Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Nani mbaguzi zaidi?

>> Friday, January 19, 2007


*Watu weupe au weusi?

Duh, nilisahau kuwa katika makundi mengine Ndesanjo ni mweupe.
Sijui Marekani wanajua hilo?

*Wazungu au Waasia?


Duh, hivi kumbe Wachina na Wahindi wote ni Waasia!

*Wakristo au Waislamu?
Hivi kumbe Waothodox , Wakatoloki na Wasabato wote ni wakristo!
Hivi kanisa lipi linapeleka watu mbinguni?

Hivi kumbe Washia na Wasunni wote waislamu!

*Wachaga au Wapare?

Duh, nilisahau kuwa kuna ubaguzi ambao uko na umejijenga pia ndani ya makabila yenyewe bila kwenda nje ya kabila!

*Wewe au Mimi?
HIVI KWANINI HATUFURAHII TOFAUTI ZETU?

KWANINI TWAZITUMIA SANA KUTUTENGANISHA BADALA YAKUTUUNGANISHA?

Hivi ni kwasababu ya uoga tu, au ndio kwamba ubaguzi uko ndani ya chembe zituundazo zilizojengwa kuhimili uwepo wetu hapa duniani?

Hivi tunajifunza kweli? Au ndio siku moja hapa duniani itakuwa ni watu weusi wanakandamiza watu wa rangi nyingine?

Hivi watu wote wakiwa sawa , nchi zote hazina tofauti, kila kitu sawa , itakuwa bomba?

Wewe unafikiria nini kuhusu hili?

2 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Anonymous 6:48 pm  

Kuhusu nani mbaguzi nadhani nisisi wenyewe,inchi au serikali haiwezi kubaguwa kwasababu serikali ni mimi na wewe,binadamu tuna roho za kwanini,roho za korosho.

Anonymous 6:48 pm  

Kuhusu nani mbaguzi nadhani nisisi wenyewe,inchi au serikali haiwezi kubaguwa kwasababu serikali ni mimi na wewe,binadamu tuna roho za kwanini,roho za korosho.

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP