Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Rangi ya Moyo!

>> Saturday, July 14, 2007

Watu kibao wakibaguliwa wanalalamika.
Lakini nahisi kuna watu wanaongelea ubaguzi wakati hawajawahi kubaguliwa.

Nikiongelea uzoefu wangu. Baada ya kubaguliwa na baada ya kubagua.
UBAGUZI HAUNA MPANGO.
Bongo...

....tunamchezo wa kulalamika, halafu..mchezo wakudai sisi ni watu wa amani...halafu kuwa ......nk

Mwisho wa siku , ikiwa kadude fulani, midude fulani haitimiliki, saa nyingine kwasababu ambazo hazihitaji kumlaumu mtu, mara nyingi kwa sababu tunataka kumlaumu mtu, kwasababu hatujui nini tatizo....
BADO HATUTIMILIZI.
Duh!

AU?
Lakini sisemi kuwa kulalamika nishai.Lakini nauhakika kuwa SISI WEUSI NI WABAGUZI NISHAI Kama tu WABAGUZI WENGINE.Najua kuwa unaweza Au HATA HUWEZI KUAMINI.Sisi kabla ya rangi, tushaanza wewe kabila gani, halafu weupe weupe wanapewadili kabla yetu weusi weusi
AU?
Swali:
Unafikiri Ukabila umeisha?
Unafikiria nini ukimuona mhindi yuko bomba ndani ya Tanzania?
Kabla sijauliza......
mpate Bunny Wailer.....


Duh!
Kabla sijasema sana , ngoja niache....

Mpate Sting akupe SURA YA MOYO

Swali :
Hivi roho inarangi gani?
Hivi kwanini nikisema unaroho nyeusi hufikirii kuwa nataka unisimamie Harusi yangu?
Hivi kwenye Harusi wanasimamianaga vipi?

4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Aliko 10:25 am  

Ras "Kitu"
1.Naona hii back ground ya blue inafanya baadhi ya maandishi font colours kusindikana kusomeka. 2.Habari za ukatibu wa jumuiya ya bloggers tupeni sera zenu na nini hasa mnakusudia kufanya hivi karibuni....
3.Ukimwambia mtu ana roho nyeusi maanke sikumkashifu tuu,its plain clear that binaadamu wanahusisha rangi nyeusi
na maovu hii sio kwa wazungu peke yake bali ni kwa afrika pia misemo "kama usiku wa kiza" "usinitilie usiku"nk nakumbumka kibao kimoja ambacho kilipigwa marufuku na Basata Tanzania kwa kuuliza swali kwamba "sisi waafrika(weusi) tumekosa nini kwa mungu mbona hata malaika wote kwa mungu ni weupe"
Rangi nyeusi ambao kiukweli hafanani na rangi ya muafrika maana ninavyo jiona mimi ni wa dark brown kinamna hehehe:) inasymbolize evil,death,darkness nk yale yote opposite of good.
moyo nao ukiwa mweusi basi kuna ya mambo kama jealousy,envy,hate nk hivyo mtu hatopenda kukukaribisha kwenye tafrija ya ya ndoa ambayo inatafsiri living happly ever after.

Anonymous 8:42 pm  

"Hivi kwanini nikisema unaroho nyeusi hufikirii kuwa nataka unisimamie Harusi yangu?" ...fafanua tafadhali:)

serina

Anonymous 9:34 am  

Badilisha rangi hizo we!! nyekundu kwenye samawati.. duh!

Simon Kitururu 6:59 pm  

@Aliko na Serina.Rangi ni temporary hii.Wiki ijayo Blogu itakuwa bomba.
@Serina : Aliko naona kajibu swali lako hapo juu:-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP