Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

WaAfrika Wagombanapo kuhusu Mipaka ya Nchi Zao!

>> Friday, July 06, 2007

Inasikitisha kuwa sisi Waafrika bado tunagombana kuhusu mipaka ya nchi.

  • Hivi, si ni wakoloni walikaa pale Ujerumani wakagawana bara la Afrika?
  • Hivi si ni sisi Waafrika tunatakiwa kujua baada ya miaka yote hii , na busara zetu hizi, kuwa hawa jamaa waliotugawa kwa mipaka na tamaduni, na wanaoendelea kutugawa, kua wao wanaungana?Au zile EU na... bado hatuzielewi?

Samahani......

Ila Mimi kama Mtanzania, na marafiki wengi Wakenya kuliko Watanzania katika chobisi niliyopo.
Mimi kama Mtanzania na marafiki WaTanzania kama akina Ogola ambao wameishi Tanzania nakusoma Kenya kwasababu shule ya karibu ilikuwa Kenya.
Mimi kama .........
Duh!

Swali:
Hivi sisi kama Waafrika, mipaka ni kitu kitusumbuacho zaidi ya matatizo mengine mengi, ambayo ndio sura ya unyonge wa Muafrika mweusi?

Samahani, hebu msikilize huyu Mpiga Rege (Innocent Galinoma) Mtanzania ambaye baadhi ya watu wana msahau ingawa yuko katika anga tokea enzi zileeeeeeeeeeeee.....!




Sasaaa............
Mpaka leo .......
  • Tanzania na Malawi , wanagombania mpaka umepita wapi katika ziwa Nyasa(Malawi).
Hivi , Ziwa Nyasa limegawanyika katikati au lote liko Malawi?
  • Hivi , Wamasai na Waluo (Wajaluo)ni Wakenya na Watanzania ?Au kwasababu wako nchi zote , hawahitaji passport?
Hivi unajua kuwa Tanzania na Zambia ilikuwa katika vita ya Kidiplomasia hivi majuzi ,kwasababu inasemekana kuna Watanzania 22 wamejenga nyumba ndani ya mpaka wa Zambia?


Duh!
Samahani niko mawazoni tu!
Kabla sija kuacha, ngojea nikuache na picha zangu leo...
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket
Tulia basi na Sekouba Bambino

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Innocent Kasyate 10:06 am  

Bwana Kitururu, haya mambo ya mipaka ni akili mbovu tu za baadhi yetu waafrika.Kufikiri kwetu si kupana, tuna upeo mdogo miongoni mwetu ndio maana unaona matatizo kila kukicha.
Pia bado tunawaza kikoloni ingawa tunadai tuko huru, ndio maana hata mipaka tuliyoachiwa na wazungu tunaitilia maanani sana.
Tunahitaji fikra mpya.

Simon Kitururu 9:32 am  

@Inno:Siutani Mzee!Lakini kubadili mawazo imepruvu kuwa ngumu kweli. Lakini lazima maswala haya tujadili

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP