Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Nyama Ya Bata ni Tamu, lakini......

>> Tuesday, January 23, 2007



Watu husema kuwa ukifuatilia nyendo za bata ,ni vigumu kula nyama yake. Vilevile inasemekana ukijua nyuki anatumia viungo gani kukamilisha utamu wa asali, unaweza kuona kinyaa kujilamba.

Swali:
Lakini hivi unafikiria ni kwanini huoanishi mbogamboga zilizo mea wakati ziko pale jikoni na uozo wa mbolea, mboga hizo zilipofyoza rutuba?

Sawa labda wewe unatumia mbolea za chumvichuvi na makemikali mengine ya stawishayo mboga.

Je, mbona huoanishi makemikali na kinyaa au sumu ziwezazo kukuathiri wakati unapata shibe?

Binadamu ni mtu ambaye anaweza kubadilishwa mawazo. Binadamu kwa bahati mbaya anaweza akapandikizwa imani na mawazo hata yeye bila kujijua.Kikubwa pia ni kwamba binadamu tunaunganisha mambo kipicha. Na mara nyingi si ukweli yale mambo tufikiayo hatima ya akili ya common sense, kutokana na picha tuziungazo kutokana na fikira tu zisizo na uthibitisho. Siamini kwamba kula nyama ya bata ni uchafu kwa sababu tu imeaminika kuwa anakula uchafu. Siamini asali ni chafu kwa sababu sijui nyuki alitoa wapi siri ya asali utamu kunoga.

Nachojua ni kwamba kama sisi tumeumbwa kutoka kwenye udongo na tukifa tunarudi kwenye udongo, basi tulapo mimea inayofyonza udongo kwenye kupata shibe, maana yake sisi ni wala watu.Au?

Dondoo:
Ushasikia jinsi Nguruwe apigwavyo vita?Je, ushasikia jinsi ng'ombe apigwavyo vita?Je , unakumbuka kuwa konokono asemekana safi sana na popo kunasehemu wanawala bila kuwapika?Nachojaribu kusema ni kuwa kila jamii si lazima isimzimie samaki nchanga.


Kumtengenezea picha nzuri binadamu katika mawazo ni moja ya siri na kazi makampuni karibu yote duniani yanafanya. Utakuta huyu atakwambia haya maji ya chupa ni Perrier, hii chupi ni Gucchi iliakutengenezee katika mawazo kuwa ni ya thamani zaidi kuliko nyingine. Lakini mwingine atakudaka kwa kukustua kua achana na gucchi na malebo mengine hayana thamani yoyote zaidi nunua yangu ya bei chini isiyo na lebo. Huyu atangazae kutokuwa na lebo na atangazaye lebo wote wanacheza mchezo mmoja wa kukudaka . Wote wako katika mchezo wa kuuza na hawawezi kuuza kama hawajakudaka.Cha muhimu ni kwamba je, wanacheza mcho wa kihalali katika kukujenga kimawazo?Wamarekani wanaimba tokea utoto nchi yao ndio bora kuliko zote. Wauza madoli na mpaka sigara ilikuwa kawaida kabisa , kama sio kawaida kabisa kulenga watu tokea watoto. Kuwaanda kimawazo kujua nini wazinguke nacho.

Sasa nini:

Mimi kama Mtanzania ningependa Tanzania kama nyama ya bata ijulikane kuwa ni tamu.

Sasa kwanini Tanzania haijulikani?

Tanzania tutake tusitake haijulikani kama inavyo stahili.Tanzania ni nchi yenye mambo mengi.Ni nchi inayopendeza. Lakini bado watu wanafikiri mlima Kilimanjaro uko Kenya.Halafu jiulize tu kama kitu kilichowazi kama mlima Kilimanjaro hakijulikani kiko Tanzania ni nini kinajulikana basi. Nasikitika kwamba ukiwauliza watu wengi duniani, cha kwanza watakachosema ni magonjwa au njaa.

Kwa nini Kenya inajulikana kuliko Tanzania?

Naweza sema ni kutokana na kuwa katika mfumo wa kibepari muda mrefu ukihusisha mbinu za kisoko za kibepari tokea zamani.Mbinu hizo ikiwa ni kujitangaza kwa namna ya kulenga pato. Mbinu zake ni nyingi lakini moja isaidiayo Kenya ni michezo.Kwa mfano hakuna mashindano ya mbio yenye kusifika ambayo watataka kuyaendesha bila kuwa na timu ya Kenya na Ethiopia. Kwa sababu hakuna atayeshinda atakayeaminika kashinda kikweli bila ya timu ya Kenya kushiriki mbio za masafa marefu. Ni sawa na mtu ashinde mbio za masafa mafupi kama mita 100 bila ya kuwa na washindani kutoka Marekani.Likifanyika hilo, ushindi wako hautathaminika.

Lakini ukimsoma Naomi Klein katika kitabu chake cha NO LOGO
utakubaliana naye mambo mengi kuhusu matumizi mabaya ya lebo. Lakini mimi nafikiri kuwa Tanzania, Afrika hata matombo kama jina lituwakilishalo linahitaji kung'arishwa.
Tanzania kama nchi naamini inastahili jina zuri .Na ni lebo (brand)tujihusishayo nayo tutaketusitake.

Bahati mbaya vyombo vingi vya taaluma kuanzi shule , dini hata maongezi yako na yule yanapanda mbegu zakutojiamini kuwa kifuambele kama Waafrika, Watanzania nk.Naamini watu weusi tuna kazi ya kungoa mimea yakutojiamini na ya kujipenda.Pale ambapo vyombo vya wenzetu vinapozidi kutuhusisha na njaa na magonjwa, ni sisi tunaohitajika kuweka sura mpya ya ukweli, kujenga sura mpya ya taifa litakalo tufanya tujivunie.

Nashukuru siku hizi ni kawaida kuona watu wamevaa mashati ya Tanzania.Kwa maana ilikuwa si muda mrefu watu wengi waliona ni ujanja kuvaa bendera za nchi nyingine kama Marekani na Uingereza. Na kwa baadhi ya niliowahi kuwauliza walisema kuvaa ya bongo ni nishai.Ingawa kuna ukweli kuwa yalikuwa haya patikani sana si kipindi kirefu kilicho pita.

Baada ya yote haya nakubali Tanzania tunamatatizo mengi. Lakini Marekani , Uingereza na Saudi Arabia wanayo pia. Sasa kwanini sisi tu ndio tukubali mpaka ambayo hatustahili. Kama ujinga, sisi si wajinga.

Lakini hivi kama Tanzania ni bata , nyama yake ni tamu?

Business in Tanzania

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP