Sunday, November 30, 2008

Wajanja hawako kwenye TAARIFA YA HABARI!

Kuna watu maarufu kuwa ni wajanja!
Lakini wajulikanao kuwa wajanja wanamjua mjanja hata kama si kwa jina MJANJA.

Mjanja hayuko kwenye taarifa za habari!
Mjanja hajulikani , ila walio MAKINI wanaweza kuhisi nani MJANJA.

Ajulikanaye kwa ujanja wa kutaka ajulikane mjanja, inawezekana kuna mjanja amtumiaye kuchezea watu mazingaombwe ili msimstukie nani mjanja.

Kama unataka kutatua swala, mtafute mjanja nyuma ya ajulikanaye MJANJA.
Mjanja yuko tu nyuma ya ajulikanaye na umati kuwa mjanja.

Ajulikanaye mjanja , usingejua ujanja wake bila kuwepo mjanja afanyaye MPAKA ufikirie unamjua nani mjanja, kwa sababu HUYO anasifika kwa UJANJA.

Mara kibao mjanja hajiiti mjanja na wala hajistukii au kujitambua kwa neno MJANJA ingawa yeye ndio MJANJA.

Swali:

  • Sikatika kampeni ya Obama ni Obama anajulikana kuwa ndio MJANJA?
  • SI wala rushwa na wezi waliokubuhu tuwatambuao kama WAJANJA ndio tunasikia wameshikwa?
  • Si mcheza sinema ni maarufu kuliko aliyeandika hadithi iigizwayo sinema?
Naacha basi!
Ngojea twende Haiti tukakutane na TABOU COMBO hapa akiwa na jamaa wa KASSAV katika ...
Pi Gro Pi Long


Au tuendelee tu na wa Haiti a.k.a TABOU COMBO katika "Tabou Mania"


Labda AONGELEAYE masikini ANA NAFUU kuliko MASIKINI!

Kama kuna MASIKINI aongeleaye matatizo yako, kuna uwezekano ni kweli ananafuu katika matatizo yafananayo na yako.

Inawezekana ni kweli matatizo yanaweza kuunganisha watu katika tatizo.

Labda urafiki wetu ni kwa sababu wote tuna MATATIZO ya kifafa halafu tunatembea kwa mwendo wa kudunda.

Lakini labda...
...Matatizo yakikukolea , hutakuwa na muda wakustukia matatizo ya mwingine.

Kama umeshaanza kugundua tatizo la wengine , basi kuna uwezekano tatizo lako limeanza kupungua kitu ambacho ndio tatizo!:-(

Tatizo ni.....
..... mara nyingi ni ufikirialo na jinsi ulifikirivyo ndio tatizo.

Umasikini ni tatizo, wakati kuna MAMA THERESA aliyekuwa anaamini kuwa UMASKINI ndio kitu kikusaidiacho kwenda mbinguni na si kitu cha busara kujaribu kukifuta.

Wengi tunajaribu kuondoa UMASKINI kwa sababu tunajua matatizo ya umaskini mpaka tunasahau kuwa si yote katika UMASKINI ambayo yanahitaji kupigwa vita.

Swali:

  • Ushawahi kuona maskini akiwa na furaha?
  • Ushawahi kusikia tajiri atakaye kujinyonga?
Aongeleaye tatizo lako la kunuka kikwapa wakati wewe ndiye mwenye chakula na yeye ana njaa, labda njaa haimuumi vizuri ndio maana ananusa bado kikwapa kuliko harufu ya mchicha.


Ndio....
..labda maskini hana pesa.

Lakini....
....Wewe tajiri mwenye pesa uko kamili?

Labda aongeleaye maskini anaupungufu wakutostukia umaskini wake mwenyewe hata kama ni umaskini wakudhania yeye ni TAJIRI.

Labda tunaweza kuchagua tu wapi kila mtu ni maskini kama tu wapi ni tajiri .
Isije tu ukawa unaongelea umaskini wangu ilikuepuka kuufikiria umaskini wako.


NAACHA!
SIKU NJEMA!

Ngojea Dan Dennett: aongelee Ants, terrorism, and the awesome power of meme


AU Ngojea basi tumsikilize LADY SAW aongelee tatizo la Mwanamke kuishi bila KIKOJOLEO cha kiume....(usimsikilize lakini kama kuna maneno ni matusi..)

Au tu SHABA RANKS aongelee apendavyo nanihii...(Usisikilize lakini kama unahisi inawezekana ni matusi)

Bwana au Mke wa MTU!

Huna mtu wewe kama tu labda wewe mwenyewe huna wewe.
Uhusiano wako na ulichonacho ni wakujijengea mwenyewe mawazoni , ndio maana mpaka wazazi wako ni wako mpaka uambiwe walikuokota ndio wanageuka kuwa ni wazazi wako tokea walivyo kuokota.


Unaweza kuvunja ndoa kwa sababu kuna mtu amekuchukulia mtu wako.
Unaweza pia kutafuta bikira ili ujihakikishie kuwa ni wewe tu mwenye kanyau ,ingawa wewe mwenyewe si bikira.

Labda...
...kuna umuhimu wa wewe kuwa na chako ingawa unaweza ukazidisha umuhimu kuliko ilivyo kuwa MUHIMU wakati wewe mwenyewe huli NYUMBANI na hutoi UVUNGU.

Swali:

  • Mtu akikuchukulia mtu wako unafikiri kachukua nini kama hakuondoka hata na maeneo yaliyowahi kufunikwa na nepi yake?
  • Unafikiri naongelea bwana au mke wa KUKU?
  • Unafikiri kwa nini kuna WATU hawana tatizo na wewe ingawa wanajua si bikira?
  • Wewe kama mke mwenza, huyo ni mme wako au wenu?


Jinsi mtu ajifikiriavyo akishasema hiki changu, ni UKICHAA kiiidogo.
Ukikutana na mtu mwenye chake, inamaana chako kwake labda si muhimu kama chake.

Kitu chake au chetu kinaweza kuachiwa kiote MAGUGU wakati chako kinanyolewa staili za MADENGE ili kivutie.

Tatizo ni....
...ujisikiavyo na ukaribu wako na kitu chako leo asubuhi si sawa na juzi.

Kuna wakati unajua kabisa kuwa hujisikii kwamba kuna umuhimu kitu chako kiwe chako.
Swali:
  • Si, gari ulipendalo unaweza ukaliuza baadaye?
  • Ndugu yako si ni ndugu yao ndugu zako?


Kitu chetu ni kizuri wakati mwingine kama kitu changu.

Tatizo...
...kitu chetu inamaana kuna wengine pia wanatumia hicho kidude.

Si tatizo lakini kama unakiita kitu chetu wakati unajua ni wewe pekee unatumia kama wewe ni mpenda kitu changu.


Uzuri wa kuamini una chako ni kama unaweza kuhalalisha kauli hiyo kwa muda utakao kuhalalisha ni chako.





Unaweza kubisha!
Hakuna kitu chako wakati wewe mwenyewe huna wewe mara nyingi kuliko unavyoweza kukiri.
Uwezo wako wa kuwa na chako wakati hata unashindwa kuzuia chupi isiingie mnato kwako , kitu usichopenda, inawezekana uko mawazoni tu.

Kitu chako ni aina ya kujidanganya ingawa inabidi ujidanganye saa nyingine ili uhalalishe jinsi gani tokea ujue siri kuna limtu lina kuonjea, basi kinjegere au kindizi hakinogi tena kama zamani.

Kunogewa na chako kama tu kunogewa na chake iko mawazoni tu kama ubwabwa wenyewe ni uleule.


Tunza chako kwa sababu unaamini una chako.
Kumbuka.....
.....Yote yako mawazoni tu ingawa utausingizia moyo kwa kudai yako MOYONI !

Inasemekana mpaka UJAMAA ulishindwa kutokana na watu kushindwa kutunza chetu .
Inasemekana Ubepari unafanya vizuri kwa sababu unahimiza kila mtu ana chake.

Kumbuka wakati unachako kuna wasionacho kabisa na unasema unachako kwa sababu unajua kuna wasionacho kabisa.

Kuwanacho ghali!
Kama huna labda UNANAFUU!
Swali:
  • Wazazi wako si ni wako tu ingawa ni wazazi wa kaka na dada zako pia?
HAPA Nawaza tu MKUU!

Ngojea Billy PAUL alete simulizi za yeye na MKE wa MTU... katika ME and MRS JONES.


AU Dan Gilbert ajaribu kuzungumzia furaha na huzuni katika : Why are we happy? Why aren't we happy?

Friday, November 28, 2008

Kila siku sio JUMANNE!:-(

Najua unaweza kuninunia leo ingawa ulinichekea jana!
Lakini aliyechacha jana anaweza akawa kachacha tu hata leo.:-(

NDIO...!
.....Leo ni Ijumaa kama unafuata kalenda alizobuni BULICHEKA!

Ijumaa njema na wikiendi njema!


Kwa MARA NYINGINE TENA ,Asanteni wadau wote ambao bado mnanitembelea hapa!

Nawaacha tena na LAGBAJA ambaye ni anonymous naye mzimia karibu kuliko wote katika AFRO BEAT... aendeleze tena FEYIN




Au tu KINGWENDU waanzishe katika MAPEPE


Asanteni WADAU wote kwa Ujumla hasa hawa mliokuwa nami juzi ya jana......

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket


Photobucket
Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

PEMBENI kidogo ya NANIHII!

Ukiwa pembeni kidogo , unaweza ukashuhudia vizuri!
Pembeni kidogo , labda huonji!:-(


Pembeni kidogo ya kishimo, si shimoni.

Na...
..... ni ujanja kujua ya ndani ya kishimo bila kudumbukia kishimoni.

Kipofu anaweza akakuandikia wimbo kuelezea uzuri wa ampendaye mpaka wewe unayeona unaweza kuwaza mara tatu na nusu; kajuaje MTOTO ana MASHAVU ya KUMIMINA na chunusi zinampendeza kama FENESI wakati haoni.

Kuelewa vizuri ya kwenye kishimo ,unachohitaji ni kujua kuna kishimo hata kama hujui kinaitwa kishimo.

Ukidumbukia shimoni, si kweli kuwa ,ujanja ni kutoka shimoni.

Shimo laweza kuwa ndio handaki ulikimbialo na usitalo kutoka.

Kama wote wanaamini kujitoa shimoni ndio ujanja, INAWEZEKANA ndio utapata faida zaidi kwa kubaki shimoni peke yako.

Swali:

  • Bado unajisikia kuanzisha kioski uuze ndala kwa sababu majirani wote wana kioski kiuzacho ndala?
Toka tu kishimoni kama wale , kama unafikiri faida ni kufanya kama wale.
Ukitaka kionekane vizuri au kirahisi, basi jaribu kisifanane na vile vya wengine.
Swali:
  • Unauhakikagani dunia ni ya duara wakati uko duniani?
Kumbuka...
...vitu vingine vikitolewa kishimoni Nyani hawiMJAMZITO!

DUH!
BAADAYE BASI, na usijali kama hunielewi!
NAWAZA tu hapa MKUU!

AU?


Twende kidogo Ethiopia kwa HELEN alete simulizi za YENE FIKER

Au ngoja turudi tu BONGO kwa KASSIM amlalamikie AWENA...

Thursday, November 27, 2008

NIKIKUONA tu hata kama sijachungulia , NAANZA kupata DHAMBI!

Kuna watu au hata maiti , wasio kufikirisha ya heri na baraka kama MASWALA ya MSIKITINI, KANISANI au afundishayo kungwi yakukwepeshavyo dhambi.

Labda ukiinama Msikitini au kupiga magoti kanisani unamkwaza kama tu akwazishwavyo kwa sauti yako nyororo yenye kibezi baada ya KUBANJA.

Binadamu ni kielelezo tu kama SANAMU!

Sanamu laweza kukumbusha Bikira MARIA kama tu likukumbushavyo Mwalimu Nyerere.
Muonekano wako unaamsha fikira za binadamu mwingine kinamna.

Lisichana ulipendalo inaweza ikawa ni kwa sababu linakukumbusha mama yako na LIVULANA ulichukialo linaweza likawa lina kukumbusha lijamaa ulilowahikulipenda mpaka juzi, lililofanikiwa kukusaidia kukuumiza roho kwa kukunyima NANIHII!

Swali:

  • Hivi ukiangalia picha za MAPIRAMIDI ya MISRI ,yanakukumbusha kuwa ni MAKABURI?
  • Wakati unajiangalia kwenye kioo unakumbuka unafanana na binadamu?

Lione, zuuri halafu kulitamani DHAMBI!:-(

Unaweza kuwakumbusha watu kibaka fulani mtaani ,na ukitokea ,kila mwanamtaa anaanza kuchunga pochi au chupi yake.

Kwa uwakumbushao malaika kwa muonekana na vitendo, labda kuna uwaingizao dhambi ya kujichukia kwa kuwafanya wajihisi hawafai ,kitu kiwasaidiacho kuwa karibu na malaika.

Utabakwa shauri zako!
  • Si muonekano wako unawatia watu hamu ya kidude ulichonacho kibakwacho?

Utapigwa shauri yako!
  • Si unawakumbusha watu mchawi fulani alogaye kuku?

Lakini....
...labda si kosa lako watutia dhambi kwa kuwa binadamu.

JAribu tu kuwa kielelezo chema kama binadamu.

Binadamu weye hata ufanyeje, kuna umtiaye dhambini tu.
LAbda tubu kama ni kosa lako nimechungulia na umenitia dhambi.:-(


TOPIKI IMENISHINDA!

Nawaachia Black Uhuru wazungumzie MSICHANA mwenye MACHO ya KUMEREMETA na TABASAMU la PLASTIKI katika SHINE EYE GAL/Plastic SMILE....

Au tu KRS ONE azungumzie RAFIKI katika A FRIEND

LABDA ukweli kuhusu WEWE na MIMI uko KWENYE SIRI!

Siri ya MCHOYO ajulikanaye kwa UGAWAJI, labda iko kwenye kasiriafichako, kuwa anagawa kwa shingo upande ingawa anatabasamu, na ingewezekana ,angejifaidi mwenyewe kwa jinsi ajipendavyo.

Siri yako na mimi yaweza kuwa ndio ukweli kuhusu wewe na mimi.

Siri zawezakuwa siri kwa mwenye siri, ndio maana anaaina fulani za siri.

Hatujui!
... labda DUME ZIMA linatamani wanaume wenziye ingawa linajulikana kwa kumpa mimba mama mdogo baada ya kufanikisha kwa MADAI ya bahati mbaya kumpa UJAUZITO hausigeli .

Hatujui!
....labda sista du anaUUME ingawa gauni na ushungi vya MPENDEZA na vyamtiahamu ya UKE ustadhi.

Hatujui!

......labda wanasiasa tuhisio tunajua waongo, ndio wakweli kuliko wahubirio dini WAKWELI kwa kujifanya wakweli kwa jambo wasilo na uhakika watuhakikishiavyo UHAKIKA.

HATUJUI labda!

  • SI ni SIRI?

NAACHA!

Ngojea BOB MARLEY avute BANGI kitu ambacho labda ni SIRI.....(usiangalie kama utakwazika)


Au twende kusikiliza shuhuda za MWANADADA aliyekuwa na tatizo la kutopatishwa Mimba na mumewe katika MCHEZO wa baba na mama, kapata MTOTO baada ya kuhubiriwa na DR Getrude Rwakatare kitu ambacho labda sio siri.....



Au twende tu SOUTH AFRIKA , Mahlathini & The Mahotella Queens wakiri ndio waanzilishi wa staili ya MBAQANGA , kitu ambacho si siri....

Wednesday, November 26, 2008

Staili ya kujifunza kujisikia MJINGA!

Wenye akili unawatambua KIRAHISI kwa kuwa wanajua utakachokujua ambacho hujui au unadhani ulitumia akili sana kukijua.


Labda huhitaji hata kujaribu kujifunza ili kujifunza.
Labda siku ya pili tokea kufa, utajikuta tu unajua angalau UJUZI wa jinsi ya kufa siku moja kwa sababu UMEKUFA KWA SIKU MOJA na wengine bado wako hai chooni.


Labda staili ya kujifunza kujisikia MJINGA itafudhu zaidi ukidhania kuwa wengine hawana ujinga.

Swali:

  • Unajifunza nini?
  • Unauhakika kuwa ufikiriacho unajifunza si kile ambacho hujajifunza bado?
Labda unajifunza ''NINI'' wewe mwenye AKILI wakati sisi tunaongea UJINGA.
Na ,''NINI'' usiyojifunza ,labda ni ujinga.

Lakini......
......Kufanya ujinga kunahitaji akili kama hujui jinsi ya kufanikisha ujinga ambao kuna wenye akili wadhaniao si ujinga.

Inawezekana kabisa unachojifunza si kile ufikiriacho unajifunza.
Labda ujifunzacho tayari unakifanya na unachofikiria unajifunza bado hujaanza kujifunza.

TUJIFUNZE UJINGA kama tunataka kuwa na uhakika na KUTOKUWA WAJINGA.

Nakutakia kila la kheri katika kujifunza UJINGA!

NAACHA!
Hebu tukumbushwe kidogo kuangalia UJINGA....YOU ARE DIRTY

Au ngojea Patrick ST Eloi atulize kwa Champagn'

Wadau wa bongo nawakumbuka!
Wote mnajijua natumaini!

Bila kuwasahau baadhi mlioko ndani ya picha zangu hizi za mchanganyiko ndani ya bongo kama...

Photobucket


Photobucket

Photobucket




Photobucket

Photobucket



Photobucket



Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Friday, November 21, 2008

Swala la MTOTO mzuri chupi CHAFU!:-(

Ya muhimu yako mangapi,
...kama huoni hatua ulizopiga ZI ngapi?

Kwa asiye hata na chupi,
.. ni hatua chafu chupi ,kama hana nepi.

Fahari ni ya mwenye chupi,
..ukisahau umuhimu wa tumizi la nepi.

Usafi wa hiyo nepi,
..ni mpaka uwe na nepi


Kama unahesabu ngapi,
..aliye na moja ni mwanzo wa kuwa na ngapi.

Mali iliyo makapi,
..ni mali ingawa kwako hailipi.

Mtoto mzuri kama pipi,
..nguo chupi ,maganda ya pipi.

Hata iwe nzuri vipi,
..mwisho hutupwa kama makapi.

Wamcheka chupi chafu,
..wasahau angalau ana chupi?
----------------------------------------------------------------------------------

Labda tuone zaidi kidogo ya tuonacho wakati tumekiona kinadoa.
Si angalau kipo?

Swali:

  • Kingekuwa hakipo je?
WIKIENDI NJEMA!

Tupate kidogo JAZZ kutoka kwa mwanadada nimzimiaye Esperanza Spalding



Au tu, mwanadada Tanya St. Val aje na - Zouk Chiré - Emmènes-moi

SIKILIZA mahubiri upate starehe ya KUJISIKIA unaDHAMBI!

Si mpaka sheikh ahubiri ndio ustukie una dhambi!

Dhambi ipo tu hata kama huikumbuki sasa hivi wakati ukobize ukifanya dhambi ya kufikiria wengine wanadhambi.

Akuhubiriaye utubu anaweza akawa katikati ya kujua dhambi afanyayo hata kwa kutamani kidogo akukatazayo katika mahubiri ya kuonja nanihii.

Kumbuka...
.... unafikiria ngono wakati unahubiri kukataza ngono.
.....unafikiria wizi wakati unakataza wizi na labda katikati ya kukataza wizi utastukia kuwa uliiba kwa kuibia kuchungulia maeneo yakuleteayo dhambi ya uasherati

Labda ...
... ni kweli kuwa wakati unakataza watu wasifanye dhambi ,huifikirii dhambi kinamna ya kufanya dhambi au uelewavyo wewe maandiko yanavyosema kuhusu jinsi ya kutenda dhambi.

Uelewavyo wewe maandiko NA KUHUBIRI kuwa si dhambi , inawezekana MUHUBIRI MWINGINE akawa na uhakika unatenda dhambi, kwa kudai Yesu ni Mwana wa MUNGU na ndio njia pekee, wakati kuna WAYAHUDI wanaomsubiri mpaka leo NA PIA wale wenye uhakika na ALLAH.

Tunaweza kubishana na KUINGIA dhambi kwa kukataa hata uhalali wa HARE KRISHNA katika topiki kama hizi ambazo zinacheza na imani kuliko akili ya uchambuzi ,hasa kwa wakereketwa wa dini hata kama ni ya KIPAGANI.

Naacha, lakini....
.....Inawezekana unashtushwa na stori za dhambi ya kuua.

Lakini labda....
.... hutajisikia kutubu kama wewe ukovitani, unaua kutetea dini ikufundishayo kuua ni dhambi.
AU?

Swali:

  • Hivi si bado Tanzania tunapiga wezi na kuua kwa nia ya kuwafunza adabu halafu wanakufa tukiwa bado tunashangilia ;'Piga MWIZI HUYO! '?
  • Unafikiri Rais Kikwete kashaua mwaka huu kama Rais Nyerere, au George Bush kwa kusaini muuaji anyongwe?

Labda....
...unauhakika MSHAHARA wa dhambi ni MAUTI kama vile wasio na dhambi wanaishi MILELE ya mpaka kesho vile!

Lakini....
...Baada ya kumsikiliza akuhubiriye halafu hujisikii unadhambi, labda badilisha MUHUBIRI upate starehe ya kujisikia unadhambi ili utubu.

La sivyo unaweza USITUBU wewe, OOOHOOH!

NAACHA MKUU topiki imenishinda!

DUH! Nilishawahi kuhubiriwa hapa kijijini kwa bibi na babu...
Photobucket
Pata busara za Richard St. John akupe siri afikiriazo ni za KUFANIKIWA katika- Secrets of success: Passion, persistence, pushy mothers


Au USISIKILIZE MAHUBIRI haya ,labda unaweza kupata DHAMBI.....(natanguliza samahani kama utafanya DHAMBI ya kusikiliza busara zilizochanganyika na UJINGA wakati nimekuonya)...


Basi Dr Dre anadai-Been There Done That
(Tahadhari! Anatumia lugha chafu kwa wengine ,na unaweza kujikuta umeelewa kuliko ukimsikiliza KOffi Olomide uchezaye muziki wake bila kumuelewa
.....

Thursday, November 20, 2008

BUSARA za BINADAMU kuendeleza UTAIFA baada ya KUFA kwa waliogundua MFUMO wa UTAIFA!

Binadamu wanajifanya WAJANJA halafu kuishi pekee bila kikundi hawawezi.

Kwa bahati mbaya...
...katika kundi la binadamu wajanja , KUNA MJANJA.

Lakini....
...yote ni kutapatapa kumfanyako binadamu aliyeko kwenye kibano kustukia staili ya kutatua tatizo, ikiwa ni pamoja na kuunda kikundi kukabili tatizo .

Katika kuhangaikia matatizo ya kijiji kunaaliyewaza kutatua kwa kuwa na NCHI.
Ili kuwa na NCHI, lazima kuzaliwe wazo na tafsiri ya nchi ni nini.

UBOVU mkubwa wa fikira za binadamu ni kusahau kuwa hakuna kidumucho au kuganda.

Kila kitu kinabadilika na labda ukifanikiwa kurudi tena duniani baada ya KUFA na kufariki kwa miaka kadhaa, hata Mlima Kilimajaro unaweza ukawa umebakia kichuguu halafu KIGOMA ni bahari ya Pakistani.

Unaweza kubisha!
Kila kitu kinabadilika kama siokupotea na kuzaliwa upya.
Lugha uzijuazo baada ya miaka mia kadha zitakuwa tofauti na uzijuavyo sasa.

Na....
....Binadamu na tafsiri za mambo hubadilika baada ya kujua mambo.

Swali:

  • Hivi si sikuhizi dunia haiko kama meza?

Sasaaa..
...Binadamu ni king'ang'anizi akizoea staili fulani kukubali jambo laweza kufanyika kwa staili nyingine kama ya ngwasuma.

Katika swala la mfumo mzima wa kuendesha jamii, kwa sababu tuna Mataifa basi tunayang'ang'ania kwa sababu ndio mfumo tuujuao.

Aliyebunia UTAIFA kafa!:-(
Aliyebunia UTAIFA angekuwa hai leo hii na kushuhudia jinsi watu wanavyopigana vita kwa sababu za UTAIFA angeweza kuwa na busara za kuwastua watu kuwa TAIFA umaana wake uko kwenye kurahisisha mahusiano ya watu kushughulikia matatuzi ya kuishi hapa duniani na sio kuongezea MATATIZO.

Waliobunia mfumo wa UTAIFA WAMEKUFA!:-(

Waliobunia, wangeshuhudia mpaka leo kuna nchi kama Tanzania ambayo inahangaikia swala la UTANGANYIKA au UZANZIBARI, labda wangeshangaa ya ULAYA ya NCHI kama UBELIGIJI isumbuliwayo na kama igawanyike ,WAFLEMISHi wajitawale tofauti na Wabeligiji Wafaransa.

Inawezekana ni kweli binadamu anahitaji kuunganishwa chini ya jina moja kama jina WASENGE ili kujitambua. Lakini labda hata chini ya jina WAKONGO bado inashindikana kujitambua kuwa ni Taifa moja kama kunaajisikiaye ni Mtutsi ndani ya KONGO.


Katika kutatua ya leo kama binadamu tunang'ang'ania tafsiri na mifumo tuijuayo leo ingawa mifumo yenyewe ndio hiyo mingine isababishayo Nchi kama ICELAND kuchacha kwa kufuata kanuni wakati NCHI kama TANZANIA kujisifia kwa kufuata HIZOHIZO kanuni.

Tatizo ni...
...waliogundua mfumo wamekufa na sisitumenogewa na mifumo hata kama mfumo sio lazima uwe aina moja katika kutatua matatizo ya jamiii iunganishwayo na neno TAIFA, kama sio tamaduni za walio ndani ya eneo liitwalo TAIFA.

Utaifa starehe.....
......hukawii kujikuta unapepea bendera kwa furaha kushangilia TAIFA!
Na usipoangalia utakosa raha kama huna kwenu kitu kisababishacho upende taifa lenu.


Swali:
  • Si kuna mataifa yalikuwa shamba la MTU au kampuni fulani tu?
  • Unakumbuka kunakipindi hakukua na neno AFRIKA wakati kulikuwa na watu AFRIKA?
Sipingi umuhimu wa taifa !
Naoungamkono jitihada za kukumbuka kwanini kulizaliwa mataifa na fikira zakuendeleza amani katika MATAIFA!

Kama Taifa ndio tatuzi , lilinde taifa!

NAACHA MKUU!
TAIFA lako libarikiwe mpaka litakapo badilika maana!

Ngojea tu twende kutembelea TAIFA la Zimbabwe kwa OLIVER MTUKUDZI alete za Pss Pss HALLO...

AU VYBZ KARTEL aongelee ya masikini katika EMERGENCY

Wednesday, November 19, 2008

BUSARA za BINADAMU mpenda NYANI, anichukiaye kwa MADAI nina sura kama NYANI!

Moja ya kitu Waafrika weusi wafananishwachonacho na WABAGUZI wa rangi, ni NYANI.

Unaweza kumshangaa Mzungu mbaguzi apendaye nyani kukuchukia kwa kudai unafanana na NYANI mpaka ukutane na Mwafrika akutukananaye; 'NGURUWE WE!' akiripo anavyopenda NYAMA ya nguruwe ingawa anamchukia MNYAMA aitwaye nguruwe.

Watu wanakutafutia sababu ya kukuchukia kwa kutumia akili za kibinadamu ziwawezeshazo KUKUCHUKIA kama OMBAOMBA na kuwawezesha KUJISIKIA vizuri kwa sababu WAMEMSAIDIA ombaomba na swawabu kiduchu wamepata kwa MUNGU au MIUNGU wao.



Swali:

  • Hivi bado ni binadamu pekee na sio tumbili au mende uliyemsikia akisema binadamu wanaakili sana na wamebarikiwa kuliko viumbe vyote ikiwemo kuku?


Binadamu labda anaakili ndio maana anajua kubagua wazuri na wabaya.
Binadamu labda hatumii akili ndio maana anabagua wabaya kutoka kwenye wazuri.

Labda ...
...binadamu anatumia akili kubagua ingawa ikibidi atasingizia aliyenaye ;ANA ROHO NZURI halafu kwa ZIRO DISTENSI ni mzuri kuliko aonekanavyo kwa mbali na wewe UMTAZAMAYE.
Moja ya Sababu inaweza kuwa NI kujaribu kuhalalisha tu SABABU zakuwaNAYE atembeaye kwa mwendo wa kuku, baada ya kukosa wa MWENDO wa bata ampendaye mwenye sura nzuri asiyemrudishia pendo kwa kisingizio ANA sura mbaya.

Unaweza kushangaa , lakini wabaguzi ni binadamu na ingawa unaweza kuwanyoshea kidole wale BIN ADAMU wengine, mbaguzi ni wewe na mimi pamoja na yule umshangaaye kwa KUBAGUA.

Inawezekana kabisa kuwa aonaye wabaguzi hajajistukia tu kuwa kuna awabaguao yeye mwenyewe kwa visingizio......
  • mweupe sana
  • yule Mhindi
  • Huyu muarabu
  • Yule chotara
  • yeye Mgogo
  • kale kana upele kidogo
  • hili Isilamu
  • Lile Pagani
  • lile mimacho kama balbu
  • huyu..... nakadhalika sita.

Sasaa....

BInadamu ni MTUNDU!
Anawezakupenda macho yako kama ya samaki aliyekabwa na kuchukia pua yako kama kidole gumba kwa kuangalia sura yako ileile.

Uchaguzi kuwa anakupenda na kukuchukia vinaweza kusababishwa na kukuhofia au kujihofia.
Inawezekana wewe ni tishio kuwa umekuja na njaa wakati UGALI wenyewe KIDOGO ndio maana anajikuta anakuchukia kwa kumtia wasiwasi atakufa na njaa.


Nachojaribu kusema ni...
....Tukumbuke tu kuwa makini katika kulaumu watubaguao wakati hatujali tuwabaguao.

Mlalamishi sana katika UBAGUZI ,mara nyingi ni yule aathirikaye kwa kupungukiwa kitu kwa kubaguliwa.

Unaweza usijali sana kama UBAGUZI unakuongezea kakitu hasa unakokataka.

Tukumbuke kuwa kuna leo na kesho lakini

Swali:
  • Hujawahi kumchukia mtu bila kujua sababu?

Basi naacha topiki!
SI tunakumbushana tu?

Ngojea TOPIKI ibadilike OBAMA na waheshimiwa kadhaa waongelee WALIVYOVUTA Bangi....

Au kwa msaada wa S. Msafiri K. wa Safirisafariyamuziki Mwalimu Nyerere aongee tena...


Asanteni tena Wadau WOTE hasa Mliokuwanami hivi karibuni ambao wengine mtajistukia katika picha hizi zangu za karibuni....
Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

PhotobucketASANTENI sana WOTE!

MVUMILIVU anasikia MAUMIVU hata KAMA ni ya utamu kuzidi ZAIDI kidogo KAUTAMU katamu!

Mvumilivu anavumilia tu kwa shingo upande.

Ingekuwa amri yake asingetaka kujishebedua aingie katika shughuli nzima ya kuvumilia hata kama ni kuvumilia jamaa litoke CHOONI.

Kama unavumilia , imezidi KIPIMO!
Kama unafurahia kuvumilia, hauna cha kuvumilia ,UNAISHI tu na ufikiriacho kutobadili.
Utamu ukizidi , labda sio utamu ,na kunawatakao kushauri uongezee maji.

AU..
......Utamu ukizidi, labda bado ni UTAMU , kwa sababu hata CHUNGU ni aina MOJAWAPO ya utamu.
Ukiuzoea utamu uliozidi , utataka kuongezea sukari kwenye utamu wa kawaida wa jana ili izidi utamu na uwe UTAMU UMEZIDI kama ulivyozoea leo.

Tatizo ni......
...... apendaye chai ya asali anaweza kukiri maji ya kunywa ni matamu pia.

Inawezekana kabisa kwamba unasikia maumivu kama ulivyojianda kusikia maumivu, la sivyo adhabu inaweza kuwa ni mazoezi ya KICHURACHURA kama sio ya KUKONYEZA kama adhabu upewayo umejiandaanayo kwa kuwa inaitwa MAZOEZI.

NA...
.....labda mvumilivu hodari ameshageuza maumivu kuwa ndio hali halisi ya maisha yenyewe.
.....Kwa kawaida unaanza kujiandaa kuvumilia kabla chamoto hujakiona , kama tu ujiandaavyo ujuapo utakanyaga moto kama unahisi unajua maumivu ya moto .

Swali:

  • Ushajiona unavyobadilika sura wakati unajiandaa kushika moto?


Maumivu ni changamoto zaidi mwanzoni , kuliko mwishoni ukijiandaa kufa ,kama sio kukata tamaa KUWA pamoja na kuwa na roho nzuri jamii inafikiri mchango wako ni wa kifala.


Vumilia!
Inasemekana Mvumilivu hula mbivu kama sio HUZOEA maumivu.

ILA....
...wakati unavumilia, kumbuka unaweza kuzoea maumivu kama sio kufa KWA MAUMIVU.

Na uvumilivu wa maumivu ni wa maana tu kama unaleta maana kwako.
Kama unavumilia ili jamii isifie , unaweza ukavumilia halafu USILE MBIVU.

NA....
......Pamoja na maumivu yako,jamii itaendelea tu bila wewe na uvumilivu wako.
,
Swali:
  • Unauhakika kuwa huwajui waliovumili na kutokula mbivu?
Kuna ambao hawatakuambia kuwa, labda pamoja na umuhimu wa mchango wako, utachangia zaidi ukifa na kuwaachia wengine maumivu ili wajifunze kuvumilia.
UVUMILIVU nishai ndio maana unaweza kujikuta unavumilia mpaka UONGOZI wa WAHESHIMIWA wajinga katika SIASA zetu za kutafuta AHUENI.

VUMILIA lakini...
.... uvumilivu wako wakutaka KUKWEPA kufanya dhambi ili uende MBINGUNI, labda ni busara INGAWA ,hujui hata kama TOGWA uzipendazo zitapatikana PARADISO kama ZIPATIKANAVYO kule JEHANAMU kwenye uasherati na mbilimbi za KONYAGI.


DUH!
ASANTE kwa kunivumilia unajua tena nawaza tu hapa!
NAACHA basi!

Hebu tujaribu kumvumilia Rais Nyerere akiongea KISWANGLISH na WASWAHILI wenzake katika kutufikishia hekima za KUKOPA....kama S. Msafiri K. wa Safirisafariyamuziki alivyomdaka.

AU ngojea tena tumvumilie MCHUNGAJI MUNISHI aonyeshe UVUMILIVU wake kwa KIKWETE....

Twende tu basi GHANA kumpata VEEDA atulize kwa Bribi Yaaye ME

Friday, November 14, 2008

Kama UMEKINAI kufanya kwa siri, FUMANIWA YAISHE ili YAANZE!

Kama bado ulikuwa hujajiandaa watu wengine wajue ufanyacho, unaweza kufumaniwa kwa kitu ambacho UNGEWEZA tu kuweka wazi mwenyewe WATU WAJUE kuwa kilema chako WEWE DUME ZIMA , ni matiti hayana CHUCHU.

Lakini....
....Labda kila siku unaanza hata kama unaanzia ulipoachia jana.
Labda unaendeleza kwa KUTOENDELEZA kwa sababu unasita KUKIRI umefikia sehemu ambayo ni faida kwako ukidakwa kuliko kuendelea na usichojua, kukihitaji, wala kukifaidi.

Unaweza kufanya mpaka ukafikia kisehemu ,CHINI JUU haikupeleki MAHALI na hunapakwenda.

Cha ajabu....
....... ni KWELI kuna KA ahueni utakokapata ukishafumaniwa, kwa sababu huhitaji kufanya siri tena, na kwa kufumaniwa unapakwenda ambako ni kuishi na UKWELI kuwa umedakwa.

Tatizo ni..
... ukishafumaniwa na sio siri tena , unaweza kusahau, lakini maana yake unaanza upya na mara hii unaanza kuishi HUKU kila mtu anajua kuwa wewe mwizi halafu ni kweli unabusha ,ndio maana unapenda kuvaa kanzu.

Starehe ya kufanya kwa siri ni tamu mpaka ifikiapo wakati umezoea sana KIDOGO kufanya kwa siri mpaka imechosha au haikusisimui tena kama jana, na unataka kubadili staili ya kufanya kwa siri.

Kufumaniwa kunaweza kukawa ndio suluhisho la tatizo lako la kuendeleza kautamu ulikoanza kukakinai kutokana na kufaidi kwa staili ileile , uchochoro uleule tu, wakati labda juu ya meza nako kungefaa siku nyingine, kama jamvini kusivyofaa kulia UBWABWA tu.


Binadamu kama binadamu ni rahisi kusahau, hata kama kusahau ni kwa KUSAHAU maumivu ya kufiwa na KUKU wako Mpenzi.

Njaa ikianza kuuma tena, kumbukumbu ya chakula kizuri ulichowahi kula msibani juzi, ni kumbukumbu za mbali sana tu na zikusaidiazo kuendeleza kukutaabisha tu. .

Lakini...
.. Ni kweli kumbukumbu zako hata kama sio nzuri sana UKIBAKWA, huwezi kusahau, KUMBUKUMBU zipo na ndizo zinaweza zikawa KICHOCHEO cha mwanzo wako wakujiadhari na WANADADA kwa sababu ni liMWANADADA lilikubaka.

Kumbukumbu zako za jinsi ulivyoaibishwa , hata kama unasema unazikumbuka leo kama vilevile ilivyokuwa wakati wa tukio, inawezekana kuna mawili masita zaidi ambayo yalitokea nyuma ya kisogo chako ambayo uliyaona na huyakumbuki , ambayo yanakusababisha mpaka leo uogope MIJUSI ingawa huelewi kwanini unaogopa mijusi kama uogopavyo mende tu.

Swali:

  • Kama umefikia ukingoni na unadhani hakuna ujanja, si FUMANIWA tu YAISHE?

UZURI wa kufumaniwa ni kwamba, hauna ujanja, bali UNALAZIMIKA kuanza UPYA, kitu ambacho ni kizuri kwako kwa sababu labda usingekuwa na msukumo wa kuanza upya.

Kuishi na siri , utamu wake ni jinsi unavyoweza kujistukia ulivyokuwa na akili , hasa kwa kujaribu kuhakikisha watu hawastukii siri yako kuwa wewe MCHAWI halafu mwanamke mzima hujatahiriwa wakati nia yako utahiriwe kidoooogo!

Ukifumaniwa nishai ,watu wanaweza wakastukia kuwa wewe BOMBA la MTU na ndio ufunguo wa kwenda MBINGUNI ya kwenye MDUNDIKO.

Kuishi na siri si lazima kuwe kutamu ,hasa kusababishavyo ushindwe KUZINI hadharani kisa wewe MPAGANI au kula KITI MOTO mbele za watu ,kwa sababu wewe MUISLAMU na nguruwe ni haramu ingawa ndio nyama yako kipenzi kama NANIHII au MSABATO tu.

Lakini..
.. Ukifumaniwa unaweza kupigwa, SHAURI YAKO!

DUH!
NAacha!
Wikiendi NJEMA!

Ngoja PATRICK Saint ELOI aseme MAGNIFIK

Au tu JACOB F. DESVARIEUX aseme GOREE

STAREHE ya KULIDANGANYA limtu ULIPENDALO!

UKIAMINI unachoDANGANYWA , UONGO ni UKWELI, ndio maana dini zote kwa waziaminio ni za KWELI.

UKWELI na UONGO vyote ni muhimu na vinategemeana katika kusaidiana KUISHI.
Ukweli unaweza kukutia huzuni hata wakati unanyemelea KIFURAHISHACHO.

Na....
...Mara nyingi akuulizaye ili kuhakikisha kama kitu fulani ni UONGO, ameshahisi UKWELI uko wapi.

....ni UHAKIKA wa jambo ndio umsumbuao atakaye UHAKIKA, wakati maisha yataendelea hata kama hakuna uhakika kuwa ni kweli au Uongo, kama tu tutakavyo kufa ikiwa ni UKWELI au UONGO.

Mara nyingi unanyemelea upande wa furaha ya starehe hata kwa kuhuzunisha umati, kama unafurahishwa na ni STAREHE wahuzunikavyo.

Linaweza kuwa na furaha HILO limtu ulijualo ukilidanganya kuliko kuliambia ukweli kuwa linanuka mkojo mkojo KWA MBAAALI lisipotumia MANUKATO.

Atakayekujua kama ni kweli UONGO, yuko katika MZANI, anataka tu uongezee uzito ahisiko ndio ukweli wa hali halisi ili ajisikie ahueni.

Ahueni atapata zaidi kama utamuhakikishia ndivyo alivyokuwa anahisi , kuwa chupi imeingia mnato.
Swali:

  • Unafikiri ni kwa nini unataka kujua kama ni ukweli au uongo?
  • Unauhakika sio bora kutokujua Utamu wa Ukweli wa hali halisi kuwa unachojaribu hakiwezekani?

DUH!


Lakini , labda.....
  • Lidanganye tu limependeza, litajisikia vizuri dakika kadhaa zaidi katika maisha haya magumu na mafupi ya binadamu.

  • Lidanganye tu kuwa unalipenda lenyewe tu na utalipenda mpaka ufe ,wakati unajua kuwa wewe ni binadamu na NIVIGUMU KUJUA hata dakika ijayo kama utakuwa hai au utakutana na ulipendalo zaidi , ambalo utalipenda mpaka wiki ijayo.

  • Lidanganye tu, kwa sababu kisiri linahisi kuwa unalidanganya ila linapenda kusikia tu ukilisifia.

  • Lidanganye kama halitapata UHAKIKA unalidanganya maisha yawe motomoto wakati ukweli ni VUGUVUGU.
  • Lidanganye listukie likuache ili uanze upya na jingine la kulidanganya.

AU liambie Ukweli uende mbinguni na kuliacha liende motoni kwa sababu linakudanganya.


Lakini...
...UKWELI ni mzuri kwa sababu UKWELi unaweza kuwa ni UONGO.
UKWELI ni kwamba, kila siku hata kama hutamki, unadanganya kwa ukweli.

Napenda unidanganyavyo kwa PODA na mavazi mazuri nihisi WEWE mzuri zaidi kidogo, wakati mwili unashepu kama nywelenywele za puani.

Napenda unidanganyavyo kwa tabasabu wakati unahuzuni, ili kunisaidia kusahau kuwa na mimi nina huzuni!

Lakini. narudia....
....UKIAMINI unachoDANGANYWA , kinakuwa UKWELI.
Ndio maana dini zote kwa waziaminio ni za KWELI.

Swali:
  • Hivi ni kweli inawezekana LISURA lako ZURI kila siku linazidi kuwa baya kwa jinsi unavyozeeka?
  • Umefanikiwa kudanganya Leo?

LiDanganye basi uende motoni kama unafikiri stori za mbinguni ni UONGO !

Lakini....
..... ukweli na uongo labda vinaleta maumivu ya UTAMU sawa!
SEMA UKWELI tu UMCHOSHE , si angekuchoka tu hata ungemdanganya.

NAACHA MKUU!

Tupumzike Na kupata BUSARA kwa kuangalia kidogo WANAWAKE wakipigana....

Halafu labda tumpate tena SHEIK mtoto a.k.a Muslim Saeed tuone uwezekano wa kupata BUSARA , akizungumzia kuhusu ALLAH


Au tu LUPE FIASCO aendeleze katika DAYDREAMING

UKIJIANDAA kucheka UNAWEZA usicheke MSIBANI wakati MAITI inachekesha!

KUNA kitu unajua , ndio maana KUNA kitu kinakuchekesha!

Lakini...
.....Cha kwanza ufanyacho ukizaliwa, ni KULIA!
Kucheka kunakuja baadaye, halafu utachekeshwa na kitu chochote afanyacho akudongolosaye, na utacheka mpaka ukumbuke chuchu au uanze kulia kisa unausingizi, umejinyea, kama sio kujikojolea wewe toto changa.

Unaweza ukabisha!
KITU chochote ukionacho hapa duniani ni kichekesho !
Inawezekana kabisa mwendo wa BATA kwako si kichekesho lakini wamvunja mbavu mtu fulani.
NI kweli unajifunza kuchekeshwa KITU kama vile ujifunzavyo kuchamba baada ya haja kubwa.

Haki ya MIUNGU au KIBUYU tena!;...usipojua kitu, hakuna KICHEKESHACHO.


Ndio maana...
.....Watanzania wachekeshwao na ZE COMEDY wanaweza kuonekana taahira, kwa wasioelewa hali halisi ya Tanzania isababishayo hata lafudhi ya KISUKUMA imchekeshe MSUKUMA aliyezaliwa KIBAHA.

Na...
... kama EDDIE MURPHY au DAVE CHAPELLE wanakuchekesha, usishangae kukutana na adhalilikaye kwa kukushuhudia huchekeshwi na visa vya PWAGU na PWAGUZI, kama sio KIPEPE.

Usiwe na wasiwasi lakini...
...ni kweli tukikutazama unaonekana mjinga kama mimi, kwa kucheka uchekeshwapo mbele ya waiostukia unacheka nini na kwanini akijamba inachekesha.

...ni kweli mara nyingine ukianza kucheka kwa sababu kwako kinachekesha, wengine wanaanza kukucheka wewe kama tu ambao huchekeshwa na kicheko chako kiwakumbushacho kuku akipaliwa.


Swali:

  • Ushaliangalia kwa makini kubwa zima likijaribu kumchekesha mtoto mchanga?
  • Unakumbuka lugha watu wazima watumiazo kulichekesha toto changa ziletavyo maana?
Lakini....
....Inaudhi kuangalia kipindi cha vichekesho halafu huchekeshwi:-(
..unaweza kumhurumia pia ajitahidiye kuchekesha halafu hachekeshi!

NDIO...
....Wakati unahitaji kucheka , utachekelea ujinga tu hata kama unajifanya wewe hupendi mambo ya kijinga.

NA....
......labda, maisha yako yana maumivu ,kama kubwa zima unafanya maandalizi ya kwenda kuchekeshwa au unalipia ili uchekeshwe.
Swali:
  • Unakumbuka enzi zako za kucheka kwa sababu kuna kichekesho na sio KUCHEKA kwa kuwa umejiandaa kucheka kwa sababu kuna kipindi au LIMTU lichekeshalo ?


INAWEZEKANA wachekeshaji ndio watu wenye huzuni kama wewe mwenye huzuni!

INAWEZEKANA wewe na mimi ndio wachekeshaji na ndio VICHEKESHO!

Cha ajabu....
......labda unafuraha ,na labda bado unataka kuendelea kuchekelea sana kwa kujidai kumkataza akuambiaye ujinga kuwa; atakuvunja mbavu kwa kukuchekesha asipoacha kukushikashika kwa kauli tofauti na zikulizazo, kama sio kwa vidole vigusavyo kwenye kitekenyeo.

Halafu ...
.....utadhani kwenye huzuni ni vizuri kujaribu kucheka.
Cha ajabu ....
....kwenye huzuni , mara nyingine ndiko huruhusiwi kucheka , kisa lijamaa walipendalo na labda hata hukulipenda, limekufa!:-(

Kumbuka maisha yako ni yako peke yako na yanakupa uwezo wakustukia kichekeshacho kivyako mwenyewe, ingawa unachekelea KANYAU!

Siku uchekayo sana , unaweza kusahau , labda ndio siku yako ya huzuni .

CHEKELEA tu hata UJINGA, lione vile!
Nani kakuhakikishia vya maana sio UJINGA?

Chekelea tu kama unaweza na kumbuka HUZUNI inakusubiri tu kwenye KONA!
DUH!
:-(

Swali:
  • SI unakumbuka kuna walioshangilia SADAM HUSSEIN kakata roho?
NAACHA MKUU, topiki imenishinda!

Hebu twende kidogo kushuhudia jamaa likimpiga MKE wake kisiri kwenye DANSI


AU twende tu bungeni KENYA kushuhudia WAHESHIMIWA wakipigana....

AU ngojea tu niwaachie GROUNDATION wajaribu kuongea WAKATI pia UKIANGALIA PICHA za mpiganaji MANDELA

Wednesday, November 12, 2008

Hotuba ya Mwl. J.K Nyerere siku ya Jumanne Machi 14, 1995

Hotuba ya Nyerere iko kwa SUBI.
Inyemelee kwa kukongoli hapo chini..

nukta77: Hotuba ya Mwl. J.K Nyerere siku ya Jumanne Machi 14, 1995 (sehemu ya 1/3)

Asante Dada SUBI!

Tuesday, November 11, 2008

UTAMU wa MALAYA ,ukilipia!

Tuzungumzie UTAMU wa maembe kama kuna KA uwezekano neno MALAYA ni MATUSI!

NA labda....
...... tofauti ya utamu wa maembe na MALAYA, ni kwa sababu tunamfikiria MALAYA katika UTAMU HUU, ingawa pia anaweza akawa ananuka maembe.

UTAMU ni UTAMU, tofauti ni kasaikolojia nyuma ya apataye UTAMU katika matarajio au hata uhakika au kukosa uhakika kuwa atapata UTAMU kama autarajiavyo.

Urahisi au ugumu wa kupata UTAMU unaweza ukarekebishwa kwa fikira kuwa WEWE MLENGA UTAMU una kitu kikuwezeshacho kukusaidia kudaka UTAMU, kama vile pesa ,KAMA sio nyanya chungu.

Urahisi au ugumu wa kuwa utapata utamu, unaweza kukuza ufikiriavyo UKUBWA WA UTAMU au uhitajivyo utamu wa asali wakati hata utamu wa MAHINDI YA KUCHOMA ungetosha.

SAIKOLOJIA YA ALIPIAYE inamsaidia tu MLENGA UTAMU kumiliki matarajio kuwa anapata atakacho kwa sababu kalipia.

Lakini...
.....Kupewa bure kunautamu PIA, hata kama hupendi vya bure.

Tatizo ni.....
...... akupaye bure , anakunyima kumiliki KIBEZI cha kulaumu kama alichokupa hakina sukari.

Na....
.....Ukilipia, hushangawi kwa kulalamika; kanyama KAMBWA kenyewe kalikuwa kidogo halafu bomba la ugali.

Swali:



Inajulikana kuwa Mwanamke na DUME wote wamejaliwa baraka za kuweza kuwa MALAYA kwa tafsiri fulani ya KAJINA HAKA katamu 'MALAYA' ,kama anapokea fedha au nanihii, kama malipo ya kitendo.

Fedha inasingiziwa kuwa ndio malipo MALAYA apokeayo YEYE kwa kutoa baraka KWAKO kwa kujishughulisha ili WEWE ufike safarini au AKUPE nafasi kwako WEWE uonyeshe maringo yako KATIKA SHUGHULI ili ufike , IKIBIDI ,bila hata kufikiria asikiavyo utamu YEYE .

Lakini...
... MALIPO ni malipo hata kama sio fedha utumiayo katika biashara yako ya UJIMA, ndani ya nipe nikupe, ambayo ukinipa chumvi nitakupa muhogo.

Na labda unalipa kwa kumfundisha hesabu na wala sio kwa kumnunulia chipsi dume wakati wa mapumziko.



Swali:
  • Si inasemekana hakuna cha bure?
  • Si wewe mkali wa masomo halafu unaboa na hukawii kufundisha MTU ukichekewa?
  • Hivi mahari sio kulipia?

Labda ni kweli kufurahia kwako ulichotumia kulipia, hata kama ni senene, ni kwamba ulitaka kulipia na alitaka kulipwa .Na utaondoka kiwanjani ukijitutumua kama jemadari kwa sababu umelipia ,na yeye ataondoka anacheka mwenyewe kama HAKENUI MENO, kwa sababu kakulipisha zaidi kidogo bila kusafisha vizuri sehemusehemu za haja ndogo.


Sasaaa...
.....inawezekana labda unalipia UTAMU kwa lijamaa lako ingawa umelioa, limekuoa au ni LIJAMAA ambalo UNALIFIKIRIA tu kwa sasa, na hata siku moja hutawahi kujadili bei ya KUWA limtumwa lake kwa kisingizio wanadai maisha ya uhusiano ni magumu, MVUMINILIANAGE tu, kwani hata MAUMIVU ni UTAMU.

Unaweza usistukie ...
......kisaikolojia, hulipii kama hufikiri ununuavyo ni kununua au kumnunulia .

Lakini...
.....kama unapenda vya bure, utapenda tu vya bure UKIPATA.
......ukipenda vya kulipia , LIPIA, labda ndio furaha yako HATA KAMA bure unaweza kupata .

Kwa sababu labda vya bure , unahisi ni bure kwa sababu HATA ULICHOLIPIA kitakuwa bure mpaka uhisi UNALIPIA.

Kama unafaidi zaidi nanihii ukilipia, lipia ufaidi ,kwa sababu labda unalipia hata kwa kujiuliza sijui ulipie au la.Kwa maana vya bure upatavyo HATA KAMA NI VITAMU , utahisi haviji na kachumbari kwa juisi ya ukwaju, kitu kitakacho kuhakikishia mapungufu TAMU TAMU ya UTAMU.
Swali:
  • Unahisi hujawahi kulipia utamu?
  • Hivi ukitenda mazuri ,wanaodai utalipwa mbinguni ,unafikiri wanazungumzia malipo gani kama hujawahi kulipia hata kupiga chabo , kama shoo yenyewe bei ghali?

NAACHA MKUU!
Ngojea Sheikh YUSUF ESTES abadilishe topik na kuongelea kama unaruhusiwa kuangalia TV

Au ngojea MWANAFALSAFA aeleze asitavyo KUOA katika BADO NIPONIPO:

SIKUELEWI , labda WANAKUELEWA.

Ajaribuye, kajaribu ingawa simuelewi.
Nisipo kuelewa, wapo watakao kuelewa hata ikiwa ni karne ijayo.

Labda unajua , hata kwa sababu umesomea ndio maana unajua.
Labda kusomea kitu ni kukiri hukujua .
Labda una vyeti kama yeye na yule lakini unajua , hata kama kujua kwako ni kwamba hujui.

Labda unaonekana hujui ndio maana unahitaji vyeti, wakati sentensi yako kwa wakusikilizao , wewe ni profesa hata kama ni wa kuuza kigenge.

Tufundishe basi tusiojua!
Labda unajua tu na hata hukuenda shule ziitwazo shule , jando, na wala hukunemwa.

Kumbuka ajuaye , bado anaweza kutojua kuwa dakika ya mwisho mjuaji hana ujuzi wa mwendo wa MOYO wake kabla haujafunga breki, kama asiyejua tu .

Siku ya mwisho unaweza kushindwa kumalizia hata kikohozi wakati TUNAJUA unajua kubanja.
Toa ujuzi angali unaweza!

Ndio ....
...Nakuzungumzia wewe Injinia, Daktari, Mganga wa kienyeji , Binti Halufani na hata weye KIJEBA na Gangwe wa kimasomaso ambaye ni mjuaji...

...Namzungumzia wewe, mimi na yule......

NAAMINI KILA MTU KUNA KITU ANAJUA AMBACHO WENGINE HATUJUI.

Fikiria mara kadhaa kabla hujafa nacho UJUACHO dakika nisiyoijua na labda DAKIKA usiyoijua kama utakunywa sumu , kujinyonga , kama sio kujaribu KUAGA DUNIA kwa kujirusha mbele ya MKOKOTENI katika dakika uliyopanga ambayo unaweza USIFE na kiuno umevunja!

DUH!

NAWAZA TU hapa MKUU!

SIKU NJEMA!

Tupate Puppetry of the vagina , labda inaeleweka na tusiojua(samahani watu fulani mtakao elewa zaidi)


Au Twende kidogo ETHIOPIA kwa TEDDY AFRO atupe simulizi za JAH

Monday, November 10, 2008

Lione, JEUSIIIIIIIIIIII ,halafu ZURI KAMA MKAA!

Uzuri wa kamasi lako jeupe, labda ni tafsiri tu ya Uzuri AKILINI mwako na hata lingekuwa jeusi, usingekawia KUKATAA kuanza kulilamba hadharani.

Labda rangi ya ngozi yako ni muhimu tu kama rangi ya manyoya ya TAUSI dume kumeremeta katika jitihada za kujishebedua mbele ya tausi jike atakalo kumimbisha mayayi yake.

Labda ni kweli rangi yako ikiwa tofauti kidogo na ulivyo leo , utajiona mzuri zaidi kutokana na kulizoea li rangi la ngozi yako tokea uzaliwe, ambalo halikawii kuota ukurutu kama wewe si mahiri wa kuoga.

Lakini.....
...labda binadamu anaakili kuliko kuku ingawa , kuku mweusi na mwekundu wana kawaida ya kuendeleza ushoga bila kumteta kuku wakijivu kwa kutagishwa na JOGOO lenye rangi ya kahawia kwa mbaaaaali!

Swali:

  • Hivi ni kweli ZERUZERU hana rangi halafu kwa binadamu mwenye akili ,Mzungu na KAratasi vyote vyaweza kuwa vyeupe?
  • Umestukia weusi wajichubuao kama wewe ni mweusi unaweza kuwagundua zaidi kuliko weupe watumiao kila njia kupunguza weupe?

Sasaaa...

....Uzuri wa mkaa utaujua zaidi ukihitaji mkaa.

.....Uzuri wa rangi nyingine isiyofanana na rangi yako, labda unaujua kwa sababu unahitaji rangi nyingine.

TATIZO ni ....
.....NI KWELI UNAHITAJI rangi nyingine?

Uzuri wako labda unategemea umezungukwa na wabaya wanamna gani.
Na jinsi ujuavyo uzuri, ni matokeo ya jinsi ulivyojifunza na kufunzwa nini ni uzuri.

Na labda wewe ni mzuri !SIKUBISHII!
Swali:
  • Si toto baya ni zuri kwa mama yake?
  • Ushawahi kusikia mama kalinyima nyonyo toto kwa sababu ya jinsi lilivyo baya?

Jichubue, inamaana unataka kuwa mweupe kwa sababu za kujifunza kuwa utafaidi zaidi ukiwa mweupe.
Jichubue , utapendeza kama MICHAEL JACKSON.UTAJISIKIA vizuri tu kama ndio nia yako.


Hebu tumchungulie kidogo MICHAEL ,katika safari yake ya rangi...


Tatizo ni....

.....Hata uwe na rangi gani , kuna watakao iona haifai katika shughuli.
.....Ukimuuliza Barrack OBAMA , anaweza akakusimulia wampendao kwa rangi yake ,na wasio stukia rangi yake kama ilivyo kwako ingawa unafikiri kila mtu anajua KUWA wewe ni CHEUPE DAWA.

Kumbuka....
....Kuna sehemu wewe ndio haswa kivutio, na wengine wanataka kuwa kama wewe na wakiweza watajiotesha chunusi kama wewe kwa sababu umesababisha watu waone ni bomba la kitu kubinya chunusi kisimani.

.....hata kama wewe ni mweupe ushindaye juani kupata SUN TAN uwe mweusi kiduchu, bado sio mzuri kwa watu fulani halafu ni wengi tu.

NDIO....
... kwa watu fulani lazima wewe unasura mbaya ingawa wewe ni mzuri kijijini kwenu ambako ni AKILINI MWAKO.


Cha kusikitisha ni....
  • JAMANI mpaka karne hii watu waue wenzao kisa rangi tu?
  • Ni lazima Tanzania pamoja na umaskini tuanzishe biashara za kuua zeruzeru kwa nia ya kutajirika?

Mimi ni mweusi na sina tatizo na weusi wangu na labda wewe ni mweupe .
LAKINI labda kama dunia nzima tungekuwa tunafanana na ni rangi moja, nahisi kuna kitu ingepungukiwa ingawa labda tatizo lingeendelea kisa saizi ya ULIMI WAKO MKUBWA KIDOGO KWA SHUGHULI ya kulamba na UNAUMIZA.

Katika kutafuta kujielewa sisi kama binadamu, tunatafuta sababu kibao zisababishazo tuanze kufikiria tofauti zako na zangu na sio yaliyo mengi ambayo ni ushuhuda wote ni binadamu na tunahitajiana na tuko sawa INGAWA sio SAWASAWA .

Labda lakini tofauti ni kwamba wewe una akili na mimi ni mjinga, ingawa tofauti hizo zinaweza kukupa moyo wa kuishi ili unifundishe na kuniondoa ujinga na sio kunichukia kwa ujinga wangu.

Labda wewe unanguvu mimi dhaifu.
Nitetee basi !

Wakati tunazungumzia rangi au hata uzuri , labda kuna swala la muhimu zaidi tunaloliruka lisababishalo nakuona wewe CHEUPE dawa.
Tulifikirie basi kabla hatujachukua hatua!

Lione vile, meno mabaya halafu wala sio kibogoyo, ingawa halipendi meno yake kwa KUWA limesahau kuna vibogoyo!
LooH!

NAACHA BASI!
Tupate basi hekima ya Shekh AHMED DEEDAT atukumbushe kuwakumbusha wanawake wafunike vichwa au kunyoa nywele ili USIWATAMANI...(kazi kwako kama wewe kipofu na huhitaji kuona ili uvutiwe!:-()

Au ngoja tu PADRE na SISTER watuonyeshe UPENDO.....

R.I.P MIRIAM MAKEBA!


Mwanamama huyu katutoka. Naamini MIRIAM MAKEBA mchango wake ni mkubwa sana katika kuutangaza muziki kutoka Afrika duniani.

R.I.P mama!
(March 4, 1932-November 9,2008)



Muziki wako unaendelea kuishi kama hivi.....


Sunday, November 09, 2008

NICHEKEE niKUTONGOZE!

Unaalika kuambiwa !
Labda unaalika kuambiwa utakacho kuambiwa .
Unaweza kualika taarifa ingawa inaweza ikawa ni taarifa ya msiba wa jamaa unayetaka kisiri AFE.

Asilimia tisini na saba pointi sifuri, sifuri, sifuri, ulishamkubalia KIKWETE akuuzie maswala ya HARI MPYA wakati nia yako ni chupi ya zamani.

LAbda....
....ukihisi nafaa, sihitaji kauli yako kuniruhusu nikuchungulie sehemu sehemu.
Jicho lako ingawa wewe KIPOFU, laweza kunilengesha kuwa umekaa mkao wa kunilengesha maeneo NANIHII , nijue naweza kuchungulia NANIHII.

Kabla hauja ninong'oneza labda ushanitamkia kuwa una HAMU ya kunikubalia kama ulivyo mkubalia kuwa wewe MVIVU na unaenda KAZINI kwa sababu IMEBIDI tu!

Ni kweli pia unanogewa kwenda kazini ili uwe BIZE na maisha ,uhalalishe kuwa MAISHA YAKO YANA MAANA , na LABDA ni KWELI , kazi inakupa kanafasi ka KULIA, kumlilia na sio KUMCHEKEA au kumchekea apozeshaye MAUMIVU YA KIPELE kwa kionyeshacho UTAMU wa KIPELE.

DUH!
NAACHA basi MKUU!


Ngojea nimuachie Bill Clinton aendeleze katika....BOPIKILIKI


ASANTE tena kwa wadau wote !
Baadhi mnaweza kujistukia katika picha zangu ZA juzi ya jana......
Photobucket


Photobucket



Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket
Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket


Au labda Peter Tosh atukumbushe kuwa kama imeshindikana sasa hivi UNAWEZA KUANZA UPYA katika PICK MY SELF UP.

DUME likionjwa!

Jamii inataka kutuhakikishia kuwa ni JIKE linaonjwa wakati kuna wajulikanao kwa kula firigisi za BEBERU.


Labda kuna dume lisilo mtu!
Labda jike linaliwa kama unafikiri JOGOO si dume.

Kuonja ni kujaribu kama inafaa au haifai.

AU?
Kuonja sumu kama unajua ni sumu ,labda unajisikia kufakufa.


Najua unaweza kuonja makamasi kama unahisi kuwa ni siri yako wakati uko peke yako.
Labda nusa mavi yako kwa sababu bado unafikiria hayanuki kama kinyesi cha yule.
Ukionja dume, labda unajitahidi tu zaidi kidogo kwasababu huna uhakika Jike lina kautamu mtarajiwa.

Swali:

  • Unakumbuka labda katika mahusiano ya kuku wawili jike, labda mmoja ni jike?
  • Unajua labda katika Jogoo wawili katika penzi, labda mmoja ni jike na halitagi?

Kuna wengi kisiri wanaweza wasiwe na hakika....
.....lakini labda kama wewe sio nyama , USIONJWE lakini.

DUH!
Topiki imenishinda..



Ngojea basi tumsikilize MR PREGNANT akiri matatizo ya DUME ZIMA kutoona KIKOJOLEO.

Au twende mtaani JAPAN ....Katika BAD MAN FORWARD

Friday, November 07, 2008

KAMA HUNIPENDI, nipe tu MWILI WAKO kibahati mbaya ,kwa KUTUMIA AKILI!

Sina makuu!
Akili zako chuo kikuu, zangu shule ya vidudu na kuukuu.

Huhitaji kumuuliza mwalimu mkuu,
dhambi waniingiza kichwani , katikati na hata kwenye miguu.

Binadamu mwana haramu weye !

Nikikuangalia , ni mtu na wala sio mwewe.
Nikiwa dhaifu, wan'tia kiwewe.
Akili natumia mpaka kudoea lako pendo weye.

Nipe mwili, roho na moyo vya Mungu wako weye.
Nipe kidogo tu , sana nitachoka, nakumtamani yeye.
Usinifunze sana, nikijua , nitataka mahiri kuliko wewe.

Nipe kidogo nichangamshe damu.
Wewe na mimi ni binadamu.
Ya roho siyajui na hayatoki damu.
Tutayajua tukifa au kuishiwa damu.

Mwenzio na hamu!
Mwili wako kuliko akili ,wan'tia hamu.
Akili zako, ujauzito hazipati, hazin'tii hamu.

Unaakili utafikiri si binadamu!

Kama hunipendi ,mwili nipe, umen'tia hamu.
Kama dhambi, mijeledi wanichapa, jehanamu.
Naomba kidogo basi weye mwanaharamu!
-------------------------------------------------------------------------------------------

Wikiendi njema!
Tutaonana Majaliwa ,na usiniulize la hapo juu, mwenzio sina hamu......

Tutembelee kidogo koo lako lakini ..............Kuangalia VOCAL CORDS zako karibu na KIDAKA TONGE




Au Koffi Olomide na Lokua KANZA waendeleze simulizi za DIABOLOS

KAMA MAGIC JOHNSON ASINGETANGAZA kuwa ANA UKIMWI!

Ukimuangalia Magic JOHNSON unaweza kusahau kuwa ni mwaka 1991 ndio aligundua ana vijidudu vya UKIMWI. Anaweza akawa ana afya nzuri hata kuliko mimi na wewe hasa kama hatujacheki kama mwilini tuna vijidudu hata vya UTAPIAMLO.

Na labda ni kweli yuko fiti kuliko yule.....na .... ambaye unafikiria kucheza naye mchezo wa baba na mama pale gizani kwa sababu unaaibu ndio maana ushafikiria utazima taa wakati ukitoa sehemu za faragha.

Hebu muangalie hivi sasa alivyo ,baada ya zaidi ya miaka kumi na saba ya kuwa na UKIMWI, wakati akihojiwa na CNN kuhusu ushindi wa OBAMA



AU tuangalie tu habari muhimu kutoka CNN kama ihusuyo kuku kaonekana anavuka barabara...

OBAMA kashinda URAISI lakini bado MIMI nina MATATIZO ya kubanwa MKOJO!

Ingekuwa poa kweli kama kufanikiwa kwa Kinjekitile kungehakikishia mafanikio ya Kadoda.

Tatizo ni...
Zubeda akila , Mwanahawa anabaki na njaa tu kama hana msosi.

Hali halisi haigandi, na kafuraha hata kakufurahia mazoezi ya kutengeneza mtoto, kana nukta baadaye kidogo.
Kafuraha ka mafanikio ya wengine kanaweza kasikusaidie wewe kufanikisha kutunga mimba na kanamaisha mafupi tu.

Lakini labda ni kweli kuwa mafanikio ya muislamu ni mafanikio ya mkristo kwa sababu wote ni binadamu, ingawa inawezekana pia kuwa ushindi wa Nyerere ndio kushindwa kwa Iddi Amini.

DUH!
........Maisha magumu mpaka unaweza ukajifariji kwa ushindi wa mwingine kupoza kiduchu.
Maisha magumu mpaka unaweza ukasikia raha kwa kumsifia umjuaye kwa umahiri wake usioujua utakao kujidanganya unaujua.
Swali:

  • Unafikiri nani anakujua vizuri wakati wewe mwenyewe saa nyingine unanuna bila kujua sababu zako za mnuno wakati uko peke yako chooni?
  • Unauhakika na ya kesho?

Maisha maguuuumu halafu tunakufa!:-(

Maisha magumu mpaka.....
  • KAMA mkristo wa jumapili, JUMAPILI inakukumbusha kwenda MSIKITINI!

  • UKIIONA Bidii, inaweza kukutia uvivu, kama jangwa likukumbushavyo msitu.

  • Kuna wajuao wewe ni MUISLAMU wa kusali ijumaa watakaoshangaa jumatatu inakukumbusha kwenda kanisani .

Unaweza ukadhani kuwa kitu kizuri wafanyacho ni kivutio cha wote kufanya vizuri.

Lakini bidii inatia uvivu hata kama ni ya kushusha kilo au kumwaga lita baada ya kumaliza kula na kunywa.

Bidii za wengine zinaweza kukukatisha tamaa kwa kustukia ugumu wa shughuli itakayo kulazimu kuvua kabla hata hujavaa.

Ni utundu lakini kuudanganya ubongo wako kuamini kuwa kwa sababu kapata na wewe utapata.
NI ushujaa kujitafutia kama chake kwa jasho lako bila kuingiwa hamu ya kumloga , kwa sababu alivyopata inakutia moyo labda nawewe utapata na huamini uchawi na sio mwizi ingawa tokea mdogo unatabia ya kudokoa sukari.

Tatizo ni....
...aliyepata anaweza akawa ameiba kile kidude.

Lakini.....
Inawezekana ni busara kuweza kuishi na kukosa na kuelewa kuwa walionavyo, vyao ni vyao na wala huvihitaji kama tu usivyoliihitaji limchumba lako au limtu ulilengalo kama bado halijakupata.
Swali:
  • Unauhakika wakati unahangaikia maswala ya kulenga wewe sio mlengwa?
Lakini.....
.....NI AFYA kufurahia mafanikio ya wengine.
Kwani ni lazima kila siku iwe wewe tu ndio unapata jamani?



Naacha basi MKUU!

Hebu tumsikilize MUNISHI akumbushie mitazamo ya Wakristo katika MANABII wa UONGO

Au labda nimuachie tu MAD COBRA asifie ngono katika FLEX.....

Thursday, November 06, 2008

WAKATI unabisha HUKUJAMBA, labda unatumia nguvu za KUTUMIA nguvu TU!

MAITI haiachii ushuzi.
Kama hupendi harufu mbaya , inawezekana UNAUWEZO TU wa KUNUSA na sio kweli unapenda harufu nzuri.

Tunaweza tukajifanya hatukusikia ingawa unajua tunajua umejamba.

Kumbuka lakini....

Mara nyingine tusikiacho si kijambo ingawa tunabana pua wakati unajua uliburuza kiti tu.
Ukidhani tunadhani umeachia ushuzi, unaweza ukawa unajisikia kama tu ulivyojamba.

UKIKAA KIMYA si lazima maana yake HUBISHI na hutumii nguvu kwa kukaa kimya.
Swali:

  • Unafikiri hujajaribu kukibishia kijambo leo?
  • Bado hunibishii tu? LOOH!
  • Unauhakika hutumii nguvu kujaribu kunielewa kama niandikacho ni ujinga au ushuzi?
Ukijamba , kumbuka kuwa ulikuwa na cha kujamba.

BASI NAACHA MKUU!

Twende tena kiduchu basi KAMERUNI kwa RICHARD BONA aseme EYANDO


AU twende tu na South Afrika kwa SOUL BROTHERS waseme INTOKAZI

UKIONYESHWA picha ya LIMTU mara kwa mara nakuambiwa hilo LIMTU ni YESU.

Naamini unaweza ukadhani unajua sura ya KITUMBUA ingawa UKWELI ni kwamba unajua kitumbua ni utamu tu wa kitumbua na sio umbo la kitafunio kiitwacho KITUMBUA.

Lakini unaweza kukibadili umbo kitumbua na kukiita jina SIKUJUA , kama unahisi ndio jina kitakachoitika.

Unaweza kusahau!
Ukionyeshwa picha ya KAKOBE mara kwa mara na kuambiwa huyo ni KAKOBE, hukawii kuanza kuamini kuwa umuangaliaye ni KAKOBE.


KUMBUKA TU kuwa ukiendelea kuitwa NGURUWE kila mara na watu au PUSI wadhaniao unaitwa NGURUWE, hutakawia kuanza kugeuka au kuitikia jina NGURUWE.

Swali:

  • Unaitwa nani vile?
  • Unauhakika hilo jina lako ni wewe?
SIKU NJEMA!

Tulia tuangalie ujinga kama vile ujinga ni kuzaa


Au ngojea Wasalu Muhammad Jaco aka LUPE FIASCO aseme DUMB IT DOWN

ASANTE SANA kwa wadau wote na pia ambao hamkunitenga juzi ya jana ambao baadhi ni .....

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket
Au endeleza kuangalia kiwezacho kuwa ni busara kutokana na kona ya mtazamo wako sasa hivi kutoka kwa BUSTA RHYMES katika Lyte ya ass on FIRE

MFUATA dini, mvuta BANGI na MLEVI, kama wote ni WALEVI wa hichohicho kilevi chao ingawa MNYWA pombe ndio aitwa MLEVI!

Unaweza kubisha!
Ukiwaangalia wote bila sauti wafanyayo kwenye nyumba yao ya kilevi ingawa inaweza kuitwa KANISA au MSIKITI kama sio CHOO, wafanyayo katika kusujudu yaweza kukukumbusha mcheza mziki achezaye mziki vizuri wakati hakuna mziki .

Staili za kainama kainuka, kapiga magoti kabinuka, zinavalishwa heshima tu jamaa watafsirivyokuwa unamsujudia MUNGU wao wakweli ambaye ukweli wake kwako unauhakika kwa sababu wewe MSABATO na sio MLUGALUGA kama wale wajambao katika kuita MBINGU au kujaribu kukwepa JEHANAMU .

Kumbuka hata ubinuke vipi , kama humbinukii MUNGU au ZUBEDA aaminikaye analipa katika jicho laafikiriaye anajua nani ana tamutamu kunoga, wenye kuona waweza kutaka kukuokoa kwa kuzani unambinukia MIUNGU na sio MUNGU.
Swali:

  • Ukimsujudia kalumekenge unalamba eeh?

BAADAYE BASI!
Twende KAMERUNI kidogo kwa RICHARD BONA atekenye kwa kibao EKWA MWATO

Wednesday, November 05, 2008

Kuna mambo yawezayo KUKUKUMBUSHA wakati UMEVAA,ni kweli CHINI YA NGUO au GWAGURO bado uko UCHI!

Wakati natafakari ushindi wa BARRACK OBAMA.............

Labda ni kweli sio sisi wote wenye ujasiri wa kufanya.
Labda ni kweli sisi sote TUNA uwezo wa kufanya.
Labda tofauti ya wafanyao na wasiofanya pamoja na mafanikio ya utengenezaji wa mimba au ugali iko nyuma ya kujiamini na kujua halihalisi au kujijua.

Waweza kujisahau na kuishi kutokana na muonekano na sio halihalisi.
Hata kama hali halisi ni ukweli kuwa wewe ni uwezaye ,waweza kujikuta unaishi kama jamii ilivyokufunza kujiona au hata baba , mama na ndugu kama sio marafiki, walivyokupiga makonzi kwa kufanya wadhaniacho hakitakiwi kufanya hata kama kinaleta firigisi mezani.

Ukifuatilia jinsi watu wapatavyo moyo na matumaini ya uwezekano wa jambo kutokana nakushuhudia awezavyo mtu mwingine, waweza kustukia kushamiri kwa kutokuwa na uhakika chini ya sura za kishujaa za watu bwelele katika kuweza jambo.


Labda kwa watu weusi tunahitaji kuhakikishiwa na Ushindi wa Barrack Obama kuwa tunaweza kutokana na halihalisi ilioshamiri duniani kuwa mtu mweusi hawezi na Obama kama mtu mweusi aliyeweza ni nguvu yetu katika kutuletea imani yetu kuhusu sisi kwetu wenyewe.

Tatizo ni kwamba .......
....matumaini kama moto wa kuni , huhitaji kuni zaidi na zaidi na wachochea moto pia ili moto uendelee kuwaka.

Halafu.......
Histori sio shule nzuri, kamatu unakumbuka kuwa, kwa watu weusi , baada ya uhuru wa nchi nyingi za kiafrika , kulikuwa na mfumuko wa matumaini kuwa tunapiga hatua kujikomboa kwa kila aina ikiwepo muonekano na sifa za mtu mweusi, kitu ambacho mpaka sasa hivi kinasumbua.

Mpaka sasa......

  • Tunaendelea kupigana Congo , na sio muda mrefu hata Kenya ambako tumaini jipya kupitia Obama linaamsha hali ya kujisifia mtu mweusi, hakukua na amani.
  • Mtu mweusi katika tamaduni nyingi duniani inaaminika ana rangi isiyofaaa.

Sasaa tukumbuke tu kuwa ...
.. ukifurahishwa sana na kitu labda cha muhimu ni kujiuliza kwanini umefurahishwa na hicho kitu.
....ukifurahia sana kuvaa nguo , jaribu kukumbuka kwa nini unavaa nguo.

Labda kuna pengo ndio maana unataka kuziba.
Kuna pengo labda ndio maana tunafarijika.
Lakini.....
...kwa nini kuna pengo ?
Swali:
  • Unafikiri kwenye pengo nilazima pazibwe?
  • Unafikiri unaweza?
TUSIUE matumaini, chochea moto.
TUSIUE matumaini, ongezea kuni moto usizimike.
TUSIUE matumaini, FANYA.
Siku njema!


Tulia lakini na Martin Luther King Jr-I have a dream


Au tulia tu na Stevie Wonder -FREE

HONGERA OBAMA!

Hongera !
Tukumbuke tu bado yeye ni binadamu!


Au ngojea nitembee kwa video......
Kutoka kwa MadWhiteJAmaican kama utani watu wakifanya na kuhisi tu kuwa labda weupe hawatampigia kura......


Wengi kama akina Mighty Sparrow....Barrack Obama wakistukia uwezo....


Akina Fatboy Slim - Cant stop BARRACK



Ndani ya ushindani..The dance off



Mpaka hotuba ya ushindi.....

Monday, November 03, 2008

Labda KUPIGA KURA sio DEMOKRASIA bali ni JITIHADA za WAJINGA na werevu KUJARIBU kukubaliana.

Swali:

  • Ni nini kweli itofautishayo upigavyo kura na apigavyo kura akitaka na ukataapo ?
  • Unajua nini na anajua nini kiwatofautishacho katika maamuzi yahusuyo hata juisi ya ukwaju?
Inasemekana ni busara kuwa wengi wape.

....Lakini labda wengi wakiamua wanaweza kuchukua hata kinguvu, kwani wachache hata kama ndio wenye nguvu, labda waamue tu kuwa hawatalala kamwe ilikuweza kuziba kona zote za walio wengi kuja kutungua mapera wakati wote.


Labda hakuna mjinga wala muerevu kutokana na kwamba ujinga na uerevu ni mambo yakubunia tu na cha maana ni kwamba umechagua na unataka kuwa ushinde na walioshindwa wakubali na kuishi na ushindi wako wa ubwabwa , wakihisi au kutumaini angalau hata ukoko watapata kama sio utandu.
DUH!

Nawaza tu Mkuu,USITISHIKE!

Pumzika na Mganga wa kienyeji atabiri ushindi wa Obama

Au ngojea tuwasikilize Wabongo akiwemo Mwenyekiti Maggid Mjengwa



DUH
Asante pia wadau wote ikiwamo hawa ambao hamkunitupa hivi majuzi
Photobucket


Photobucket

Photobucket

Photobucket

Photobucket



Photobucket

Photobucket

Photobucket
Photobucket
Bila kuwasahau Bitty Maclean na Peter Hunnigale

Photobucket
Photobucket

Bitty..
Photobucket
Kama alivyonisaidia kwa kupiga wimbo wake huu.. It Keeps Rainin'


Au Peter Hunningale

Photobucket
Photobucket

kwa kunikumbusha wimbo wake huu- Roots & Culture

Saturday, November 01, 2008

NINA hamu na WEWE ingawa NITAKUCHOKA.

UNACHOSHA saa nyingine kama MIMI na YEYE, usijidanganye!

Labda mimi na yeye tumepungukiwa na uwakilishacho au utugawiacho, ingawa unagawa kinyemela, ndio maana hujastukia.

Ukinipa au kumpa, labda nimepata au amepata.
Nikipata, labda sikuhitaji ,ingawa sina uhakika na yeye kama anakuhitaji baada ya kumpa namna vile bila hata aibu.

LOH!

Kumbuka lakini.....

......Labda unanipa mbele wakati nataka nyuma.

Kumbuka lakini....
.....Mara nyingi wa mbele ndio wa kwanza kugonga ukuta ,na wa nyuma ndio chaguo la chui.


Nikikataa, bado labda hujazidisha!
Ukikataa, kumbuka nilitaka kukupa.
Swali:

  • Unafikiri hujamchoka?
  • Unauhakika dakika ijayo hutaanza kufikiria kuwa labda umemchoka?
Naacha basi!
BAADAYE basi kama hujafa!
Labda nitakuwa nimekufa baadaye lakini!
Si baadaye wote tutakufa?
AU?
USITISHIKE!
SIKU NJEMA!


Tulia na DELLA MANLEY akiwa na MUTABARUKAwakisema I KNOW


Au labda turudi tu TANZANIA kwa mwanadada ambaye na udhaifu naye, aitwaye NURU, akikiri anampenda MSELA


KABLA hujachomoa ,SI lazima ULIINGIZA au ILIINGIA.

Kuna vitu viko tu , ukichomoa labda haikuchomekwa.
Kama tu ulivyozaliwa na makengeza, haukuchagua kuzaliwa kujikuta mkristo halafu kunajisi dhambi.

Ujanja ni kuishi tu na ukweli .
Hata kama si mjanja, hali halisi ndio ukweli wenyewe hata kama hali halisi ni kwamba hupendi bamia.

Kujilaumu kwa ukweli kuwa una matege, kwaweza kukusaidia kujisikia vibaya wakati asiye na matege, ana miguu kama njiti.

Chomoa tu ukitaka.
Si iliingia?

Kujilaumu hata kama kunaundugu na kitu kibaya , labda ndio kitu kinachokusaidia kujisikia kuwa uko hai.
Kutojilaumu kwaweza kuwa kunakusaidia tu maeneo fulani katika wewe ambayo yana kaukweli kuwa hunampango na wewe ni boaring.

AU?

Jifinye basi usikie maumivu, kama huna uwezo wa kunywa sumu.
Na kama unanguvu ya kutafuta sumu uvunguni, labda unaweza bado kucheza nguti mkekani.
Ishi basi!

Swali:

  • Una uhakika uko hai kama hujui waliokufa wanajisikiaje?
  • Nani kakuambia kucheza bao sio kazi?
DUH!
Tulia na DJ FATBOY SLIM awarushe watu UFUKWENI pale Brighton