Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

ZILE NYIMBO ZIIMBWAZO KATIKA LUGHA TUSIZOELEWA!Duh!

>> Sunday, March 30, 2008

Starehe za miziki, mara nyingi ni jinsi ikusuuzavyo roho.

Hebu mpate huyu dada akiimba wimbo kama asikiavyo....

(Kama unaujua wimbo wa Mariah Carey, unajua naongelea nini!:-))


Katika enzi zangu za kutembelea vilabu, gongo , mbege, konyagi, dodoma waini, na... nilistukia kuwa nyimbo za injili zinapigwa baa, chobisi na... hata kupita pale nyumbani kwa walokole au nyumbani kwa mchungaji.

Maswala ya ndombolo ya solo, sukusu, kibinda nkoi au kibinda nanihii......nk., yalinigundulisha kuwa, naweza kucheza miziki nisiyoelewa inasema nini ,na demu wa nyumba ya jirani aniringiaye, nikampata kama bonasi.

Lakini...
.......kisa cha kumpata hausigeli wa nyumba ya jirani kilikuwa na utata!
Katika kumpata Zubeda wa jirani, ilihitaji kuonyesha ujuzi wa kuondoka Ngwasuma dingiridingiri mpaka chini, nilikatika kisawasa, nilicheza sana, wengine waweza wakasema nilidansi sana, halafu mpaka yule wahusika wamuaminio kuwa ni muhimu ndani ya maeneo, akaja mezani kwangu, halafu akaonyesha kuzimia staili yangu .(Samahani kwa msio na .... au hata msio na uumee ,...au wale wasio na uke , njugu , peremende na....nahisi mnastori zenu za yule hausiboi, baba mkwe,mchaga wa kioski cha jirani, mpare fundi viatu au....yule aliyeng'ang'ania nanihiii na....)

DUH!
Lakini yule Mkongo, Mbongo, na.. aimbaye kwa lugha ya lingala,kikerewe na... au.... na.... atakuwa ni miongoni mwa watu ambao hata kabla sijafa nakumbuka kawimbo fulani ambako sikuelewa anasema nini. Lakini kalikuwa kawimbo kazuri.

Yule bingwa maeneo , si lazima aelewe msanii katika fani anasema nini ndani ya utundu au hata maisha.
KITU KIKUHUSUCHO , UTAELEWA KICHINA, kigagagigikoko kama embe dodo limekuchekea!

DUH!

Swali:

  • Ushawahi kuelewa mbwa anazungumza lugha gani wakati kakukenulia meno tayari kukuondolea ile siri uifichayo kuwa wewe muoga?

Hebu msikilize kidogo PAPA SAN akilia, kabla sijaendelea kunong'ona.


Nyimbo ni lugha!
Wewe, mimi na yeye, tunajaribu mara nyingine kusikiliza MUHUBIRI , SHEKHE, BABA, HAUSI GELI , MLONDA, na... anasema nini.

AU?

Tupo wengi tutamaindi ukikosea tundu la choo cha shimo na kunya pembeni.

AU?

SAMAHANI!

Nilitaka kusema tuko wengi tutachukia ukikosea sentensi au neno ndani ya lugha.

Nisemavyo si usikiavyo!
Naweza nikakuimbia mpaka juzi yake....
Naweza kukutongoza mpaka nikalia.....

Atanikililia nanihii!
Unajua tabasamu naweza nisipate?

USIKIACHO NDICHO ULICHOSIKIA.

AU?

Swali:
  • Hapa naandika maandishi, huhisi kama unasikia sauti yangu kuwa nasema nanihii kwa kutumia sauti?
  • AU?
Naacha!
Mpate Vanessa Paradis


Swali:

  • Hivi wewe unaongea lugha gani?
  • Unaijua hiyo lugha eeh?
DUH!

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP