Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kitchen Party na....

>> Friday, February 23, 2007

Hivi hii party imepataje umaarufu namna hii?
Siipingi!Usinielewe vibaya.

Kabla sijasema sana:
Swali:
Hivi wanawake wa kibongo wanaridhishwa kimapenzi?

Duh!
Samahani akina dada , badala ya kimapenzi kwenye swali hapo juu, nilikuwa namaanisha ngono.
Wakati ukifikiria msikilize Sade akisema smooth operator....




Naamini binadamu anaruhusiwa kujitafutia sababu za kufurahi. Na nakiri sijui ni nini kinatokea huko.Lakini nasikia kunamafunzo kibao akinadada hupata. Au ndio aina mpya ya kumfunza Mwali kama ilivyokuwa katika unyago?

Huwa sipendi kuandika mambo katika kuegemea katika jambo nisilolijua sana. Ila nachojua kuwa jamii yetu inahitaji sana mafundisho yawezayo kuokoa mahusiano ya watu. Iwe katika ndoa au hata katika urafiki wa kimapenzi.Tatizo kubwa linatokana na misingi iliyobobea hata kwenye mila zetu. Mila zetu mara nyingi zimewafunza wanawake kuridhisha wanaume na pia kuwafunza kukaa kimya pale wasipo ridhishwa.Kuna makabila machache Tanzania ambayo yalikuwa na historia ya kuwafunza wanaume kuwaridhisha wanawake katika ngono.Ni mara chache utasikia staili kama katerero nk. ambazo hubobea kumridhisha mwanamke zikizungumziwa katika mila nyingi.

Kuna hoja zinajengeka kuwa moja ya sababu kubwa ya mwanamume na mwanamke kuwa na nguvu ya kuonja nje ni hii hali yakutoridhika na kitowewo cha nyumbani.Inasemekana kuwa ingawa mahindi ya kuchoma ya mtaani yananukia zaidi na ni matamu watu wengi wangeweza kuvumilia mpaka wafikapo nyumbani kama wanauhakika mahindi ya kuchoma yale ya nyumbani yapo na yanaridhisha kubwa kuliko.

Sasa eeh! Turidhishane basi!

Ila tatizo mbinu za kuridhishana mara nyingi hakuna pakujifunzia. Sasa kama huko kitchen party kunamasomo haya basi akina dada mnawini, ngawa na mashaka kuwa somo la siku moja na la mazingira niyasikiayo ya Kitchen party latosha

SASA eeh!

Nafikiri tunaongelea sana matatizo mengi yatutatizayo Watanzania. Lakini mara nyingi tunaruka hili la mahusiano.
Kumbuka mahusiano mazuri huzaa wazazi wazuri.Husaidia kupunguza magonjwa.Husaidia kupunguza watoto wa mitaani.Husaidia ukuaji wa watoto walio lelewa vizuri. Huzaa watoto wafanyao vizuri katika shughuli zao. Hupunguza matatizo chungumzima.

Sasa kwanini hatufundishani hizi mbinu za kuridhishana?

Mimi nafikiri tunahitaji kukuza uwazi wa maswala haya. Tumeua mila za unyago na jando. Sisemi tuzirudie. Nachotaka kusema nikwamba si yote yaliyokuwemo katika mila hizo yalikuwa yanaumiza jamii. Tuchukue mazuri tuunganishe na yanayohusiana na maisha tuishio sasa hivi. Tuyafundishe yawezayo kusaidia hata ikibidi somo hili liwe kwenye silabasi za shule.

Duh!
Katika kuzungumzia kuridhishana, nimekumbuka swala la matako.
Rafiki yangu mmoja Mzungu kaniambia anapenda matako makubwa kuyaangalia tu. Kasema kinachomshinda ni pale ajaribupo chuma mboga ambayo ndio madoido apendayo akiwa katika shughuli, hawa sangara wanasababisha ajisikie hafiki ufukweni. Sasa mimi nikamsamehe kwa kuwa alikuwa mkweli.Kwa hiyo msiwalaumu sana wapendao dagaa, huwezi kujua siri ni nini.

Duh!
Na hili jina Kitchen Party, mie lanizingua. Au ndoa inauhusiano zaidi na Kitchen kuliko mambo mengine? Kwanini haikuitwa sherehe ya jikoni lakini?

Sasa kwa wale ambao wanaume wao ndio wazima zaidi katika maswala ya Kitchen, wawe na Chumbani Party nini?

Najiuliza tu!
Lakini unajuatena leo ijumaa. Nakuacha na Lagbaja


Wikiendi njema!

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP