Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Bikira Wawili Usiku wa Ndoa.

>> Friday, March 28, 2008

Usiku huu wa ndoa.....,
wote tuko butu.

Tufurahi kuanza ndoa.

Maswali ni mengi .
Nashindwa kukohoa.


Matarajio ya umati....
Kuna kitu tutaondoa.


Sijui tuzime taa , kabla hatuja chojoa?

Kama kipofu...,
.....amwongozaye kipofu,
dunia msitu.

Nani atatuokoa?


Tunajua tuna kucha zihitajizo kunoa.

Nani wakumuuliza jinsi ya kunoa?

Na...
....tusipojiuliza nani twa mkomoa?

--------------------------------------
Najaribu kuongelea jinsi dunia inavyobadilika haraka sasa hivi, na ukweli kwamba hakuna ajuaye kwa uhakika jinsi ya kukabili mambo kibao, kisiasa(wengine wanasema siasa ya China bado ni mbaya wakati inakuza uchumi) na , kiuchumi(angalia Marekani kila mtu anavyo ongelea ni njia gani ya kujikwamua), kimaisha, kidini(wengine watakuambia Uislamu bomba na bado wengine watakuambia mambo yote ni Usayantoloji),nk.

Kila mtu anavutia kwake,kwa sababu na uwezo wake wa ubongo wa kibinadamu.

AU?

DUH!
Tulia na Aaron Neville akikuambia TELL IT LIKE IT IS.

Pilipili ni kali, je tuzidi kuinunua?
Baadaye Basi!

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

KKMie 5:02 am  

Hiyo bikira ni ngonjera/la au shairi....liminivutia kweli.

Si acha utoro....au at least uage basi kha!

Simon Kitururu 6:39 am  

@DI:Sijatoroka bado:-)

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP