Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Watanzania na matakwa Gari Mkweche!

>> Thursday, January 11, 2007

Binadamu anazaliwa tayari akitaka. Kuna mambo mengi watu wamejaribu kuelezea kuhusu matakwa ya binadamu. Mtoto akizaliwa tu atalia kuashiria kuna mapungufu. Kuanzia hapo safari ya kutaka inaanza. Wengi nafikiri tumeanzia katika kutaka maziwa ya mama, lakini leo hii matakwa yetu yashakua magumu hata kuyaelezea. Na ukichanganya matakwa yetu yote Watanzania ukayaweka katika umbo la gari basi gari hilo ni mkweche.Mkweche kutokana na ukweli halina mbio na huaribika haribi kila wakati. Na ukimuuliza mtu mwingine anaweza kusema hata maili kadhaa lilizovuka ni kutokana na kuvutwa. Sasa gari hili ni lazima litengenezwe la sivyo tutabaki maporini.

Baadhi ya watu waliojaribu kuelezea matakwa ya binadamu na nini kinawasababisha wachukue hatua fulani fulani ni huyu Abraham Maslow.
Yeye aliyagawa matakwa haya katika sehemu tano katika miaka ya arobaini huko.

1.Kibaolojia na kimaumbile kama:hewa, chakula, kinywaji, pakuishi, ngono, kulala nk
-Biological and Physiological needs - air, food, drink, shelter, warmth, sex, sleep, etc.

2.usalama: kujikinga na mambo kama mvua,juakali, usalama kama kutozurika na wanyama watu wengine,nk
-Safety needs - protection from elements, security, order, law, limits, stability, etc.

3.Kukubalika kundini na kupendwa au kupenda:Kundi la kikazi,famili,mpenzi nk
- Belongingness and Love needs - work group, family, affection, relationships, etc.

4. Sitaha/heshima:heshima binafsi/kujiamini, kuwa huru, kuheshimika katika jamii,cheo nk
-Esteem needs - self-esteem, achievement, mastery, independence, status, dominance, prestige, managerial responsibility, etc.

5.Haja ya kujitimizia mambo:
-Self-Actualization needs - realising personal potential, self-fulfillment, seeking personal growth and peak experiences.


miaka ya tisini mwingine katika kumuelezea Maslow akaongezea nyingine tatu

1.Kujua:
-Cognitive needs - knowledge, meaning, etc.

2. Maswala ya kutafuta uzuri wa kujitakia. Kama vile uzuri kwa kufanya mazoezi...nk
-Aesthetic needs - appreciation and search for beauty, balance, form, etc.

3. Matakwa ya kusaidia wenzako kufikia pale watakapo
-Transcendence needs - helping others to achieve self actualization.

Ukitumia mtazamo wa Maslow katika kuangalia Watanzania utakuta kila mtu yuko katika sehemu tofauti kimatakwa. Wengine ndio kwanza wako katika namba moja wakati wengine wako namba nane. Wanyonge wanahangaika kupata msosi na pakulala wakati wengine wanayasikia matatizo haya redioni.Hili ni jambo lakawaida ni liko duniani kote. Ila nadhani tofauti ya Tanzania ni kwamba matakwa yetu hayafuati mkondo mmoja.Na Tanzania hakuna mfumo uliojijenga uongozao utimilizaji wa matakwa ya watu katika mwelekeo mmoja. Hivyo tajiri na masikini mara nyingi ukifumba macho husikii tofauti. Vilevile mwenye busara na mjinga mara nyingi ukifumbua macho huoni tofauti.

Tatizo jingine katika gari matakwa mkweche hili ni ukweli linaendeshwa na dereva anayebunia barabara. Basi hapo ndio utamu ulipo.

Pamoja na ugumu wa kuyachambua matakwa ya binadamu ,mimi bado nafikiria kuwa ni vigumu zaidi pia kuyaelewa kabisaaaaa matakwa ya viongozi wa Tanzania. Kwa maana mara nyingine naona kama wanatabia zilizo changanyika.Wanafanya mambo kama walalahoi halafu hapo hapo wanafanya mambo kama ya wenyenazo. Viongozi wengi wa Tanzania ni ombaomba halafu hapohapo wafujaji. Rushwa wanataka katika ombaomba zao halafu vilevile hukawi kusikia wanavyofuja mali za umma.

Hivi Watanzania wanataka nini?

Dondoo:
Hivi wewe unataka nini?
Labda tuseme unataka mtoto. Wa nini? Labda ili familia ikamilike? Ili iwe nini? Labda iliakusaidie Uzeeni. Ili iwe nini? Kama ni ili akusaidie uzeeni. Je, wewe unataka mtoto au unaweka bima ya uzeeni? Majibu na maswali ya unataka nini ni mengi.

Lakini hebu niambie! Hivi ni kweli unataka hicho unacho kitaka au unadhania tu kuwa una kitaka?

Umuhimu wa kujua matakwa yako na kwanini unataka ni muhimu. Mara nyingi unaweza ukadhania tu unataka kitu kumbe ukweli ndio huo kuwa unadhania tu. Ukipewa hicho kidude unagundua wala hukihitaji. Kujua ukweli kuhusu tabia za matakwa yako si rahisi lakini ni muhimu kujaribu kufikiria jambo hili. Unaweza kujikuta kuwa unapoteza muda kwa vitu ambavyo si muhimu kwako.

Dondoo:
KUJUA. Je, unajua?
Mwandishi Robert Fulghum alishawahi kuandika katika kitabu chake kiitwacho All I Really Need to Know I Learned in Kindergarten kuwa baada ya mihangaiko yote akagundua cha muhimu alichokuwa anataka kujua maishani mwake alijifunza shule ya vidudu.
Mimi nafikiria katika matakwa pia unaweza ukakuta baadhi ya mambo mengi tulisha yapata zamani. Sasa kilichobakia ni kujua kuwa hakuna haja ya kuhangaikia mambo ambayo tunayo tayari. Tulenge mambo ambayo tunayahitaji au kwa maneno mengine twende katika ngazi nyingine katika matakwa. Tatizo lililopo mimi nadhani ni kuchanganya yale matakwa tuyatakayo ya muhimu na yale matakwa ambayo tunadhani tunayataka.
Tatizo pia ni kwamba tunaongozwa katika chi yetu itupayo uwanja wa kutimiza matakwa na viongozi wanao dhania tu. Nafikiri inabidi tufikie wakati ambao tutapata viongozi watuongozao katika safari hii ya kutimiza matakwa wanaojua na sio kudhania tu.Kiongozi anayejua atajua kutumia watu wote katika hamu zao tofautitofauti za kutimiza matakwa kujenga mfumo ambao ni mzuri katika kutimiza matakwa ya watu wote.

Sun Tzu katika kitabu chake cha The Art Of War anasema:
The skilful employer of men will employ the wise man, the brave man, the covetous man, and the stupid man. For the wise man delights in establishing his merit, the brave man likes to show his courage in action, the covetous man is quick at seizing advantages, and the stupid man has no fear of death.

Mtumiaji mzuri wa watu ataajiri mtu mwenye busara, mtu shujaa, mroho wa vitu,na mjinga. Kwa sababu mwenye busara hupenda kujulikana ana busara, shujaa hupenda kuonyesha ushujaa, mroho ni mwepesi kudaka upenyo wa kujipatia, na mjinga haogopi kufa.

Nilipenda mfano wake huu kwa sababu alionyesha kuwa katika vita mjinga na mwenye busara wote ni muhimu. Mimi nasema katika vita yetu hii ya kujikomboa matakwa yetu wote ni muhimu. Na yakijulikana na tukiwa na madereva wanaojua barabara yatazaa jamii ambayo iliyoendelea , inayotatua matatizo yake bila kuomba msaada wa kuvutwa. Kwani katika kutimiza matakwa yako unatimiza na matakwa ya wakuzungukao. Na kama barabara inajulikana daima hatua itakuwa ni mbele na kwa mwendo mzuri.

Katika dunia ya leo ambayo Afrika, tanzania na mtu mweusi ametumiwa sana kutimiza matakwa ya wengine ni muhimu Afrika,Tanzania na mimi nawewe tupate matakwa yetu. Hivyo basi tuyajue matakwa yetu.

Sun Tzu pia anasema:
Knowing the enemy enables you to take the offensive, knowing yourself enables you to stand on the defensive.Attack is the secret of defence;defense is the planning of an attack.
Ukimjua adui unaweza kumshambulia, ukijijua unaweza kujilinda. Kushambulia ni siri ya kujilinda; kujilinda ni kupanga kushambulia.

Narudia tena:
HIVI WEWE UNATAKA NINI?

Haya nawaacha wakati mawazoni nikiendelea kufikiria haya maisha tuliojikuta tumezaliwa na kuishi katika mstari wa mbele vitani kama Eddy Grant aelezeapo hapa chini katika wimbo Living on the frontline

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP