Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Staili ya kujifunza kujisikia MJINGA!

>> Wednesday, November 26, 2008

Wenye akili unawatambua KIRAHISI kwa kuwa wanajua utakachokujua ambacho hujui au unadhani ulitumia akili sana kukijua.


Labda huhitaji hata kujaribu kujifunza ili kujifunza.
Labda siku ya pili tokea kufa, utajikuta tu unajua angalau UJUZI wa jinsi ya kufa siku moja kwa sababu UMEKUFA KWA SIKU MOJA na wengine bado wako hai chooni.


Labda staili ya kujifunza kujisikia MJINGA itafudhu zaidi ukidhania kuwa wengine hawana ujinga.

Swali:

  • Unajifunza nini?
  • Unauhakika kuwa ufikiriacho unajifunza si kile ambacho hujajifunza bado?
Labda unajifunza ''NINI'' wewe mwenye AKILI wakati sisi tunaongea UJINGA.
Na ,''NINI'' usiyojifunza ,labda ni ujinga.

Lakini......
......Kufanya ujinga kunahitaji akili kama hujui jinsi ya kufanikisha ujinga ambao kuna wenye akili wadhaniao si ujinga.

Inawezekana kabisa unachojifunza si kile ufikiriacho unajifunza.
Labda ujifunzacho tayari unakifanya na unachofikiria unajifunza bado hujaanza kujifunza.

TUJIFUNZE UJINGA kama tunataka kuwa na uhakika na KUTOKUWA WAJINGA.

Nakutakia kila la kheri katika kujifunza UJINGA!

NAACHA!
Hebu tukumbushwe kidogo kuangalia UJINGA....YOU ARE DIRTY

Au ngojea Patrick ST Eloi atulize kwa Champagn'

Wadau wa bongo nawakumbuka!
Wote mnajijua natumaini!

Bila kuwasahau baadhi mlioko ndani ya picha zangu hizi za mchanganyiko ndani ya bongo kama...

Photobucket


Photobucket

Photobucket




Photobucket

Photobucket



Photobucket



Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

MARKUS MPANGALA 6:15 pm  

Lakini ujinga nao una faida zake, si unaoja jinsi wanavyichangana mara dada kuchafua chupi na kaka eti kapenda? labda ujinga ni muhimu ili wajinga wajue umuhimu wa ujinga. Pengine wajinga na ujinga hawapatani lakini hawajui kama ni wao ni ndugu wa damu. Mkuu hivi hawa watu wajinga na mjinga bora ujinga? ndiyo inawezekana nikiandikacho ni ujinga lakini ngoja kwanza...... mjinga na wajinga afadhali nini au ujinga na mjinga kipi bora
NAACHA MKUU kwaherii

Simon Kitururu 2:08 am  

@Markus:Haukuwezi kuwa na kinyume cha ujinga kama hakuna ujinga.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP