Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Hapo Zamani Sikuwa Hivi!

>> Sunday, January 14, 2007

Ukisikia msemo usipofundishwa na wazazi utafunzwa na ulimwengu unaweza ukafikiri maana yake ni kwamba upumzike kama wazazi washakufundisha. lakini ukweli ni kwamba hata ufunzwe vipi na wazazi ulimwengu hautakuonea aibu kukufunza, utakukatia denge tu na kukuweka kwenye kona.

Nazitamani enzi za utoto ambapo ukitaka kitu wazazi wanakupa tu. Halafu wakichelewa unaweza ukalia au kununa mpaka unapewa. Siku hizo kwa bahati mbaya ni za mpito. Ukweli wa maisha unaanza kuingia na siajabu ukakushtukizia tu.Ghafla unaanza kusikia unaanza kupewa shikamoo.Inafikia siku unastukia kuwa uko peke yako au labda ndio wewe unategemewa.

Dondoo:
Je , unawakumbuka watoto yatima na wale ambao inabidi wajitafutie wenyewe tokea utotoni?

Ukiwa na bahati unastukia mambo ya starehe au usipo bahatika moja kwa moja jasho linakutoka. Kwa wengine mtungi, mivuto na ngono inapata nafasi zake kutokana uhuru unaojitokeza kutokana na umri au kukua na kipato.Kama wanabongo fleva vijana wa Ngweair
hapa chini wanavyotuelezea siku yao.


Dondoo:
Lakini unawasikiliza wanasema nini?

Hapa sasa ni patamu kwa sababu kutokana na nguvu za ujana lolote laweza kutokea ambalo lika elekeza maisha yako kulia au kushoto. Enzi za mababu zetu au hata mababa zetu kulikuwa na taratibu zinazofuatwa za kimila ambazo zinamuongoza mtu katika kukabiliana na mambo mbalimbali ya maisha. Kwa wale waliokuwa wanapelekwa jandoni, walikuwa wanafunzwa jinsi ya kuwa mwanaume ndani ya familia. Na kwa wanawake walikuwa wanafunzwa jinsi ya kuishi na mume na kulea watoto na mambo mengine muhimu katika familia. Uchaguzi wa mke au mme ulikuwa ni wa wazazi ambao walihakikisha kuwa wanakutafutia mtu ambaye anasifa waaminizo zinakufaa.Kupendana mlikuwa mnajifunza baadaye. Hili jambo pamoja na mapungufu yake lilikuwa linaondoa baadhi ya matatizo ambayo tunakutana nayo hivi sasa.

Kizazi chetu ambacho tumejichukulia jukumu kina kasheshe zaidi.Halafu jinsi dunia inavyobadilishwa haraka na mateknolojia na mambo mengine kadhaa, kwa asilimiakubwa unaweza kujikuta mambo ya busara na ujinga kwa wengi ni magumu kuyatenganisha.Kuna mambo mengi unaweza kuyachukulia mfano lakini moja wapo ligusalo watu wengi ni mahusiano. Mahusiano katika jamii yanabadilika. zamani ulikuwa unawezatu kuamua kumtembelea mtu kwa sababu ni ndugu yako. Siku hizi pamoja na kwamba jambo hili linatendeka ,lakini hata ndugu anaweza kukustua ebwana eeh!Umekuja kufanya nini ?Unajua hapa waya mkali hivyo kama huna mpango afadhali anza tu.
Siku hizi hata wazo la mahusiano na umpendaye au hata wazo zima la kupenda tumelitafsiri vingine.Hivyo tunaanza mapema zoezi la mahusiano. Na mara nyingi inachukua kuvunjika kwa mahusiano kadhaa kabla hatuja tulia. Na hata tukitulia bado zoezi zima la mahusiano si rahisi. Tena afadhali siku hizi tuna simu nyingi bongo hivyo simu kama hizi aziongeleazo Muddy Waters hapa chini ni kawaida sana.


Maisha ni mchezo wa ajabu sana. Kwa maana unachezeka kinamna nyingi. lakini kitu kimoja cha ajabu ni kwamba siamini kuna anayeshinda kila kitu. Ukiwa angalia akina Mandela utagundua kunasehemu kuna mapungufu. Halafu utasikia Mfalme hana furaha na masikini anacheka mtaani. Halafu mchezo huu hauchagui shehe wala mwizi.

Lakini katika yote ,wengine hatutakwepa kukubali pamoja na ugumu wa maisha na yote mengine yatufanyayo tuishi namna hii , HAPO ZAMANI HATUKUWA HIVI.

Au Miriam Makeba anasemaje?.......



Lakini usiwe na wasiwasi ,kuwa na furaha kama akwambiavyo Bobby Mcferrin hapa chini.



Kuna marafiki zangu kadhaa wapitiao hapa wanasema niache kuongelea mambo haya. Lakini kabla sija acha niachie maoni yako .

HAPO ZAMANI WEWE ULIKUA Je?

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP