Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Hivi kama Afrika sisi ni masikini haturuhusiwi kucheka?

>> Saturday, February 03, 2007


Mapambano yanaendelea!
Kabla sija sema......
Kassav


Nashangaa kwamba nimekutana na watu wanashangaa, itakuwaje Afrika ina matatizo bwelele lakini Waafrika bado wanatabasamu.Mwingine akaniambia kuwa Afrika iko nyuma kwasababu Waafrika tunatabasamu wakati tuna shida. Mimi naamini hii ni kurahisisha mambo. Furaha na kilio si siri ya kwenda mbele kimaendeleo.Ni siri iishiyo ndani ya binadamu. Naamini kuwa Waafrika, hata kwenye kucheka hatusahau kilio. Au?

Swali:
Hivi maendeleo ni nini?

Halafu.....
Mory Kante

WIKIENDI NJEMA!

1 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

MTANZANIA. 2:22 am  

Nashukuru kukuta umepitia pale nyumbani. Karibu tena. Kuhusu hii mada nina mambo mawili;
Mosi, Mungu ameweka kitu sahau ili kumfanya bin-adam asiwe mwenye huzuni muda wote.Hii inasaidia kuweza fanya mambo mengine. Waafrika bila kujali yanayotusibu katika nyanja mbalimbali tumejaliwa furaha."Wacha tucheke"
Pili, nilihudhuria tamasha la muziki wa kiafrika na hakika kundi la Mandika family toka Guinea Conakry lilitia fora baada ya kuigiza kibao cha YEKE2 hali iliyoamsha shamra2 ukumbi mzima. Ni kibao kizuri kusema kweli.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP