Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

UKIMUOMBEA MTU KWA MWENYEZI MUNGU , UNAMUOMBEA NINI?

>> Sunday, March 30, 2008

Samahani ! Sijaenda Kanisani!
Samahani! Sijaenda msikitini!
Samahani!Sijaenda kwenye sinagogi wala pale... na pale....

DUH!

Najua lakini maswala ya ijumaa , jumapili , juma kuminatatu, asubuhi ,jioni na...kama mtu wa imani, inaweza kumaanisha kitu fulani.

AU?

Duh!

N
ashukuru wewe umeenda msikitini, kanisani , kule wa Hindu , na...... , halafu ukakumbuka kuniombea.

AU?

Nami sijaenda na sikuenda maeneo ya kumuomba MWENYEZI MUWEZESHA YOTE, lakini nimekuombea na nakuombea.
Nahisi katika vitabu fulani , ukisoma haraka haraka , unaweza kuamini mimi ni miongoni mwa wale watoto wapotevu.

Swali:

  • Katika vitabu fulani ,si ni ukweli mwana mpotevu anastukia akipata kibano ,baaada ya muda fulani uitwao baadaye na kutubu?
  • Lakini wewe ambaye hujapotea, UJAPOATE?
  • Ushatubu dhambi zako?
  • Hivi ni dini gani zile zikuwezeshazo kutubu ukizidisha nanihino?
  • Au hauna dhambi?

Nashukuru wewe umeenda maeneo ya kukutana au kukuruhusu kupiga magoti , kuinama na........................ katika kunyenyekea na kumtii Mwenyezi Mungu kiheshima, katika hali ya kusawazisha matatizo , dhambi zako na pia kutuombea sisi wenye dhambi.
Swali:
  • Unauhakika ukipiga magoti , kuinama , kurukaruka, MWENYEZI MUNGU hatastukia kuwa kisiri, unatamani nanihiii......ngono na asiye wako, kilaji , kudokoa mboga jikoni , au kuiba mahindi ya kuchoma shamba la jirani?

AU?

Swali:
  • Weye ambaye una uhakika wa ...Unaweza kunipiga jiwe kwa sababu nimepotea?
  • Una uhakika?
Staili ya kupotea, kwa jina jingine inaitwa UBINADAMU.
Naamini kabisa, bila ya nguvu za Mwenyezi Mungu, Allah, Yahweh , Murungu na...., unaweza kutamani kakitu kaliko katazwa kinamna.

Swali:
  • Ushawahi kutamani nanihino ambayo imekatazwa na baba?(Samahani!Nilimaanisha iliyokatazwa na DINI fulani uifuatayo iongeayo ukweli mtupu?)
Staili ya kupotea, ni ubinadamu.

Naacha!

Swali:
  • Kwanini unahisi kwa imani yako wewe au yule , una.. au anaweza kuamini nimepotea kwa sababu nimesema nimepotea?
  • Umepotea?
  • Kwanini imaniyako inakuponza ulazimike kuamini kuwa ni ukweli?

SAMAHANI ! NAJIULIZA TU!Usinitukane ukiwa chooni au pale sehemu ulipo.

AU?

Msikilize MUNISHI....



Duh!
Namsikiliza Marvin Gaye lakini vile vile!Msikilize basi.

AU?

BAADAYE BASI!

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP