lakini.....................!


Siku njema!
Ngoja ASWAD (Nyeusi)walainishe siku kidogo....

Tuesday, May 22, 2007

Bwiti!


Nashindwa kuelewa kwanini kutoka Afrika ni Vudu inayosikika kuliko dini nyingine yeyote kutoka Afrika.
Hivi Tanzania kwanini dini zetu za asili hazitambuliki kwa majina? Si maanishi kuwa ni lazima mtu aziamini hizi dini. Lakini kwanini majina yake nayo imekuwa mwiko kuyajua?
Utasikia jinsi zinavyolinganishwa na kuoanishwa na uchawi, lakini husikii sana zikitamkwa kwa majina yake. Utasikia tu jinsi gani karibu kila lugha izungumzwayo kwa mfano Tanzania, ina jina la Mungu au Miungu. Kinachoshangaza ni kwamba hatuzungumzii dini zilizokuwa nyuma ya majina haya ya Mungu na Miungu.

Pia hata hii dini ya Bwiti yenye asili ya Gabon, ni mara chache ukisikia watu wakiiongelea.Ingawa ni miongoni mwa dini chache za Kiafrika ambazo zinakubalika katika nchi zilipo kama dini. Wengine dini ni zile tu tulizoletewa.
Hebu cheki Wadau wa Bwiti wakikuimbia nyimbo za dini...


Ila inasemekana mizizi (ibogaine) waitumiayo wakati wa ibada imegundulika kusaidia kutibu watu waliokumbwa na tegemezi la kutumia madawa ya kilevi. Kwa hiyo hata kama huamini wasiyo amini angalau kakitu kutoka katika imani yao kuna watu kana wasidia.Au sikiliza hiki kitu...


Duh!Lakini haya mambo ya dini mmh!Mi chichemi!
Siku njema!

Tangazo la Msiba!


Kwa niaba ya Ndugu Magonela Malima, tunasikitika kutangaza kifo cha baba yake Mzazi Mzee Malima kilichotokea ghafla huko Musoma Tanzanina hii leo.Kikao cha rambirambi na kutoa pole kitafanyika hapo kesho tarehe 23/05 ukumbi wa Chelsea,Helsinki, Finland saa moja usiku.Mfiwa anatarajia kwenda kuwahi mazishi hivi karibuni.Kwa wasioweza kufika wanaweza kuwasiliana na Magonela au Fidelis(Mtimkubwa) kwa taarifa zaidi.
Photo Sharing and Video Hosting at PhotobucketKwa wasiomjua.
Huyu pichani, ndio rafiki na ndugu yetu aliyefiwa Magonela.



Kwa wasio na namba au email yake na ya Fidelis unaweza kutuma ujumbe kwenye e-mail yangu:skitururu@gmail.com , na nitazi forward kwa wahusika.

Mungu Amlaze mahali pema peponi Mzee Malima!

Monday, May 21, 2007

Mheshimiwa!


Twakuita Mzee Mheshimiwa
Kwa sababu ya heshima na staha
Kama msalani
Twakutunzia heshima na staha
Ndo sababu ya Samahani....
Ingawa karne haina hekima wala mastaa
Kama maslahani...
Cha moto twa kiona katika kukutunzia heshima na staha
Mzee Mheshimiwa!
Shikamoo!

Duh!
Unajua kuna mtu atataka kujua namaanisha nini hapa!

Mpate tu Erykah Badu,Cee lo na Big Rube

Sunday, May 20, 2007

Milima Haikutani , lakini binadamu.........


Kuna kastarehe kakukutana na rafiki yako baada ya muda mrefu.Kuna kastarehe pia kakukutana sehemu ambayo kwa kawaida mtu usingewaza kuwa utakutana na mshikaji pale.
Duh! Haka kawimbo kako kichwani!Unakumbuka Archie Bells and the Drells?

Lakini kabla sijaendelea.....
Ngojea niwakumbushe baadhi ya washikaji wanaokumbuka zile safari za hizi sehemu.
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ukitembelea hapa ujue pochi yako ishapungua kiasi...

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Kuna mtu anapakumbuka hapa?

Lakini kabla.....
Ngoja Erukah Badu aseme.....




Haya tuendelee......

Basi nimepata bahati yakukutana na rafiki yangu JHIKOMAN . Baada ya miaka mingi kidogo ilikuwa ni furaha kukutana naye.Kwa wasiomjua, huyu ni mwanamuziki wa Reggae Tanzania ambaye usisite kusikiliza kazi zake.Hababaishi.
Ngoja ni weke baadhi ya picha ......


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Jhikoman

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Marti na Jhikoman


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Vilpu na Jhikoman


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Jhikoman





Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Jhikoman na mimi



Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Jhikoman na mimi

Sasaaa !Ngojea nianze! Jumapili njema !
Nakuacha na Big Youth

Friday, May 18, 2007

Ile Kura ya Ukatibu wa Jumuiya!Na hii Wiki mwisho!

Leo mimi mvivu kuandika.Lakini kumbuka mwaka jana kama leo niliandika...... ngojea niseme..............

Sasaaaa........!Nikumbuke hukuuu.Halafu gombea na weweee!Si Unajua hii jumuiya lazima iende mbeleeeeee!

Najua washikaji kibao niwajuao , wiki mwisho hii wanajaribu kupata nafasi ya kufikiria mambo wanayoamini kuwa ni muhimu.Halafu ukweli ni kwamba ni mambo muhimu.Lakini ,kumbuka ni wiki mwishooooo!Tuangaike tu, lakini tukumbuke yote ni muhimu.

AU!

Ngoja Marvin Gaye aseme....


Lakini.......!

Ngoja nimuache Mzee Martin , akiwa katika kushangilia timu yake ya Bacelona kwa ......













Eee Bwana eeh!Si utani!Hii kali!
AU?

Sasaaaaaaaaa........!



Katika hii wiki mwisho kumbukeni kuwa ingawa tunaendeleza kazi, tukopamoja ingawa najua hatutaonana .

Ngojea nimuachie mkuu wa kikao na wanzabanga hiki kitu cha R Kelly



Duh!

Nimestukia hicho kitu!Unajua kuwa .......
Sisemiiiii !Lakini tukopamoja
Basi ngojea Samba Mapangala asemeeeee.....



Lakini.....

Ijumaa njema!
Tutaongea baadaye ,
AU?

Wednesday, May 16, 2007

Katika Mwaka Umelala Miezi mingapi?


Usistuke!Najiuliza tu! Si unajua tena kale kamchezo ka nusu kufa tukafanyako?
Duh!Na maanisha kulalaaaaa!Samahani , nimekumbuka kuna watu mwiko kusema kufa!
Sasa ......
Si umestukia mwaka unavyotoweka wakati huu mradi wa kuishi hauonyeshi sana mazao yake?
Usistukeeeeeee!
Wote tulikuwa macho miezi kadhaa tu!Mingine tulikuwa tumelala kwa kisingizio usiku umeingia.
Halafu katika miezi tuliokuwa macho tuli:

  • Enda kwenye kitchen party
  • Hatukumisi kisimani kungojea kama Zubeda atatokea ,ili apatiwe ile kauli
  • Tuliugua kichwa na kuchoshwa na kua macho
  • Tukatumia muda kujifunza mambo yasiyotusaidia kitu
  • Tulichukua njia ndefu badala ya fupi kumkwepa Abdallah ,tuliye mkopa
  • Tukachukua kale kamda kengine , tumepoa tu kwa kukosa kujua tufanye nini
  • Tulifanya pia nanihiii,... na zile kadhalika kadhaaa.......
Duh!
Umestukia kama unasoma hapa, maana yake uko macho eeeh?

Siku njema!


Lakini ngoja nimuache anonymous anizinguaye Lagbaja

Kwa Mpendwa Halufani!

Salamu nyingi zikufikie hapo chobisi ulipo!

Mimi huku sijambo ingawa ndio hivyo tena unajua hali ya dunia hii tuishio, kuna mengi bado yananizingua na mengi tu nimeshindwa kufanya .Sijakata tamaa lakini!Ingawa siachi kujiuliza maswali kuhusu dunia hii yetu kuwa;

Hivi Ni Kweli Dunia inatakiwa Kukosa Kasoro?

  • Ukizungumza na wataalamu wa mazingira, watakwambia jinsi gani binadamu anaharibu mazingira

  • Ukizungumza na wenye misimamo mikali ya dini ,utaambiwa jinsi gani shetani anavyozidi kumharibu binadamu

  • Ukiongea na wataalamu wa afya, watakwambia jinsi gani afya ya binadamu inavyotishiwa na hali ya dunia hivi sasa.

  • Ukiongea na wakubwa, watakuambia jinsi gani wadogo wanavyozidi kuharibika kitabia sasa hivi.

  • Ukiongea na mamilionea , watakuambia jinsi gani thamani ya shilingi milioni ilivyoshuka sasa, lakini jinsi gani waweza kupata vitu vingi sasa hivi kuliko zamani .

  • Ukiongea na masikini , watakuambia jinsi gani umasikini unavyozidisha makali hivi sasa.Na jinsi gani masikini anavyoshindwa kujisitiri hata kwenye mambo madogo.
Sasa .....
Ukifuatilia historia iliyonukuliwa tokea enzi za mababu na kabla ya mababu, si utakuta kuwa;


  • Kama ni hali ya hewa na mazingira, yalibadilika.Kukapita kipindi kisemekanacho kuwa dunia nzima iliganda na ikayeyuka , na mabara kugawanyika bila binadamu kuwa na mchango wowote katika hilo.Ma dainasoo wakapotea duniani ,tukabakiwa na Kifaru, mbu, skopioni na kadhalika wachache.
  • Kidini , kwa jicho la dini zenye sifa duniani siku hizi, nikimaanisha ukristo, uislamu, nk;si ni ukweli kuwa idadi ya waumini wazifuatazo ni wengi zaidi siku hizi, ukilinganisha na wakati Waijipti wanaamini Farao ni Mungu?
  • Ukizungumzia afya ya binadamu katika kipindi hiki cha sayansi na uharibifu;si inasemekani binadamu anaishi miaka mingi kuliko zamani?Lakini hapa si nukuu miaka ya kwenye biblia ambayo hukawii kusikia mtu alipofikisha miaka mia nane........!
  • Kuhusu tabia; si nasikia karibu kila kizazi huona kifuatacho kimeharibika?Halafu na miziki ya kizazi kipya ndio hata usiseme!Makelele tu, ukimuuliza Babu yangu!
Lakini mpendwa Halufani ,
Dhumuni la barua hii nikutaka kukujulia hali tu! Mimi bado niko vilevile. Kuna wakati na furaha, wakati mwingine na hasira, wakati mwingine na huzuni,wakati mwingine nafanikiwa, wakati mwingine nashindwa na wakati mwingine nipo tu mawazoni ni, nikiamini;Au ;

  • Naamini kuwa haya ndio maisha na najitahidi kuyakabili niwezavyo kuyaboresha.Nafikiri na wewe unakubaliana nami kuwa maisha ukinuia yanaboresheka!
  • Naamini ni busara kuilinda dunia isitetereke, lakini pia naamini kuwa kuna mambo ya kidunia , yatakayobakia kuwa ya kidunia.Hata binadamu afanyeje dunia itaendelea kuwa na maana ya dunia ikiwa binadamu ataendelea kufikiria kua kuna sehemu bora zaidi mahala pengine ambapo baadhi ya watu wengine hupaita mbinguni.
  • Naamini kuwa masikini wa sasa hivi hawezi kukubali kubaki maskini kinamna walivyo leo wakati wanajua tajiri anaishije na anawaibiaje.Itafika siku atajichukulia chake hata kwa nguvu.Lakini , dunia itabaki kuwa na tajiri na maskini mpaka mwisho wake, ingawa umaskini utakuwa katika tafsiri nyingine si ya sasa ambayo kuna watu wamezidiwa na matoke, wakati wengine wanazidiwa na shughuli zakutupa maganda tu.
  • Naamini tabia ya binadamu itabakia kutafsirika katika makundi ya tabia mbaya na nzuri.Sina uhakika nani atajulikana kuwa anatabia mbaya au nzuri lakini!
Sasa nisikuchoshe sana na barua hii ndefu!Siunajua siku hizi tuna vimobiteli?

Nakutakia kila la heri katika mradi wako wa kuishi!

Ndugu yako katika kuwa hai,
Mawazo.

PS :Wasalimie wanaume na wanawake hapo mradini kwako!
Halafu si unamkumbuka Maiko Jakisoni

Tuesday, May 15, 2007

Hivi unauhakika na Tarehe ya Siku yako ya Kuzaliwa?

Ni kawaida kudhania kuwa kila mtu anajua tarehe ya kuzaliwa kwake.Lakini ukweli ni kwamba asilimia kubwa tu ya watu duniani hawajui siku yakuzaliwa kwao. Vijijini ambako bado watu wengi huzaliwa majumbani kwao kwa msaada wa mkunga, ni kawaida kusahau au kutojua umuhimu wakutunza kumbukumbu ya ni lini mtu kazaliwa.

Lakini KABLA SIJAENDELEA......

NICHOTAKA HASA KUSEMA NI KWAMBA MWAKA JANA TAREHE YA LEO NILIIFUNGUA BLOGU HII.INGAWA NI TAREHE 17/MAY NDIO NILIANZA KUPOSTI KWA WOTE DUNIANI WASHUHUDIE!

Lakini...........

Hivi tarehe ya kuzaliwa labda inaumuhimu. Kwa sababu za kimfumo wa dunia na hata kiafya wakati waganga wanajaribu kupata dozi yako ya PPF.


Sasaaaaaaaaaaaa.......!

Sherehe ya siku ya kuzaliwa unapoisherehekea unamaanisha nini?

Au unasherehekea kuwa umezaliwa?

Je , usingezaliwa kungekuwa na noma gani?


Lakini ukweli ni kwamba nimekutana na watu wengi tu ambao wamebunia tarehe ya kuzaliwa kwa sababu si za kufoji cheti, ila kutokana na ukweli hakuna ajuaye wamezaliwa tarehe gani.

Basi...
Kama hatujui kitu, angalau tarehe ya kuzaliwa tunaijua!
AU?

Duh!
Nisikuzingue!Endeleza tu eundelezacho!
Sasa ngoja nikuache na Yvyone Chaka Chaka

Siku njema!

Ladysmith Black Mambazo!

Kabla sijasema.....


Hawa jamaa wamenifurahisha sana Jana nilipopitia kwenye onyesho lao.Staili yao ni ya pekee iliyofanya watu tuliohudhuria kusuuzika na roho! Ngojea basi ni dondoshe baadhi ya picha nilizo zipiga kutokea nilipoketi.......
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket




Kabla sijakuacha na moja ya wimbo wao, nawaacha wadau walionisaidia kupiticha wiki mwisho iliyopita.....
Asanteni washkaji!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Clemoooo!

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mzee wa Zimbabwe aka Tvangirai

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mzee wa Kisumu
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mos G

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Nairobi Prince

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mzee wa Nairobi

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mzee wa Zenji

Na wengine wengi....Asanteni!


Haya basi nawaacha Ladysmith Black Mambazo na Paul Simon

Friday, May 11, 2007

KUHUSU ile LAWALAWA ichocheayo UKIMWI


Kabla sijasema......
Mcheki DANY ENGOBO


Binadamu tu wadhaifu!
Na vichocheo vya maswala ya ngono ndio vinazidi kujaa.Sababu kubwa ni sisi wenyewe binadamu kupenda au kushindwa kuepuka matamanio ya kimwili ambayo tumezaliwa nayo.Kuna kipindi matamanio ya kimwili yalikuwa ni kuhakikisha tunaendelea kuzaliana,lakini jinsi muda unavyokwenda, ngono imekuwa ni starehe zaidi ya uzazi.

Hata kwa wale waonekanao watu wa dini, mara nyingi hakuna tofauti sana. Nakumbuka enzi zangu wakati sikosi katika maswala ya dini. Nakumbuka wakati naimba kwaya kanisani, ilikuwa ni balaa! Huwezi kuamini jinsi watu wanavyoweza kusikiliza neno la Mungu wakati wakijiandaa kwenda kufanya ngono mara tu baada ya kutoka kanisani. Si unajua tena kuna watoto wa geti kali huruhusiwa kwenda kanisani tu.Hivyo muda huo huo inabidi utumiwe kufanyia shughuli ili arudi nyumbani bila kustukiwa alikuwa kapitia geto.

Tukiachana na kamfano hao juu...

  • Nilikua tu nataka tukumbushane hii ijumaa kuwa ni ukweli kwamba UKIMWI upo na unaua.
  • Na matamanio yapo na yataendelea kuwepo.
Najua ni jambo tulijualo!Lakini najua pia pamoja na kwamba wote tunajua , huwa tunatetereka mara nyingine!Hivyo hakuna haja ya kusahau kuwa huyu mdudu atatuondoa tukijisahau.

Haya tena!Tucheze kwa uangalifu!

Ijumaa njema!
Nakuacha na majaribu mengine ,yajayo kwa mtindo wa wimbo huu-KIUNO

Thursday, May 10, 2007

Yesu alitundikwa Msalabani!

Ndio maana watu wanavaa Msalaba shingoni .
Je , angenyongwa tungekua tuna vaa kitanzi?

Duh! Kumbe Mesaya hakusema tuvae msalaba lakini.......
Ee Bwana eeh !Nawaza tu!
Karibu tena Mawazoni!
Lakini wapate tena Soukous Stars!

Nyumbani kwa Kitinda Mimba!

Nilimuomba Mzee Maggid amtembelee Mama!
Asante kwa kufanya hivyo. Unajua haya maswala ya Ughaibuni nayaacha hivi karibuni. Mimi Kitinda mimba.... Narudi kwa mama hivi karibuni!
Kabla sijasema ngojea nimuache Richard Bona...

Sasa kabla sijaendelea , ngojea niache baadhi ya picha za chobisi Maggid
alizopiga.
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mtoni -Rock Garden
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Chobisi ya mama ileeeeeee!
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Hapa ni ileile chobisi ya mama kwa karibu kidogo....
Duh!
Napamisi , lakini.....
Ngoja Manu Dibango anisaidie..

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mjengwa alimkuta Shangazi yangu pia.......
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Maggid Mjengwa eeh!Mama anakushukuru sana kwa kumtembelea.Ulichukua lakini tunda alilokua anakuchumia?Huyu ni mama yangu Mzazi. Nilimuaribu tumbo kwa sababu mimi ni Siziliani , kama unaelewa nacho sema.

Lakini....
namuachia Sizzla...


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Kabla hujafika chobisi ukitokea kwa mkuu wa Mkoa lazima uvuke mgomba huu...
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Hapa ni kutoka bustanini kwa mama ndio morogoro ionekanavyo.Umestukia Uwanja wa Jamuhuri pale chini?

Lakini unajua tena , pamoja nakupata faragha ya nyumbani , polisi wapo pia

Hebu Mpate KRS One


Mjengwa, nimefurahi sana!

Asante sana!

Wednesday, May 09, 2007

Daraja!


Ni Kiungo.....
Kiunganishacho kulia na kushoto....
mwa kulia na mwako shoto

Ni Kivuko.....
Kikuvukishacho ukikimbilia hata moto....

Ni Maisha....
yalo shwari ,tulia kama bahari....
kwani waweza lia kabla kuona pwani..

Mwisho wa mwisho daraja ni daraja

Tuesday, May 08, 2007

Hivi Jirani Kala nini?


Kuna mambo mengine ni binafsi utake usitake.Lakini cha ajabu kuna mambo ya binafsi ya watu tunapenda sana kuyafuatilia. Na wengine tunapenda vile vile kuwashirisha watu katika mambo ya binafsi.Hilo lisisahaulike!

Cha kujiuliza ni , kwanini kuna habari muhimu ambazo haziwavutii watu kama habari za ajabuajabu za watu fulani?

Ukipitia katika tovuti mbalimbali , utakuta mpaka Afrika takwimu zinaonyesha watu walikuwa wanafuatilia sana habari ya Clinton na Monica Lewinsky kuliko habari za Clinton na maendeleo ya nchi zinazoendelea.
Hivi sasa Tanzania ni rahisi kustukia watu wakijadili Amina Chifupa
na matatizo yake ya ndoa kuliko ugonjwa wa Tetanasi , urudio kwa nguvu.

Lakini hili jambo linasababu zake !

Ukiniuliza mimi kwanini karibu dunia nzima umbeya una afya sana, naweza kusema sababu kubwa inatokana na mapungufu yetu binafsi.

  • Wengi hufarijika kustukia kuwa kumbe na wengine wanamatatizo kamasisi
  • Wengi hufarijika kujua kwa kujilinganisha na wengine tumewini au ndo tuko bado palepale.
  • Wengine tunafarijika tu kusikia kuwa na wale tufikiriao wako safi na wamefanikiwa kupita kiasi, nao wana matatizo yao kama sisi.
  • Wengine hutaka tu kujua jirani kala nini bila la msingi zaidi ya kutaka kujua anapataje kitambi.
  • Kwa kifupi ni mchezo wa saikolojia ,uzaliwao katika harakati za kutaka kujua sehemu yetu katika jamii na pia kutaka kujua yale tunayofichwa kujua, na hivyo kuyafanya yawe yanavutia.
Sasa ....
Utaniuliza kwanini nia ya kutaka kujua mambo fulani ambayo umbea hutusaidia majibu unanguvu kwa wengi kuliko kutaka kujua serikali ya Tanzania inatumiaje kodi.

Jibu:
sijui!

Lakini, nacho jua ni kwamba kufuatilia kodi zimeenda wapi ni jambo gumu. Ukikumbuka kuwa sisi binadamu ni wavivu kwa asilia. Ni rahisi kuchukua jambo rahisi kama vile tulivyo kuwa tunataka kufuatilia mwalimu darasani kavaa chupi ya rangi gani, au swala kama ; siku hizi kwa akina Kitururu bado wanakula mlenda tu?

Pili naamini maswala ya umbea kila mtu anaweza kujadili kwa ufasaha. Umbea kila mtu anaweza kwa ufasaha zaidi ingawa baadhi yetu kama vile katika kitu chochote tunaweza tukawa mabingwa zaidi, hasa kutokana na jinsi gani tulivyougawia umbea muda wetu wa wakati tuko macho.

Lakini pia tukumbuke kuwa ni wengi watafuata mambo rahisi, habari rahisi, lakini wapo wapatao kuridhishwa na maswala magumu. Ila wafuatao mambo magumu watakuwa wachache daima. Tufuatayo marahisi tutashinda kura kama mtu ataitisha uchaguzi.

Swali:
Unafikiri umbea na mambo ya umbea si muhimu katika jamii?

Ukiniuliza.......
Nnitasema kuwa umbea na mambo ya umbea ni muhimu katika jamii. Lakini umbea na mambo ya umbea yakitawala kunahatari kubwa kuwa asilimia kubwa ya watu itakuwa haijui kuchambua mambo ya maana.Asilimia ndogo ya wajuao na wenye kujua jinsi ya kutumia muda wao vizuri katika mambo muhimu na ya umbeya watakua katika nafasi nzuri ya kuwashinda wafuatiliao umbea tu.
Kitu ambacho kitasababisha wambea waendelee kutaka kujua vya siri vya wawahisio kutofautiananao katika jamii.

Lakini si ushakutana na apendaye mwenyewe kukuhadithia vya siri?

Hawa lazima watakuwepo.Nao wanakidhi kitu hicho hicho ; kwa kukuambia hujijua na kukujua, na kujipa auheni ya kuongelea jambo ambalo halitaki ujuzi.

Ushastukia unavyojisikia vibaya ukijadili jambo la maana halafu ukastukiwa hujui?Ushastukia hujali sana asilimia ya ujuzi wako wakati unakabiliana na mbwembwe za kusikiliza au kutoa umbea?

Lakini unakumbuka stori ya umbeya inaanzaje?
Hapa na maanisha kianzio kama vile utakapo kusimulia hadithi unaanza:Hadithi hadithi!Hadithi njoo utamu kolea............

Duh!.
Ngoja ni rudi kwenye Jirani kala Nini...................

Hivi jirani kala nini?

Duh!
Sijui!


Amina Chifupa na ndoa yake je?

Duh!
Sijui!

Kodi ya wananchi Tanzania inatumiwaje?

Duh!
Sijui!Ingawa kunakipindi nilidhani najua.

Haya tena!Siku njema!
Namuacha Tracy Chapman


Sunday, May 06, 2007

MARAFIKI !

Unahisi kuwa mimi na wewe ni marafiki tofauti sana na marafiki wakimbiao watu wakati wa shida?
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Sasa aaaaaaaa..........



Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Nilikudaka katika mwendo wa kutoka.........



Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
T.I hukunitenga...........:-)





Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
BADARA The Gambian prince!..........




Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Tanzania na Ghana





Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Kuku aka Liberian rebel!........





Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Aliko aka Altunez! Kazini!.......Kazi ilikuwa poa Mzee!





Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mkuu wa Kikao aka Raymond!





Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mzee Bakari na Bonanza wakipatiwa stori........




Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mimi na Jani Toivola





Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Kari na Mimi






Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
George na Mimi







Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
George na Mtimkubwa






Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Sari na Mimi






Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mimi , Tidjan na Amara







Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Albert, Mari, Johan na Martin




Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Edo, Mimi na Aliko



Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Mzee Wax,Mimi na T.I

Byamumgu naona nilikutenga jana:-)!

Jumapili Njema!
Nakuacha na Kaysha

Saturday, May 05, 2007

Kumeza Kohozi na kutema mate!


Samahani !

Najua tendo la siri hili!
Au unabisha?

Siunakumbuka unavyompiga kibaka aliyeiba kitumbua mara moja?
Na kumuacha bosi aibaye keki kila siku atanue!
AU?
Unakumbuka nikiongelea sehemu za siri unavyojisikia vibaya?
Duh! Umekumbuka nahisi!

Nakubaliana na wewe!
Kwa sababu kohozi ni siri halitakiwi kuongelewa?Ingawa linamezwa kisiri.
AU?
UMESTUKIA EEEH!
Nakuacha na BAABA MAAL


KIINI MACHO!


Unakumbuka tuonekanavyo nijitihada tu ya tutakavyo tuonekane?

Mara nyingi mimi na wewe pale kwenye genge la nyanya la Zubeda tulipo kutana......

Tulicheza tu kiini macho!
Nikajifanya sitaki kwenda kwa mama ntili e......
Kwasababu nilikuona unatoka hotelini.....
Halafu ukajifanya unanunua nyanya ....
Wakati ukweli nikwamba unampenda kikweli Zubeda , halafu ulikuwa umeenda gengeni kumpa kauli!
Duh!
Kabla sijaendelea...ngojea nimuache Mutabarukaamwage shairi...


Sasa tukiachana na swala la Zubeda......!
Ni ukweli unaweza ukawa unanichukia!
Halafu inawezekana ninakuzingua !
Lakini .....!
Wote tuna cheza kiini macho !

Si unajua diplomasia?
Lakini bomba!

Dondoo:
Usipoelewa namaanisha nini usijitahidi sana! Hii kitu naandika , haimuhusu mtu yeyote!Niko mawazoni tu!

Mpate tena Steel Pulse... Samahani niko kwenye reggae mood!


Friday, May 04, 2007

KUTAHIRI BEI NAFUU TANZANIA!KARIBUNI WATALII!

Kuhusu kichwa cha habari hapo natania tu!AU?

Kuna kitu kimoja kimenigusa leo , baada ya kukutana na habari kuwa waanzilishi wa Benji Jump wanadai haki ya kutambulika kuwa wao ni waanzilishi.Baada ya kusoma historia ya benji jump, na hii sehemu ya visiwa vya Pentecoste, Vanuatu kipindi fulani, ndio nilipata kujua jinsi gani watalii walirekodi maswala na jinsi kwa ubunifu wakaiga na kugeuza mila kuwa mchezo.Hili limenifanya nikakumbuka jinsi gani watu wanaweza wakaja kwenu wakaiga chenu halafu wakakifanyia kazi mpaka hawahitaji chenu tena!Huu mchezo wa benji ingawa watu hawa wapasifiki wameuanzisha , sasa hivi wanadai haki yakutambulika tu kuwa waliuanzisha. Ingawa kwao ilikuwa si mchezo , ilikuwa ni kuonyesha ushujaa kabla yakujiunga katika kundi la wakubwa, wakuja walipoustukia wakaukarabati wakaufanya wao.

Sasa.... Kwanini naongea hili?

Jeff Msangi aliongelea jinsi alivyotembelea Busch Gardens-Afrika , akiwa mitaa ya kusini mwa USA, akajikuta yuko nyumbani.Maana wana mbuga yenye wanyama kibao uwajuao wa Afrika Mashariki.Wana mpaka magari yenye namba za Tanzania yakuzungushayo Mbugani. Kwa ujumla wanatengeneza Serengeti yao ambayo wanaiendesha kiufasaha na kuhakikisha inalipa kuliko labda Serengeti itulipavyo wabongo.


Unaweza kuamini hili gari liko mbugani Marekani?

Picha kwa hisani ya Jeff Msangi








Sasa ......
Sisi Watanzania tunaweza kusema kuwa mtu hawezi kukopi Serengeti ikawa na utamu wa serengeti, lakini mimi naamini utamu wakitu unasaikolojia yake.Ndio maana watu wanasomea advertisement, marketing nk . Kisaikolojia mtu anaweza kukubadili mtazamo wako.

Swali:
Unakumbuka kunakipindi ilikuwa bomba kunywa kokakola ya kopo?Sasa unafikiri koka kola ya kopo inautamu tofauti na ya chupa?

Tukirudi katika kutahiri.............

Ndio , tunahitaji kuitangaza nchi yetu ilikuiongezea pesa za kuiendesha bila kutegemea mikopo.Na tunavivutio vingi ambavyo havijulikani bado.Lakini tusiwadharau ambao wanachukua wanyama wetu na kuanzisha mbuga zao.Ni ukweli ukichanganya na mabadiliko ya hali ya hewa(Global warming) , twaweza kujikuta ni sisi tumepungukiwa wanyama na nguvu ya kivutio halafu walioiga wameneemeka mapaka inabidi sisi ndio tutembelee kwao kuona vilivyokuwa vyetu. Halafu tutaanza unajua hawa simba walikuwa wetu!Halafu mpaka tunaanzisha vi-NGO vya kudai kutambulika kuwa sisi ndio tuliokuwa na serengeti halisi.

Okei , labda nimezidisha hapo!Inawezekana hili halitatutokea sisi. Lakini vizazi vyetu vijavyo je?

Swali:
Unafikiri hizi serengeti zianzishwazo ughaibuni zitakufa au zitakuwa kubwa zaidi karne ijayo?Unafikiri jinsi hali ya hewa inavyozidi kutotabirika haiathiri mbuga na vivutio vyetu vingine?


Basi tuendelee kuitangaza vyema nchi yetu na Afrika yetu!Ingawa si lazima kujitangaza kama tangazo langu hapo juu!Umelisahau nini?

Jikumbushe......
KUTAHIRI BEI NAFUU!KARIBUNI WATALII!

Duh!Munishi naye nasikia anataka kuwa raisi!Wewe je?
Endeleza ijumaa naye basi........Duh!Mimi sio mdini kabisaaaaa usinistukie kutokana na injili!:-)




Hivi waandishi wa habari wakimfuata BuDa na kuto mfuata mesaya kama Munishi atakavyo itakuaje?

Sidilia kwa Mtoto

Kuna ukweli kuwa kabla ya umri fulani sidilia haina kazi kwa mtoto!
Sababu kubwa ni kwamba hajaota matiti.


Inasemekana wakati wa utumwa Marekani , weupe walikuwa wanadai kujua kusoma na maswala ya elimu hayamfai mtu mweusi(Mtumwa).Moja ya sababu waliyokuwa wakiitumia ni kwamba ana ubongo usio mudu maswala ya shule.

Katika dunia ya sasa ambayo mtu mweusi anaweza kwenda shule au kubahatika kwenda shule, pia bado watu wengi wanadai ukitaka kumficha kitu mtu mweusi , andika hicho kitu kwenye kitabu.
Duh!
Inasemekana hata ukiandika mtandaoni , mtu mweusi yeye hasomi!
Kwa sababu inaaminika hana tabia ya kusoma. Matokeo yake hata ukimpa sidilia ya taaluma iwezayo kumsaidia ,kwake yeye ni yanini?Kwasababu hata matiti ya kuvalisha sidilia ya kujisomea hayajaota.

Unajua hilo si kweli kwa sababu mimi na wewe tunajisomea sana!
Unajua tena!Tukimaliza kupitia zile picha na video za ngono ,husoma zile habari fulani fulani nyingine za nanihiii!
AU?


Sasa.....!

Unajua kuwa asilimia kubwa ya Waafrika hawana nafasi ya kujisomea wala vitabu hivyo ambavyo wangejisomea labda.Hili linaeleweka! Ila wale ambao tunabahatika kujisomea tunasoma nini?Si siri, utakacho kukijua na cha muhimu kwako labda si cha muhimu kwangu.Lakini kama kinakusaidia, nakupa tano.Freshi hiyo!
Ndio , nakukubalia kuwa mtu huwezi kujua yote wala kujisomea yote!Lakini?

Ee bwana eeh!

  • Inadaiwa kuwa hata sidilia ya tekinolojia mpya tukiletewa leo , hatuna matiti ya kuvisha.
  • Tunaambiwa hata wasomi wetu wakiafrika wakiamua kurudi Afrika leo wote, hawana nyenzo za kutumia vipaji vyao. Wataota tu ukurutu katika ujuzi wao kutokana na kuwa na sidilia saizi mbovu.

Sasa.......!

Mimi naamini kuwa mambo mengi haya tuyasikiayo si ukweli mtupu! Ingawa sikatai kuna ka ukweli kinamana!
Lakini, mbona wenzetu wamefanikiwa kutatua mambo mengi tu kivyao bila utegemezi ?

Tukirudi kwenye sidilia,..............!
Swali:
Ushawahi kuona mtoto mdogo analilia sidilia akipewa inakuwaje?

Haya turekebishe basi hizo sidilia!Au ni ukweli matiti hayajaota?
Ijumaa njema!
Nakuacha na Procol Harum



Wednesday, May 02, 2007

Lugha ya pesa!

Lugha ya pesa nafikiri ndio ielewekayo zaidi ya Kiingereza , Kimandarini(Kichina), .......na hata kuliko lugha hii tukufu ya Kiswahili!

Lugha hii ya pesa imetusaidia sana hapa duniani kuendeleza rushwa na mambo mengine kibao.

Lakini unastukia kuwa ingawa tunaisifia pesa, muda wa muda ukifika watu hujichukulia vyao.Halafu pesa yako inakuwa haina thamani.
Inasemekana wakati wa meli ya Titanic ilipoanza kuzama, matajiri walikuwa wanataka kuhonga kupata sehemu za maboti ya dharura.Hakuna mtu aliyekubali pesa hata mmoja!

Swali:
Lakini si niukweli hii pesa na mali hizi hatuzikwi nazo?

Inasemekana Zimbabwe sasa hivi ile lugha ya pesa inabidi uje na gunia kutokana na inflation.

Duh!
Kunajamaa aliimba kuwa pesa ni sabuni ya roho!
Najiuliza tu kuwa, tukishakufa si roho inautoka mwili? Sasa hii roho mbona inaiacha tu hapa kipengele(duniani) hii sabuni ya roho?

Hivi kuhusu hawa walionazo hizi pesa wanavyozidi kuongezewa, ni mpaka lini wasionazo wataendelea kukogesha roho kwa sabuni za mbunju?

Jumatano njema!

Raisi Nyerere na Mobutu Seseseko Kama Kurwa na Doto!



Unaweza kubisha kuwa hakuna cha kufananisha kati ya Raisi Julius Kambarage Nyerere na Mobutu Sese Seko Nkuku Ngbendu wa Za Banga.
Lakini ukijiuliza sana unaweza kustukia kuwa inawezekana ni aina tu ya nguvu na jinsi ya kujiridhisha, ndivyo vilivyokuwa tofauti, ndivyo vilivyosababisha tofauti ya machaguo yao ya nini muhimu.

Dondoo:
Unajua watu wengi hujiridhisha wenyewe kwa kutumia njia ya kuridhisha wengine?


Ni kawaida kabisa kumsifia Nyerere kuwa alikuwa mtu wa watu na kumkandia Mobutu katika hilo.Sababu kubwa ni jinsi Nyerere alivyojaribu kuwa karibu na wananchi wa kawaida na Mobutu alivyojaribu kuwa Mfalme na kuwa karibu na matajiri.Ukiwauliza famili za akina George Bush , wanaweza kukuambia Mobutu alikuwa poa sana!

Swali:
Hivi Nyerere alikuwa karibu na watu wa kawaida kama mimi na wewe?

Labda........................!

Ni kweli sera zake nyingi zilionyesha moyo wake wakutaka kumuendeleza mtu wa kawaida.
Lakini tusisahau kuwa mambo mengi pia yalikuwa ni majaribio yake mwenyewe ambayo utekelezaji wake na mantiki zake unaweza kuzihoji usipate jibu.Naamini yako mengi tumsifiayo kwakututendea ,alikuwa tu katika mudi yakufanya kimridhishacho binafsi , ambacho kiliwezekana kutimizwa kisaikolojia kwakutufikiria siye.

Sasa tukirudi katika kwanini inawezekana kiini cha Nyerere na Mobutu kuchagua chochoro tofauti za kufuata kinaweza kabisa kuwa kimoja..............................................

  • Mobutu mpaka kuitwa dikteta ilitokana na kupenda kutawala na kuwa na nguvu kwa wengine kwa kutumia kile akiwezacho binafsi.
  • Nyerere mpaka kuitwa Mwalimu na baba wa Taifa , naamini ni kwasababu pamoja na kupenda kutawala, aliweza kutawala na kuwa na nguvu kwa watu tokea kuzaliwa kwake.Alizaliwa kwenye uchifu, aliweza kwenda shule katika kipindi ambacho Tanzania haikuwa na wasomi wakutosha. Baada ya kutawala Taifa nzima likamwita Baba wa Taifa , mwalimu, nk .hivyo alikuwa na nguvu kwa watawaliwa na watawala hata asingekuwa na ofisi.Hivyo kufupisha stori, Nyerere alitawala kutokana na kilichomjiakatika uwezo wake binafsi.

Hivyo inawezekana kabisa kuwa Nyerere hakua na haja ya kujisumbua kuwa dikteta wakati haki yake ya kutawala na nguvu yake kwenye jamii ilikuwa kubwa hata bila ya kujitangaza kuwa Mfalme wa Tanzania.Kisaikolojia kahamu ka ufalme kwake kalishatimia

Mobutu yeye hata Uraisi alipora!Lakini inawezekana kilichokuwa kina msukuma ni kilekile kilicho msukuma Nyerere.Ila yeye hakuwa na nguvu za kama Nyerere za kujifariji hamu yake ya kuongoza na kuwa na nguvu katika jamii yake bila kutumia nguvu za pesa na jeshi lililomsaidia kuchukua Uraisi kwa kupora.Pesa kwake ilikuwa muhimu ili awazidi wengine ili wamuonee gele na kumuogopa kinguvu.

Swali:
Hivi unafikiri Nyerere alikuwa maskini?

Katika kale kahamu kakujifajiri kwa yale tuliyonayo kwenye jamii hasa yanayo tengeneza sura tonekanayo kwenye jamii , kila mtu anastaili yake.

Kama hapa duniani wote tungezaliwa bila macho nafikiri kunawengi wasingeyajali mengi wayajalio sasa hivi.

Swali:
Ushastukia ukisafiri kwenda sehemu watu wasipokujua tabia yako inageuka kidogo?

Wengine tuletutabiatwetu tubaya ndio tunatuachia bila kujali, tukiwa maeneo wasiyotujua.
Si unajua tena ile tabia ya kwani nani ananijua?
Halafu nasikia wengine huko vijijini Tanzania tunapata sana marafiki wa jinsia ya tofauti kutokana na kamba tuwafungazo kutokana na ukweli hawatujui.Nasikia hako katabia kamepeleka sana UKIMWI vijijini.

Duh............!

Tukirudii katika kujulikana kwa Kurwa Nyerere na Doto Mobutu....

  • Nyerere, wote tulikua tunamjua.Na moja ya sifa zake ni kwamba mtu watu, anaakili sana, anajua karibu kila kitu.Halafu usisahau alikuwa na jeshi la masususu , ambao kuna kipindi ukiwa na Colgeti nyumbani wageni wakija inabidi muifiche kuogopa labda utaonekana mbadhirifu wa mali ya umma. Nguvu hii na kisaikolojia alikuwa kajitosheleza.Hivyo wengi hata kumbishia walikuwa wnashindwa hata walipoona anakosea. Duh!Aka kasifa kake kamekaa kidikteta kidogo lakini!

Tukienda kwa Mobutu hata mengi ya kusema hakuna. Ukimuondolea pesa ambazo alikuwa anajichukulia serikalini, na mavazi yake fulani ya ghali ya kimagharibi na ya kiafrika ya kifalme, alikuwa hana mengi ya kukutisha.Hivyo yeye kufikia kastarehe ka Nyerere ilibidi ang'ang'anie nguvu na ajaribu kwa nguvu sana kuhakikisha kuwa unamuona yeye zaidi kuliko wewe....

Lakini kuhusu kurwa na doto hawa(Namaanisha Nyerere na Mobutu) , unaweza kunibishia........!

Lakini nachojua sisi wote pamoja na kutaka kukatishwa tamaa na mengi , bado tunahangaikia U-Utopia!
Na katika hili la kuangalia jamii tuishizo mara kibao watu tofauti huliona swala moja kitofauti.
Si katai mchango wa Nyerere kwa Tanzania na mimi binafsi.

Lakini........

Na sikatai mchango wa Mobutu ambaye pia kama ujamaa wa Nyerere ulivyoonyesha mushkeli katika utekelezaji, na udikteta na ufahari wa Mobutu umetuonyesha mapungufu yake.

Haya basi tuendelee kuutafuta huo U-Utopia!
Lakini naombea hawa Maraisi wetu wa sasa wajaribu kujifunza makosa ya waliopita.Halafu wajifunze kujiridhisha na kupata faraja moyoni kwa kuturidhisha na kutupatia faraja moyoni.

AU SIO ; MUHESHIMIWA KIKWETE!:-)

Sasa tutafanyaje?