Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Kwa kuwa PROFESA MBELE sio ISSA MICHUZI!:-(

>> Saturday, August 28, 2010

Katika kijiwe  nilichopitia MUDA si MREFU,...

.... moja ya hoja ilikuwa  ni UFANANISHAJI na umuhimu wa wafananishwao katika JAMII.:-(

Kwenye MABLOGA wa ki -BONGO ambao wanatujumlisha na siyeMABLOGA ambao sio warefu,....
.... ikaanza hoja ya kwa nini  kuna WABONGO  waendao zaidi katika BLOGU fulani fulani kuliko BLOGU NYINGINE  ambazo kuna wadaio ndizo zimeenda shule zaidi na kunasa  BUSARA ZAIDI kuliko BLOGU ambazo wanahisi labda hazina mchango muhimu sana  kwa JAMII .

Swali:
  • Unafikiri ni kweli watu wote kwenye jamii, uonalo ni muhimu WEWE ni lazima na wao walione ni MUHIMU?


Moja za BLOGU maarufu na wafananishwao ikawa ni pamoja na  blogu ya  Lady Jay Dee, Kaluse na busara zake, Profesa Mbele , Mjengwa na Anko Issa Michuzi  bila kumsahau Chemi che Mponda, Dina Marios, Dinah wa DINAHICIOUS, Matondo , Mubelwa Bandio,Muzee wa Lundu NYASA, Edo Ndaki,..,...,... Matiya  William Malkiory,...na wengine wengi.:-(




Mengi yaliongelewa na kila MSHABIKI alikuwa na lake ni kwanini KALUSE ni zaidi ya BWAYA, au Yasinta Ngonyani ni zaidi ya Matondo Nzuzullima,.....
.... bila kusahau kuwa mjadala ulinoga pale WASHABIKI wa Profesa Mbele walivyo kuwa wanadai kuwa Profesa Mbele Mchango wake ni mkubwa kuliko wa Issa Michuzi kitu ambacho kilijibiwa na hoja kama:..
....kwani mchango wa Issa Michuzi kama ni mdogo kwanini hata akilini kwako kanasa MPAKA kila ukitaka kujua YA BONGO  moja ya kifusi cha habari za bongo ukifukuziacho ni hichohicho cha Mkuu wa Wilaya aka Issa Michuzi....nk..



Swali:
  • Kwa ni haiwezekani kuwa kila mmoja mchango wake ni muhimu  kwa auhitajio?
  • Kwani mchango wa Mama mzazi  na wa  Baba mzazi lazima ufanane  kwa kufananishwa kwa kipimo kimoja ki umuhimu wao?
  • Hivi ni kwanini watu hupenda kushindanisha  vitu NA WATU  hapa duniani , na kama napenda miziki ya Profesa J kwani inamaana  ni lazima Profesa J awe ni mkali kuliko Mwanafalsafa au AY ?

Hoja hizi za nani zaidi ZIMENISHINDA na mpaka leo ukiniuliza siwezi kudai najua ni nani zaidi kati ya Peter Tosh na Bob MarleyLady Jay Dee na Ray C Tatunane na Watafiti, SINDIMBA na MDUNDIKO, ....:-(


Swali kidogo zaidi:
  • Hivi Rais Mwinyi na Rais Mkapa nani zaidi?
  • Kwani unauhakika Nyerere alikuwa ni zaidi ya KAWAWA kwa Nyerere?


NI wazo tu liendeleao kunikuna kwakuwa nimeondoka katika kijiwe ambacho bado  Wamshabikiao Issa Michuzi na Wamshabikiao Profesa MBELE wanaendelea kulumbana nani zaidi ingawa kwa mtazamo wangu ni kwamba wote  wawili{Profesa Mbele na Issa Michuzi }nauhakika kuna shule wamewapa na nashukuru kwa kuwa mie ni mshabiki wa wote hawa MABLOGA WAWILI WABONGO ambao ni hazina ya TAIFA.



NI HILO TU MKUU!


Na hebu  nijaribu tena kujaribu kustukia ni nani zaidi kati ya Bob Marley na Peter Tosh wakati najua hakuna watu wawili duniani wawezao kushindanishwa kwakuwa naamini hakuna watu wawili WALIO sawa.:-(

Hebu Bob Malya arudie -Crazy Baldhead



Au tu Peter Tesha akune kwa ndude-Mama Africa

8 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Yasinta Ngonyani 2:10 am  

Mmmmh! Ama kweli kaazi ipo sikujua kabisa kama kuna kushindana katika kublog nilichodhani ni kwamba wote tuna nia moja ya kufikisha ujumbe kwa jamii. Lakini sikuwa kabisa na hili la nani ni bora kuliko nani. Ahsante Mt.Simon kwa matembezi yako na kukuta malumbano hayo na pia kwa kutokuwa mchoyo.

Fadhy Mtanga 7:07 am  

Mie nadhani ni ufinyu wa mawazo kujaribu kufikiri hayo. Kila bloga anablog kwa interest binafsi. Lakini kila blog naamini huwa na mchango fulani muhimu. Kupitia blogs tunapata maarifa ambayo tusingeyapata darasani.
Mtu mmoja aliwahi kuniuliza nani mkali kati ya Sidney Sheldon na Mario Puzo. Nilimjibu mkali ni yule unayemsoma wakati huo.
Mie mabloga wote nawaona wakali tu ndo maana wanablog.

Koero Mkundi 9:57 am  

Kuna wakati nilidhani kuwa maoni mengi katika blog ni dalili kuwa inasiomwa na watu wengi...... kumbe sikuwa sahihi, kuna watu wengi sana wanasoma blog tena wengi wa kutosha.

Kwa upande wa umarufu, sina uhakina na hilo, lakini nadhani kila mtu ni maarufu katika anga zake kwa maana namna anavyofikirisha watu.......

Masangu Matondo Nzuzullima 3:53 pm  

Mtakatifu, mjadala huu uko wapi? Naomba link.

Ningependa turejelee maoni makini ya Evarist Chahali aliyoyatoa katika hoja inayofananafanana na hii kule kwa Mzee wa Changamoto. Maoni hayo hayanapatikana hapa:

http://changamotoyetu.blogspot.com/2010/05/shule-shule-shule-twafunzwa-tufunzapo.html

Juzi nilitazama kipindi cha TV hapa kilichokuwa kinalinganisha eti serial killer yupi ndiye alikuwa "mkali" zaidi ya wengine. Binadamu!

MARKUS MPANGALA 6:35 pm  

nasubiri wenye imani wamalize kwanza kubishana SWAUMU ni haki au siyo haki na ina uhusiano gani na mungu.

Simon Kitururu 8:20 pm  

@Masangu Matondo Nzuzullima: Mjadala haukuwa mtandaoni.:-(
@Wote: Mmmmmhhh!

Yasinta Ngonyani 8:51 pm  

Mt. Simon kama hakuwa mtandaoni ulikuwa wapi? Je huwezi kutupeleka huko ilinasi tuungane nao?....Kapulya kwani nilikuwa nami nijue ni link gani hiy????

malkiory 9:33 pm  

Kitururu: Pamoja na kuchelewa kuweka kalamu, nadhani gossiping nayo ni sehemu nzuri tu ya kujipatia feedback. Nadhani michango ya wadau itakuwa ni chachu katika kumaliza ubishi wa mdahalo uliozuka kijiweni.Cheers!

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP