Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Unapenda kula mate eeh?

>> Thursday, January 18, 2007


Unalikumbuka busu la Yuda Iskarioti?

Nilikuwa na jaribu kuelewa historia ya busu kwa kipindi kirefu kidogo. Hii ni baada yakuanza kujiuliza hivi ni kwanini watu wanapigana mabusu. Pia baada yakuona mabusu ya kila aina. Mabusu ambayo mara nyingi hunichanganya akili ni yale nionayo Viongozi wa siasa wakipigana mbele ya kamera ilikuashiria salamu ,uelewano.....nk.

Ukifuatilia kuna mambo mengi yanayo ashiria hii tabia binadamu walijifunza tu. Katika kufuatilia ndio nikaja kugundua kuwa kumbe kuna watu wamesomea mpaka udakitari katika kuchunguza busu.Nikaja kugungua kuna somo la philematology ambalo ndio likufanyalo ubobee katika stadi za denda.

Inasemekana inawezekana kabisa kuwa binadamu wamejifunza tabia hii kutoka kwa wanyama wengine. Kama ni kweli, mimi siwezi kushangaa kwa maana ukishuhudia mambo ya fanywayo na binadamu wapiganao busu unaweza kustukia mengi tu niya kinyama.

Lakini ni binadamu pekee ambaye amelipa busu sura na maana nyingi. Utasikia Waeskimo wanapigana busu kwa kugusanisha pua ilikuashiria salamu. Wafaransa wanakupa hili busu la kifaransa, mara nyingi kuashiria pendo kwa wapendanao, ambao wanapeana ruhusa yakunyonyana ndimi, ruhusa ambayo inaweza kuambatana na ruksa nyingine za miingiliano. Kuna busu takatifu ambalo lilizoeleka makanisani na kadhalika. Utasikia kuwa Yuda Iskarioti alimpiga busu Yesu ilikumsaliti. Utasikia mwingine kapigwa busu ilikuzalilishwa. Vilevile nafikiri uliwahi kuona Kofi Annan akimpiga busu Arafat katika kuashiria salamu.Lakini busu maarufu ni la wapendanao. Ukiwakuta wapendanao wakilana denda mwenyewe utakoma na jinsi waonyeshavyo kusikia utamu.

Katika haya yote mabusu mimi naliogopa zaidi hili busu la Yuda Iskarioti, busu la usaliti.

Dondoo:
Lakini unakumbuka kuwa mdomo unasemekana kuwa una bakteria wengi kuliko hata sehemu za siri?


Inasemekana zamani Afrika ,hasa sehemu za chini ya jangwa la sahara hatukuwa na tamaduni za mabusu(hapa naongelea denda la kimapenzi).

Inasemekana mara ya kwanza Waafrika Afrika Kusini walipoona wazungu wanakulana denda walidai hii si poa ni uchafu .

Look at these people! They suck each other! They eat each other's saliva and dirt! — Tsonga people of southern Africa on the European practice of kissing, 1927

Lakini naamini ukienda sasa sehemu hiyo hiyo jambo hili litakuwa ni la kawaida.

Inawezekana kuwa kusalitiana kulikuwepo , lakini ukweli ni kwamba kupo. Sasa mimi naona hata busu la usaliti limeota mizizi.

Inashangaza jinsi binadamu tunavyojifunza kirahisi kuzoe mambo.

Sijui sana historia ya busu Tanzania . Nachojua denda linanguvu Tanzania. Watu wanakuladenda la nguvu.Lakini linanisikitisha kuwa denda la usaliti halichukuliwi umaanani na wala halionekani.

Swali:
Hivi sisi Tanzania ndio tungekuwa tumeendelea, matajiri, na wenye uwezo unafikiri tungekuwa tunatoa busu gani?

Mimi natishika sana na jinsi sisi tunavyozoea mabusu haya ya kutusaliti. Natishika na jinsi kwa kisingizio cha diplomasia viongozi wetu wamebobea katika mabusu ya usaliti,busu la Yuda Iskarioti.

Nasikitika kuwa wengine tunazoea hata kudanganywa, shida, ...nk kwa kisingizio kuwahiyo ndiyo hali halisi.


Unapenda denda eeh?
Ngojea niwaachie Ladysmith Black Mambazo wakuletee wimbo ...

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP