Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Coco Fathi Reinharz- na mapishi ya Kiafrika katika steji ya dunia

>> Tuesday, January 02, 2007

Katika kuongea na rafiki yangu mmoja, nilipata kuzinguka kwa jinsi gani kuna watu wengi duniani wanaamini Afrika hatuna mapishi. Kutokana na vyombo vya habari kuzidisha habari za watu kufa njaa Afrika, basi kuna watu wengi waaminio kuwa Waafrika hula chochote ilikuwa hai tu. Wanadhani kuwa Afrika hatujui ladha za vyakula, kwani hatuna luxury hiyo.Ikabidi nicheke sana, kwa maana nikawauliza hivi hata historia za juzi juzi ambazo zinaikubali Afrika kama sehemu ambayo utundu wa viungo vya Chakula umesahaulika? Hivi hata Zanzibar si ilishawahikuwa maarufu duniani kutokana na viungo?

Lakini sasa hivi naona wameanza kuibuka wapishi wa vyakula vya kiafrika wanaosifika na kuanza kutambulika kimataifa.Mmoja wapo ni huyu Coco Fathi Reinharz aletaye mapishi ya kiafrika kwenye Five Star hotels. Ninachojua, sifa yao kubwa imetokana kuweza kuandaa na kukifikisha chakula mezani kwa staili ambazo Wamagharibi wanazizimia . Pamoja na jambo hili kuwa zuri najiuliza hivi kwanini ifikie mpaka tubadilike ndio tutambulike? Mbona Wachina na staili yao ya kula karibu kila kitu na pia kula na vijiti hawalazimiki kuibadili?Nafikiri mapishi mengi ya Kiafrika kutokana na ugumu wa kupata resepi zake katika maandishi, inapunguza kasi ya kujulikana kwake. Afadhali Miriam anasaidia kutatua swala hili.
Wakati nikiendelea kulitafakari swala hili, ni matumaini yangu siku moja habari ya Waafrika kufa njaa itakuwa inasomwa kwenye vitabu vya histori tu.

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP