Mtakatifu SIMON KITURURU - MAWAZONI

FALSAFA na WAZO ndani ya neno - DUH!

Hivi Mambo ni YaleYale tu! Unaweza kujinasua kutoka katika mduara?

>> Friday, January 26, 2007


Nimesikia watu wengi wakisema kuwa kiini cha matatizo mengi kuendelea kuwepo ni kwasababu watu hawajifunzi kutoka kwenye historia.Ninakubaliana na hilo. Ukianzia kwenye umaskini, matatizo ya rushwa, uongozi ovyo, na mengineyo ,yanajirudiarudia tu kila kukicha kutokana na kutojifunza.Ukichora umbo la mrudiano utapata mduara. Lakini pamoja na wengi kuamini hivyo, hii haina maana kuwa haiwezekani kuvunja mduara wa kurudiarudia makosa. Ila katika swala la kuvunja mduara huu kunatakiwa fikira safi, dhamira na wadau kujua wanafanya nini na tatizo liko wapi.

Nilipingana na baadhi ya watu waliokuwa wanadai CCM sasa ishavunja wapinzani na hivyo hakuna litakalo badilika.Walidai kuwa mduara wa uzembe ushaanza kuingia katika mzunguko wa pili chini ya CCM.Na walidai kuwa mzunguko huu hautakwisha , kamwe. Nilipinga wazo hilo kwa sababu kubwa moja. Naamini kila siku hutoa nafasi mpya ya kubadili mwelekeo. Kila siku hutoa shule kwa wakereketwa , kwa watu wengine ambao wanaweza kubadili mambo. Naamini kila siku inatoa mwanya wa wapinzani kujijenga tena.
Kuna kipindi nilikuwa nafananisha utawala wa CCM na utawala wa kifalme wa Uingereza. Ingawa ni vigumu kufananisha historia ya nchi mbili hizi, bado nilipata mwanya wa kustukia ni jinsi gani hata mzunguko wa siasa za Uingereza uliweza kubadilishwa kutoka katika ule wa mfalme kuwa na nguvu zote mpaka wa leo ambao mfalme/malkia yuko kama simbo tu.Na baada ya Waingereza kuvunja mduara haujarudia tena.Hivyo naamini CCM pamoja na mabavu sasa , hainamaana kuwa haita banwa.Na CCM kuwapo na nguvu sana katika nchi kuliko vyama vingine ni mapungufu na sio jambo bora kwa Taifa.

Kwa Uingereza walitokea akina Oliver Cromwell ambao kwa kasheshe zao waliweza kuisababisha Uingereza kuwa republic kwa kujaza zaidi nguvu kwa watu na kuzitoa kwa mfalme. Na naamini kama CCM itafikia kujisahau kwa sababu ya kukosa upinzani wa maana , watatokea akina Oliver Cromwell wa Tanzania ambao watasitisha Utawala utawaliwao na CCM na kuleta uwezo kwa watu na bunge ambalo lina uhai na nguvu ya kupinga, kusawazisha na kuelekeza taifa la Tanzania wananchi watakako.


Swali:

Tunapozungumzia kuwa huu mduara(vicious circle) hauvunjiki tunamaanisha nini?

Wengi wetu tukiwa tunaongelea mduara wa mapungufu , tunatumia mifano kama;masikini huzaa maskini , na kupata vitukuuu maskini na kuendelea.Afrika inazalisha viongozi hovyo ambao hurisisha wengine ovyo na mpaka karne ijayo itakuwa ovyo.Tunasema hivyo kwa kuamini kuwa hakuna kitakacho badilika. Tunasema hivyo kwa sababu tumekata tamaa.

Swali:
Je, tunasahau ni mambo mangapi tumeyabadili Afrika ambayo hayawezi kurudia?

Je, tunasahau kuwa ni mambo mengi tu hata katika udongo /ardhi tuikanyagayo tushayatendea mambo ambayo haiwezekani kurudisha katika hali iliyo kuwepo zamani?

Tukijaribu kujikumbusha mambo madogo madogo, naweza kusema siamini kama uchifu utarudia hali yake ya zamani Tanzania. Naamini hata ukabila hauwezi kurudia hali yake ya zamani.Na mambo mengine mengi tu. Sasa kama imewezekana kwa Watanzania kuvunja kwa kiasi kikubwa baadhi ya mambo na ni vigumu kuona kuwa yatarudia tena, naamini mambo mengine mengi zaidi yanaweza kuvunjwa yasirudie.Kama Tanzania tumeweza kuifanya kiswahili lugha ya taifa basi tunaweza kuondoa rushwa kama tabia ya taifa.

Tatizo ambalo ni la kibinadamu niliogopalo nikusahau yaliyopita . Desmond Tutu amelisema kuwa waafrika kusini sasa hivi wanapoteza mwelekeo. Wanapoteza njia ya wapi wanakwenda.Ukifikiria jinsi walivyokuwa wanapigania kujitawala juzi juzi , nivigumu kuamini wanaweza kujisahau mapema namna hii.

Lakini utashangaa ikiwa baada ya karne kadhaa Watanzania nao wakawa wamesahau mpaka kiswahili? Inaweza kuonekana kama ni hoja ya ajabu isiyowezekana, ila bila mikakati kupoteza mwelekeo kupo. Na hili ni jambo ambalo ningependa Watanzania tuwetunahakikisha hatulisahau.DUh !Nimemkumbuka huyu Askofu Tutu. Ngojea nimuachie Miles Davis anisaidie kumenzi hapa kwa kibao TUTU


Tukiongelea rushwa. Naamini kabisa rushwa tuliyokuwa nayo leo hii ni ya kiasi ambacho hakijawahi kuwepo katika historia ya Watanzania. Hivyo sioni haja ya kuacha kuipiga vita kwa kisingizio kuwa itajirudia tu. Pia naamini kila tatizo laweza kutafutiwa dawa yake ya kienyeji. Kila tatizo ni changamoto ya jawabu. Tatizo la Tanzania linaweza likapatiwa dawa ya Kitanzania.Si lazima kila wakati tutumie dawa kutoka nje.



Swali:
Lakini kwanini ni rahisi kujikuta uko ndani ya mduara bila njia ya kutokea?.

Je , ukizaliwa masikini maana yake utafariki masikini pamoja na vizazi vyako vyote?


Jibu ni ;sio ukweli.

Sasa inakuwaje kuwa walio wengi tuliotokea katika familia masikini tunaendelea kuwa masikini?

Nafikiri jibu liko kwenye ukweli kuwa binadamu pamoja na janja yake anahitaji msaada. Anahitaji mfumo wa kumsaidia ilikuweza kupiga baadhi ya hatua.Binadamu ni kiumbe ambaye daima huhitaji msaada. Mfumo unaoweka dunia katika hali iliyopo sasa hivi husaidia wenyenavyo kuongezewa na wasionavyo kuporwa hata walivyo navyo wasipo angalia. Ingawaje inasemekana hili ni jambo lililozungumziwa hata kwenye biblia, mimi siamini hivyo. Mimi naamini kuwa kila hatua au msingi mtu aupigao ni msingi umuwezeshao kupiga ile hatua moja zaidi(extra step/mile) ambayo haionekani kirahisi. Kwa matajiri ni rahisi kupiga hatua ile moja zaidi kutokana na mfumo uwalindao. Kwa maskini hata kama unawazo fulani huanzii kwenye mstari mmoja na matajiri. Ukienda benki, wewe ni rahisi kukosa mkopo wakati tajiri ambaye haitaji mkopo ndio akapewa mkopo. Ukienda kuomba kazi ni hivyo hivyo. Lakini mimi navyojua ni kwamba, matajiri hujisahau, na pia hufikia wakati ambapo wanakosa moyo wa kuendelea kujiimarisha. . Maskini kwa kujijenga taratibu hufika. Hatua kwa hatua tutafika kama tunakumbuka tunako toka. Msingi utazidi kuimarika kama tunajua kuwa huu ni msingi utuwezeshao kuhimili na kutusaidia kujijengea mfumo ambao utatusaidia kukata mduara dhaifu na kuendelea mbele.
Tusaidiane kufanya vizuri tuwezavyo, au kama FEMI KUTI akwambiavyo, DO UR BEST

0 KOMENTI a.k.a Maoni. :-(:

Idumu Jumuiya Ya Wanablogu Tanzania


Photo Sharing and Video Hosting at Photobucket

Partner

save mt. Kenya campaign
In partnership with africapoint.com

Taswira BANANGENGE

  © Blogger templates Romantico by Ourblogtemplates.com 2008

Back to TOP