Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kifo na Biashara ya Majeneza!

>> Tuesday, July 03, 2007

Inasemekana kuwa kila janga kwa mmoja , hunufaisha wengine.
Ukitazama habari kuhusu Afrika , hukawiii kusikia jinsi vifo vinavyo tawala karibu vyombo vyote vya habari.

Kama hivi vyombo vya habari vinaaminika, basi haitashangaza jinsi biashara zihusianazo na vifo zinavyozidi kushamiri Afrika.

Hebu angalia wafanyabiashara wa majeneza wa kabila la Ga huko Ghana wanavyokutengenezea majeneza kutokana na hobi zako, ujuzi wako hata umaharufu wako.

Cheki mwenyewe baadhi ya majeneza hapa.
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Ukifa kama unapenda Coca cola utazikwa najeneza hili

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Baadhi tu ya majeneza kadhaa kutokana na ukumbukwavyo...

SAHARAN VIBE aliandika zaidi kuhusu hawa jamaa.

Lakini...
Inasemekana huko Malawi biashara ya majeneza ni ya upinzani sana. Na watengeza majeneza wamefikia kuwa na sifa ya kuwa wafanyabiashara wasiopenda mzaa kabisa. Ukitembelea duka la majeneza bila kuwa na nia ya kununua jeneza unaweza kushambuliwa hata kupigwa. Inasemekana wengi wa watengeneza majeneza huuzunika sana wakisikia kuwa makadirio ya watu kufa yanapungua.

Swali:
Ulikuwa unafikiri kila mtu anafurahi watu wasipo kufa kwa wingi?


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Duka la Majeneza Malawi

Ila nacho wasifu wafanyabiashara wa Malawi ni kwamba biashara ya majeneza inapopungua ,huwa wanaanza kuuza fanicha nyingine.Naamini huu ubunifu wa kubadili bidhaa kutokana na uwepo wa mahitaji , inafaa kuigwa na wafanya biashara wengi Afrika.

Tatizo linalojitokeza tu, ni jinsi inavyojidhihirisha kuwa kuanzia wafanyabiashara wa majeneza mpaka serikali zetu Afrika ni ngumu sana kubunia nini kinakuja mbeleni.Mara nyingi soko tuna liingia bila yakujua hata kujiuliza kuwa , hivi kama leo ndizi zina hitajika kwa wingi ndio ina maana hata na kesho zitahitajika hivyo?Matokeo yake hatukawii kuzidisha tusivyohitaji na kupungukiwa na tunavyovihitaji.

Duh!

Biashara ya kifo haiishii hapo katika mifano hiyo miwili.

  • Chakusikitisha ni ukweli kuwa kifo kipo na baadhi wataendelea kuneemeka wakati wengine wakifa
  • Chakusikitisha ni kwamba kutokana na tamaduni , mara nyingi mtu akifa anaweza kugharimu waishio zaidi hata ya jinsi alivyo kuwa hai
Inasemekana asilimia kubwa ya tamaduni za Afrika zina mjengea mtu mazingira ambayo moja ya utu wake na umaana wake katika jamii unajengeka na jinsi atakavyozikwa au kuzika nduguze, umaarufu au sifa za wahudhuriao mazishi , gharama ya mazishi iangaliayo ni nini chakula, vinywaji nk watu walihudumiwa katika mazishi nk.
  • Chakusikitisha ni vigumu kwa watu kujitoa katika mfumo ambao mara nyingine huumiza waliohai na bila ya uhakika kuwa aliyefariki kuwa anafaidika na gharama waliohai walizoingia kufanikisha mazishi ya aliyefariki.
Najua si rahisi kukwepa maadili na tamaduni zetu!

Lakini .....!

Nashindwa kujizuia kugundua kuwa kumbe matatizo huzaa matatuzi.Na binadamu ahangaikiaye kutatua matatizo inasemekana hufanikiwa. Katika hoja ya hii, kifo huzalisha jinsi ya kuingiza pesa.

Sasa kama kifo kinasaidia baadhi ya wafanya biashara kuishi.
Umasikini uliotawala asilimia kubwa ya Waafrika unamfaidisha nani?

Au ndio hawa viongozi wetu nini?

Swali:
Hivi mimi na wewe tunafaidika na umasikini?
Au ndio tuseme umasikini hauna kauhaueni?

Usistuke niko Mawazoni tu!
Baadaye!
Nakuacha na James Brown

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP