Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Mchango wangu na wewe kwenye habari za dunia yetu ya kiungwana iongozwayo na George Bush

>> Tuesday, January 23, 2007

Ukitazama televisheni au hata kusoma magazeti ni mara nyingi kukuta habari mbaya ndio zimetawala. Ni rahisi kulalamikia vyombo vya habari lakini ukweli ni kwamba vyombo vya habari mara nyingine navyo huandaa mambo yake kutokana na kuijua saikolojia ya wasomaji wake.Naamini kuwa vyombo vya habari vinanguvu ya kuchonga mitazamo ya waletewa habari, lakini naamini pia vyombo hivi pia vinaweza kubadilishwa kutokana na wateja wake kubadili msimamo na mitazamo yao kuhusu habari wapashwazo. Kwa ujumla hali ya dunia ni matokeo ya nini binadamu wanafikiria na wanavyotenda. Cha kusikitisha ni kwamba, sura ya dunia leo hii inatokana na binadamu asivyofikiria.

Vitu tuvipavyo kipaumbele mara nyingi hata bila kufikiria ndio vichongavyo hali halisi ionekanayo.

Naamini shida na raha lazima vitakuwepo hapa duniani kwasababu shida huhitaji raha na raha huhitaji shida ilikuonyesha utamu wake. Lakini halihalisi ambayo inafanya wengine wasaze na wengine wakose kabisa haikubaliki. Kuna mambo mengi ni rahisi mtu kujitoa kuwa yako nje ya uwezo wake.lakini kila mtu akifanya machache aliyonauwezo kupeleka muelekeo wa mambo akupendako inasaidia sana.

Naamini habari mbaya zitakuwepo , lakini je, ni lazima ziwe zina tawala kwenye vyombo vya habari za dunia?Na sivitendo vyetu visababishavyo baadhi ya habari hizi?


Kila kukicha, vita huku, majambazi kule, magonjwa , njaa na kadhalika.

Inawezekana tunasahau kamchango ketu kamabaya au tunasahau kuchangia mazuri kutokana na kubanwa na mambo kibao.Mambo kibao mengine tuyaitayo maisha magumu.Lakini mimi naamini mchango mwingine si lazima uwe kama wa Mandela katika Afrika. Mimi naamini lolote jema linawezakuwa mchango kama mtu atalifanya.

Mfano unaweza kumonyesha pendo mtu na kumfanya afurahi?Aliyefurahi naye ni rahisi kumfurahisha mwingine. Kwa hilo tu watu kadhaa watakuwa wamepitisha wakati kwa furaha.

Duh , lakini ushawahikupenda kitu mpaka ukalazwa kwenye hospitali ya wagonjwa waakili kama Alpha Blondy asemavyo hapa...


Kuna viongozi fulani mimi naona wanachangia sana duniani tuwe na habari mbaya.
Nikiulizwa kwa nini viongozi wengi duniani huwa hawapendi kuachia uongozi naweza kushindwa kuwa na jibu.Nashindwa kumuelewa kabisa huyu Mzee Lansana Conté. Huyu Mzee ni mgonjwa na amekuwa katika uongozi tokea mwaka 84. Hivi ndio tuseme hakuna mwingine ambaye ataweza kuongoza nchi?.Huyu Mzee habari zake na mambo yake yametawala sana wiki hii. Na sioni ni kwa sababu gani anatoa mchango huu. Viongozi wengine kama akina Museveni mimi nashindwa kuelewa kwanini wawetu madarakani. Kwa maana unakuta kiongozi anapitiliza mpaka kuondoa hata yale mazuri aliyochangia kwa sababu tu awe kiongozi.

ukiongelea wachangia habari mbaya si viongozi wa Afrika tu. Ukianza kuwaongelea wakina George Bush, ndio basi tena. Chaajabu yeye ndio anayesemekana kuwa ni kiongozi wa dunia ya kiungwana(civilized world).

Naogopa kukiri kuwa tusipokuwa waangalifu au kama si waangalifu, ni mimi na wewe tunaoweza kuwa kiini cha habari mbovu kutawala dunia. Tusisahau kuwa ni mimi na wewe miongoni mwa waijazao dunia hii kimawazo na hata ki-kabon daioxaidi.
Watu wengi husema ni ndoto kuondoa matatizo duniani. Mimi nasema haiwezekani kuondoa matatizo duniani. Lakini ni matatizo, shida na madhara mengi duniani ambayo hakuna haja ya hayo kuwepo. Haya ambayo yapo kutokana na kuchangiwa na sisi binadamu kutokana na mitazamo yetu potofu na kufikiri kwetu au kutokufikiri kwetu yatutesayo au yatesayo wengine ambayo yanakwepeka, yanatibika ,hayastahili kuwepo. Ni vizuri tukijaribu kukumbuka hili.

Hivi ingekuwaje dunia ingekuwa kama John Lennon alivyoimba katika wimbo imagine?....


0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP