Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Fafanuzi ya HOJA ya kwanini inasemekana Rais KIKWETE anamuigilizia Rais NYERERE kushindwa , KWA KUTUMIA kielelezo cha SEHEMU za SIRI!:-(

>> Wednesday, August 11, 2010

[Tahadhari: Wazo limepinda na linakonakona kimtiririko kwa hiyo shauri yako kama unanisoma halafu huelewi, Miye SIMO!:-(]


Kabla sijakupotezea muda; 
KWA KIFUPI nachokilenga mjeledi  KINUNDU katika TARALILA hii ni kuwa:

´´Rais yeyote yule atakayechaguliwa TANZANIA awe kutoka UPINZANI au CCM hataweza kutimiza malengo ya WAMPIGIAO KURA kwa kuwa MIUNDO ya TAASISI za BONGO na UKIRITIMBA WAKE haufanyi kazi ipasavyo......

Na kiongozi ambaye hataweza kulenga PAMOJA NA YOTE , miundo ya TAASISI ZA SERIKALI na ufanyakazi wa TAASISI kwa kuziboresha au kuzipamburua  ili kuondoa ukiritimba - na ambaye hata lenga kujenga Taasisi MPYA  ambazo zinalenga matatizo ya WATANZANIA na TANZANIA sasa, .....
.....hata weza kuondoa RUSHWA, umasikini, UJINGA, na kwa kifupi ataendelea kurudia yaliyomshinda NYERERE ambayo yanamshinda Rais KIKWETE.´´
- Mwisho wa KINUNDU.



HEBU tuliangalie swala aka KINUNDU  kwa kuangalia jinsi KUTOKA WAZO la kitu mpaka MAFANIKIO YA KITU yahitajivyo ufanisi wa MIUNDO ya TAASISI  kwa  kuangalia dondoo za miundo ya taasisi za SEHEMU ZA SIRI aka uchi  wa MNYAMA    ziwezavyo  KURAHISISHA uelewaji  hasa UKIZINGATIA;....

 ......mfano wa JINSI  mfikiria kupata mtoto awezavyo kufanikiwa kupata mtoto IKIWA TU  miundo mbinu  na miundo ya taasisi HUSIKA zinamuunganiko usababishao KIFIKIRIWACHO kizae mimba.ukikumbuka tu hapa KILENGWACHO KATIKA MFAN ULIOPINDA ni kuangalia jinsi  MKUU wa SERIKALI na WAFIKIRIAJI WENZAKE wahitajivyo miundo mbinu bora  na MIUNDO YA TAASISI  BORA ili WAZO lizae MATUNDA.:-(


Mwanzo wa  mtazamo:

MFIKIRIA kuzaa mtoto ili kiutekelezaji azae mtoto ,....
..... miundo mbinu ya taasisi za sehemu za siri hufanikisha tu anachofikiria- hapa na maanisha kumpa mimba au kupata mimba-   kwa kuwa miundo ya taasisi za sehemu za siri ipo na inafanyakazi bila ukiritimba ,....

  • ....kitu kifanyacho WEWE KAMA MWANAUME kinakuwezeshaKUFANYA UFIKIRIACHO kiamshe hisia , HISIA ZIAMISHIAZO MAJUKUMU katika MIUNDO YA  taasisi ZA CHINI YA KITOVU ambazo zina mfanyakazi mwenye support system aka miundo mbinu na shehena ambayo ingawa kuna ladha kama motisha kusaidia kazi ifanyike na kimiminika kisafirishwe mpaka katika mdomo wa KIFAA cha fani.

  • ....kitu kifanyacho wewe kama MWANAMKE kisaidie unachofikiria na kama muda ni sahihi KITAIMINGI miundo ya TAASISI zako za sehemu sehemu  itumie MIUNDO MBINU  BORA   ya taasisi za sehemu zako za siri  ILI ziwezeshe  malighafi YAI iliyotengenezwa katika moja ya TAASISI MWILINI  ifikishwe kwenye uchochoro  WA MAKUTANIO ya yai na mbegu hasa kama  miundo mbinu ya upelekwaji wa YAI lisilodariziwa na  LILILODARIZIWA TAYARI mahali maalumu yote ikiwa ni katika kuwezesha mchezo wa baba na mama uzae matunda.

..... kitu KITUKUMBUSHACHO PIA umuhimu wa mahusiano ya watu- IKIWA KATIKA MFANO ni mwanamme na mwanamke wajuao mchezo  - ingawa KISEREKALI ni WAFANYAKAZI BORA WAJUAO KAZI  hata kama kuna TAASISI BORA  KIMIUNDO ili matunda yatokee.

KWA KIFUPI,....
....inahitaji ushirikiano wa MWANAMKE na MWANAUME  hata kama TAASISI ZAO ZA SEHEMU ZA UZAZI ziko bomba ili kusababisha matunda ya dunia kujazwa yafanikiwe kama tu ihitajikavyo TAASISI bomba ki miundo kitu ambacho TANZANIA HATUNA  ili kufanikisha MAWAZO YA RAISI  kufikia utekelezwaji murua  hasa ukikumbuka umuhimu wa TAASISI HIZO ZENYE MIUNDO MZUKA ihitajivyo wafanyakazi BOMBA..:-(



SAMAHANI ngojea nilainishe lugha:


Sasaaa....






Tanzania kwa MIAKA NENDA RUDI imesifiwa hasa na WATANZANIA WENYEWE kuwa ni nchi ya amani. Cha kushangaza ni kwamba pamoja na amani yake maendeleo yake yanautapiamlo kiasi kwamba utakuta NCHI ZISEMEKANAZO kukosa amani huwa wala hazitishwi kimaendeleo na TANZANIA ambayo hata kwenye MPIRA wa miguu wenye washabiki wenye munkari au kwenye POMBE ambako kuna washabiki wenye motisha tumeshindwa kuwakilisha katika dunia kwenye fani.:-(

Na wakati huu wa uchaguzi TANZANIA ni rahisi kushabikia KIONGOZI MGOMBEA mmoja au MWINGINE bila kujiuliza ni kwanini viongozi lukuki waliotangulia kuanzia Rais NYERERE mpaka Rais KIKWETE ,....
.....siye na amani zetu bado hatuchezi mbali na UMASIKINI, ujinga, CHUPI ZA MTUMBA ,.. ...nk

Na tunajua kuwa WATANZANIA wanaweza wakiamua hasa ukifuatilia jinsi tuwezavyo kufanikisha KICHENI PATI , harusi za ajabu, kushangilia timu za mpira wa ULAYA, mazoezi ya kupata na kumpa mtu mimba, kupata kilaji ,nk

SWALI:
  • Umenielewa nalenga nini?
  • Umesikiliza ni hoja gani za MGOMBEA ambazo zinatekelezeka na umefikiria ni kwanini KILIMO kwanza haimfanyi BISHOO ajisikie kushika jembe KIUTEKELEZAJI?

Ndio,....
...... labda TATIZO SIO NANI NI RAIS Tanzania kwa kuwa LABDA hata UMRUDISHE Moringe SOKOINE hakuna atakachofanya kama MIUNDO ya TAASISI zenyewe ambazo ni muhimu katika utekelezaji WA LILILOKUWA WAZO mambo yake  ni kama tako la Mzee aliyejisaidia kaba ya kuchambwa.:-(

Ndio,...
....na LABDA hata kukiwa na TAASISI zenye MIUNDO bora, kama hazina WAFANYAKAZI wajuao kazi na wenye munkari wa kazi ni BURE kama tu Mbwa jike ALIYE KWENYE SIKU ZAKE mwenye taasisi zenye miundo bora ifanyayo kazi sawasawa lakini hajuikumgawia mbwa dume KISHUGHULI au tu Mbwa dume hapatii MSHUGHULIKO wawezavyo kusababisha TAASISI KUTOTIMIZA lengwa ya duninani kujae zaidi MBWA.:-(

Swali:
  • SI unakumbuka ni KWANINI Waziri MREMA alifanikiwa kusababisha UJAMBAZI upungue kwa kustukia TAASISI katika miundo unahitaji vituo vya polisi vidogo karibu zaidi na WANANCHI?

NIMEACHA!

USITISHIKE MHESHIMIWA hili ni wazo tu    NA SAMAHANI kiduchu  KWA KURAHISISHA hoja ngumu na NZITO kwa kuiingilia kimtindo wa taralila za UJINGAbusara   MKUU !:-(


Hebu Don Carlos arudie mkuno-Time


Au tu DON Carlos arudie ndude-Just a passing glance





Hebu nimuachie tu Tenor Saw enzi za 1985 arudie-Ring the Alarm na pia Fever




Au tu turudi Senegal DAARA J wadunge tena kitu- ALLAH

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP