Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Ulisherehekea sikukuu ya kuzaliwa Mugabe?

>> Thursday, February 22, 2007


Mugabe alifikisha miaka 83 jana.Halafu inasemekana bado anampango wa kuendelea katika uongozi baada ya mwaka 2008. Hivi ni kweli anaamini hakuna mwingine awezaye kuongoza nchi?

Huyu kiongozi mpiganaji ukifuatilia maswala yake utakuja gundua kwa muda mrefu ilikuwa vigumu kumbana na kumlaumu. Ukichanganya siasa za kikabila za Washona kama yeye na Wandebele, na pia siasa za Afrika Kusini kwa ujumla, utakuta kuwa mambo hayakuwa rahisi sana kisiasa. Ukija kuwaingiza na wazungu wa Zimbabwe na Waingereza basi unaweza kuona jinsi gani hali ilivyokuwa ngumu kutatua baadhi ya mambo.Lakini sasa hivi naona alishapitiza na sidhani ni msaada tena kwa watu wake.

Mimi nafikiri wakati umefika wa hawa viongozi kuwa na mikakati ya kuondokea ofisini tokea mwanzo waingiapo katika ofisi. Naamini wengi wakishaingia wanakuwa hawajui jinsi ya kutoka. Wengine wanakuwa washaiba wanajua wakitoka wanaweza kufungwa. Wengine ndio hivyo tena , wanastukia kugongana na akina Tony Blair ndio inakuwa imetoka tena, hivyo wanang'ang'ania. Hii ni sawa tu na Wamarekani walivyoingia Iraq bila kuwa na mikakati ya jinsi ya kutoka.

Lakini wajifunze kutoka kwa akina Boris Yeltsin wa russia. Yeye alihakikisha anamweka kijana wake Vladimir Vladimirovich Putin ambaye hatamgusa akimaliza ulaji. Wajifunze kutoka katika uongozi wa CCM. Wao huhakikisha anayefuata hamgusi aliyepita hata kama madhambi yake yanajulikana.

Duh! Lakini inasikitisha.Huyu ni miongoni mwa viongozi ambao kama kwenda shule tu nakuipenda shule inasaidia, yeye katika viongozi wa Afrika si mvivu.Inasemekana hivi sasa bado kuna degree anaisomea.Hizi hapa chini ndio alizonazo kwakuziendea shule na kwa masafa, ukiachana na alizopewa tu na baadhi ya vyuo...
* BA (Educ) Fort Hare;
* BSc(Econ) Fort Hare;
* BSc (Econ) University of London, by distance learning;
* BEd University of London, by distance learning;
* LLB University of London, by distance learning;
* BAdm University of South Africa, by distance learning;
* LL.M University of London, by distance learning; and
* MSc (Econ) University of London, by distance learning.
Kinasikitisha pia kuwa mke wake wakwanza Sally Hayfron, aliyekuwa Mghana, anasahaulika siku hizi kama mwanamama aliyekuwa mpigania haki hata kufungwa jela kwa hilo.

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Unknown 2:57 am  

Simon naona hapa umempa Damija assignment ya kutuletea wasifu wa "mama Mugabe".

Simon Kitururu 11:51 am  

Zemarcopolo kumbe umestukia eeh!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP