Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Ukiniuliza kuhusu Tanzania vitani!

>> Tuesday, February 27, 2007

Ukimsoma H.G Wells katika kitabu chake cha The war of the worlds, unaweza kufikiria kuwa ni mpaka vibwengo kutoka sayari nyingine waingiapo duniani ndio vita kabambe inaweza kutokea. Ukifuatilia jinsi vita mbalimbali, sehemu mbalimbali duniani vilivyoweza kutokea hata zile sehemu watu walipoonekana kuwa wanaishi kwa amani,Tanzania chini ya uongozi mzuri tunaweza kuanza kupigana vita wenyewe kwa wenyewe. Ukifuatilia Bosnia miaka ya tisini, Ujerumani miaka ya thelathini, bila kuwasahau Watusi na Wahutu , hapo jirani, lolote laweza kutokea Tanzania.

Kinachohitajika ilikufanikisha vita Tanzania ni uongozi bora.
Au ulitaka niseme uongozi mbaya?
..lakini tuendelee na sababu zinazoweza kuondoa amani....
Kusahau ladha ya utamu wa amani .Uchumi kuendelea kudidimia wakati viongozi kuendelea kunawili.
Duh!
Dini nazo zikiendelea kutuaminisha maswala na kutusahaulisha kutumia akili.Akili nazo zikiendelea kukosa chakula kiiakikishiayo makali yasaidiayo kutatua matatizo yatukabiliayo, na hata pia kushindwa kututuliza katika dakika ambazo maamuzi lazima yatolewe.

Tanzania pamoja na yote ni jamii iliyogawanyika ingawa mara nyingi tunapenda kubisha. Ni rahisi sana kugundua kuwa:

  • Ukabila tunao
  • Udini tunao
  • Umasikini tunao
  • Uongozi bora ambao unaendelea kutufanya masikini tunao
  • Mfumo wa kisiasa ambao haujatengemaa tunao
  • Ujinga tunao
  • na nakadhalika tunayo.
Vita nyingi duniani zilisababishwa na zinasababishwa na maswala niliyoyataja hapo juu.

Lakini vilevile naamini tunamatumaini. Hakuna haja ya kukata tamaa.

AU UNASEMAJE?

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Unknown 12:33 am  

Simon nafurahishwa na jinsi unavyotafakari kuhusu Tanzania.dakika chache zilizopita nimeongea na jamaa yangu aliyeko uholanzi kwa kozi fupi.yeye na wenzake wanalaani watanzania wanaokaa nje.nilichomwambia ni kwamba amshukuru mungu kama kwake yeye kukaa Tanzania kumemuwezesha kutimiza ndoto zake.nadhani itabidi nimfowardie blog yako ili kumuhakikishia kuna watanzania ughaibuni wanaowaza Tanzania siku zote.

Simon Kitururu 2:52 pm  

Mzee Zemarcopolo, Mwenzio sina ujanja kwahili.Vigumu kusahau Nyumbani. Halafu mara nyingine ukiondoka sehemu unakuwa na uwezo wakuamngalia ulikotokea kwa jicho la pembeni.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP