Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Mkopo na ladha ya ukwaju!

>> Thursday, February 01, 2007

Katika kipindi nasoma Mazengo Secondary, siwezi kusahau jinsi ilivyokuwa kasheshe pale mkopo wa chapati kwa Mama Kabota ulipokuwa umepitiliza. Halafu unajua huna sababu nyingi zakuombea pesa nyumbani. Kisingizio cha kuugua ulishakitumia ukatumiwa pesa. Iliyobaki unaanza kubadilisha njia ya kukwepa maeneo yote ambayo unahisi utagongana na Mama kabota. Ukigongana naye bila kutarajia unanywea mpaka unajionea huruma mwenyewe.

Kwa ujumla kudaiwa ni jambo ambalo linazingua sana. Unaweza ukastukia umebunia njia za uchochoroni ambazo haujawai kuziwazia ili tu kukwepa kugongana na anaye kudai. Safari ya dakika tano inaweza kukuchukua saa nzima kutokana tu na kumkwepa anayekudai.

Sasa mimi inanishangaza jinsi Viongozi wetu wanavyokuwa huru kwenda kuomba mkopo mwingine. Wananishangaza waonekanavyo wenye furaha na uhuru wawapo pamoja na wanaodai. Halafu hukawi kukuta hata wakiwa likizoni wanaenda kupumzikia kule wanakodaiwa. Hivi hii ni hali ya mkopajia au hili jina mkopo linamaana tofauti kwa viongozi wetu?

Unakumbuka unavyonyong'onyea wakati unaenda kuomba mkopo?Je, huwa unapata kigugumizi eeh!

4 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 2:16 am  
This comment has been removed by a blog administrator.
MTANZANIA. 3:22 am  

Ya kudaiwa si vizuri. Waweza kuwa mtumwa hasa pale unaposhindwa. Mkuu karibu kwenye kiwanja changu.

Anonymous 8:10 pm  

Kusto,

Katika makala zako nyingi sana hii ni moja kati ya zile zilizoniacha hoi sana.

Niliongea na Dennis Londo nikamsimulia kuhusu hii akacheka sana.

Kazi nzuri, tuwasiliane,

Ni mimi nduguyo,

MtiMkubwa.

Simon Kitururu 8:49 pm  

@Mtanzania, asante kwa kunitembelea
@Mtimkubwa, asante Mzee!Duh lakini mkopo nishai!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP